Juni 5-6,Kard.Zuppi atakuwa mjini Kyiv,Ukraine kwa utume
Kuanzia tarehe 5-6 Juni 2023,Kardinali Zuppi atatimiza ziara yake huko Kyiv kama ilivyokuwa tayari imetangazwa kwa ombi la Baba Mtakatifu.“Lengo msingi ni kusikiliza kwa namna ya kina Mamlaka ya Ukraine uwezekano wa kufikia njia za amani na kusaidia ishara za kibinadamu ambazo zinachangia kupungunza mivutano.”
Na Angella Rwezaula, - Vatican.
Kufuatia na kile kilichokuwa kimekwisha tangazwa mwanzo na Vatican, taarifa nyingine imetolewa kuwa katika siku ya tarehe 5 na 6 Juni, 2023, Kardinali Matteo Zuppi, Askofu Mkuu wa Bologna na Rais wa Baraza la Maaskofu katoliki nchini Italia (CEI) atatimiza ziara yake huko jijini Kyiv nchini Ukraine kufuatia na mwaliko alioombwa na Baba Mtakatifu Francisko hivi karibuni.
Huu ni mpango ulioanzishwa ambao ni wenye lengo kuu la kutaka kusikiliza kwa namna ya kina Mamlaka za Ukraine katika kutafuta haraka iwezekanavyo njia za kufikia hali ya amani na kisaidia ishara za kibinadamu ambazo zinachangia kupunguza mivutano.
05 June 2023, 11:06