Uteuzi wa mjumbe wa Baraza la kipapa la kutangaza Watakatifu
Kardinali António Augusto dos Santos Marto,Askofu Mstaafu wa Leiria-Fátima Ureno ni mjumbe wa Baraza la Kipapa la juwatangaza watakatifu.
Na Angella Rwezaua; - Vatican.
Jumatano tarehe 15 Februari 2023, Baba Mtakatifu amemteua mjumbe wa Baraza la Kipapa la kuwatangaza watakatifu kwa Kardinali António Augusto dos Santos Marto, Askofu Mstaafu wa Leiria-Fátima Ureno.
Maombi ya kung'atuka
Na wakati huo huo, Baba Mtakatifu Francisko amekubali maombi ya kung’atuka katika Ubalozi wa Vatican katika Jamhuri ya Dominica na Mwakilishi wa kitume wa Porto Rico, yaliyowakilishwa na Askofu Mkuu Ghaleb Bader, wa kiti cha Matara ya Numidia.
15 February 2023, 16:24