Tafuta

2023.09.02 Papa akutana na maaskofu,mapadre,watawa kike na kiume na wahudumu wa kichungaji huko Mongolia. 2023.09.02 Papa akutana na maaskofu,mapadre,watawa kike na kiume na wahudumu wa kichungaji huko Mongolia.  (Vatican Media) Tahariri

Mnong'ono katika ukimya wa nyika

Mkurugenzi wetu wa Tahariri anatoa maoni yake kuhusu utume wa Kanisa dogo la Kikatoliki nchini Mongolia,ambalo kwa maneno ya Papa Francisko aliwahimiza kusikiliza minong'ono ya Mungu mioyoni mwao.

Na Andrea Tornielli.

Katika maneno ambayo Papa Francisko alielekeza kwa Kanisa la Mongolia, dogo kwa idadi lakini kubwa katika upendo, kuna mawazo ya thamani, yenye manufaa zaidi ya mipaka ya nchi hii ambapo macho yamepotelea kwenye upeo wa nyika. Kwa Kanisa hili ambalo bado changa, Mrithi wa Petro alikumbusha ni nini maana utume, yaani, “kutumia maisha ya mtu kwa ajili ya Injili.” Alisema kwamba, hasa kwa sababu alifanya uzoefu wa maisha yake mwenyewe wororo wa upendo wa Mungu, Mungu ambaye alijifanya kuonekana, kugusa katika kukutana na Yesu,  habari njema iliyokusudiwa kwa watu wote, Kanisa haliwezi kuacha kupeleka tangazo hili la “kufanyika mwili katika maisha na ‘kuinong'oneza’ katika moyo wa watu binafsi na tamaduni.”

Ziara ya Kipapa Nchini Mongolia
Ziara ya Kipapa Nchini Mongolia

Taswira ya “kunong’oneza moyoni” kwa namna ya pekee inasisimua. Ukristo haukuenea kupitia vita vya kiutamaduni au matangazo makubwa; wala kwa upande mwingine  kwa njia ya malazi ya dini hiyo ya ubepari, inayojumuisha ibada, mila na maisha ya utulivu ambayo tayari yameshutumiwa na Charles Peguy. Ni tangazo la kushuhudia kwanza na maisha ya mtu, na hivyo kuinong'oneza kwenye mioyo ya watu na tamaduni. Kitenzi cha “kunong'ona” kinakumbuka kifungu hicho kutoka Kitabu cha Kwanza cha Wafalme, ambapo Mungu hajidhihirishi kwa nabii Eliya katika tetemeko la ardhi au moto, lakini kwa mnong’ono wa upepo mwanana.”

Bikira Maria anaheshimiwa sana katika Kanisa la Mongolia
Bikira Maria anaheshimiwa sana katika Kanisa la Mongolia

Ni mrejesho tu wa ushuhuda ambao unaweza kuvutia kweli. Si kwa bahati mbaya kwamba Friedrich Nietzsche hivyo aliwashutumu Wakristo wa wakati wake kuwa: “Kwa imani yenu, nyuso zenu zimekuwa na madhara zaidi kuliko sababu zetu.!” Kwa hiyo Njia ya upendeleo wa ushuhuda, kama inavyoonekana na ambayo inafumbatwa katika uhalisia wa Kanisa dogo la Mongolia, ni upendo. Papa Fransisko amewaalika Wakatoliki wa nchi hiyo daima kubaki katika kuwasiliana na uso wa Yesu ili kurejea daima katika mtazamo ule wa asili ambao kila kitu kilizaliwa. Kwa sababu, vinginevyo, hata kujitolea kwa uchungaji huendesha hatari ya kuwa na utoaji wa huduma tasa, katika mfululizo wa hatua zinazofaa, ambazo huishia kwa kutosambaza tena chochote.”


Papa Francisko kisha alisisitiza kuwa Mnazareti, akiwatuma watu wake kwenye utume, hakuwatuma “kueneza mawazo ya kisiasa, bali kushuhudia kwa maisha yao mapya ya uhusiano na Baba yake, ambaye alikuja na Baba yetu,”  hivyo kuchochea udugu thabiti na kila mtu.” Kwa njia hiyo Kanisa lililozaliwa kutokana na mamlaka hii ni maskini, halitegemei rasilimali, miundo na upendeleo wake lenyewe, halihitaji mkongojo wa nguvu, bali “linategemea tu  imani ya kweli, juu ya uwezo wa kunyang’anya silaha, na silaha  za Yeye Mfufuka, mwenye uwezo wa kupunguza mateso ya wanadamu waliojeruhiwa.”

Wamisionari nchini Mongolia ni Injili uliyo hai
Wamisionari nchini Mongolia ni Injili uliyo hai

Ndiyo maana, Papa Francisko aliongeza kusema serikali na taasisi za kiulimwengu “hazina chochote cha kuogopa kutokana na utendaji wa uinjilishaji wa Kanisa, kwa sababu halina ajenda ya kisiasa ya kufuata, lakini linajua nguvu ya unyenyekevu tu  wa neema ya Mungu na Neno la huruma na ukweli, wenye uwezo wa kukuza wema wa wote.” Ni maneno yenye maana sio tu kwa ajili ya nchi kama Mongolia, ambapo heshima kwa dini tofauti ina utamaduni wa karne nyingi, lakini pia kwa “majirani” wake wakubwa wanaopakana nao.

02 September 2023, 14:20