Tafuta

Kardinali De Donatis atoa shukrani kwa Papa Francisko kufuatia na barua aliyowaandikia makuhani wa Roma kuwatia moyo katika nyakati hizi mpya za janga la virusi Kardinali De Donatis atoa shukrani kwa Papa Francisko kufuatia na barua aliyowaandikia makuhani wa Roma kuwatia moyo katika nyakati hizi mpya za janga la virusi 

ITALIA:Kard. De Donatis amshukuru Papa kwa barua aliyowatumia makuhani wa Roma!

Kufuatia na barua ya Papa Francisko aliyo waandikia Makuhani wa Roma Barua,tarehe 30 Mei 2020,Makamu wa Papa Kardinali De Donatis ametoa shukrani kwa niaba ya Baraza la ushauri wa kiaskofu na makuhani wote.

Na Sr. Angela Rwezaula- Vatican

Kardinali Angelo De Donatis, Makamu wa Papa wa Jimbo Kuu la Roma amemshukuru Papa Francisko kwa ajili ya Barua yake aliyowatumia makuhani wa Roma na kwamba ni zawadi yenye thamani ambayo inaongezwa katika utimilifu wa safari ya Pasaka. Barua hiyo ameiandika kuwatia moyo na kuwaalika katika tafakari ya kipindi hiki cha dharura ya kiafya kutokana na virusi vya corona.

Kwa mujibu wa Kardinali katika barua hiyo  anaelezea shukrani zake za dhati kwa Papa na kwa niaba ya Baraza zima la ushauri wa kiaskofu  na kwa makuhani wote wa Kanisa la Roma. “Tunakutakia mema. Tunao utumbuzi wa ushuhuda wako  wa ubaba na ukaribu  wako mbele ya mapadre wote na watu wa Mungu ambapo umejionesha katika kipindi hiki kigumu cha janga”. Kardinali anaandika.

Aidha amebainisha ni kwa jinsi gani wameweza kupata nguvu na msaada katika uweza wa sala zake  na hata kwa ajili ya kumsikiliza Misa zake za kila siku na katekesi za kila wiki. “Maneno ya Papa Francisko anasisitiza Kardinali De Donatis, “yametoa mwangwi kwa mara nyingine katika dunia nzima kwa kurithisha  matumaini na imani hata wale wasio waamini, licha “kelele kuu katika njia zetu na  viwanja vyetu”

“Katika uongozi wako wa kibaba na udhihirisho wa Mfuasi wa Petro umetuimarisha imani yetu wakati wa kipindi hiki cha kuchanganyikiwa” anaandika tena  Kardinali De Donatis na akimshukuru kwa ajili ya kupokea kwa imani hisia, mawazo na maombi ya mapadre wote na kuweza kuyawasilisha yote kwa Bwana!

Jitihada za makuhani wa Jimbo Kuu Roma  anaandika siku zote zinabaki kujiruhusu “kuumbwa kwa upya na kuwashwa ndani ya mioyo kwa upole na huruma, kwa unyenyekevu na ukuu wa uvumilivu katika uhai wa utendaji na wa mshikamano, ujasiri, lakini pia kutorohusu sintofahamu na tofauti,  kukataa, kinzani, wasiwasi na uzushi na badala yake kufungamana”. “Asante Papa kwa sababu unatualika tuangalie siku zijazo kwa ujasiri na mtazamo wa imani.” Amehitimisha Kardinali De Donatis barua yake kwa Papa.

31 May 2020, 13:50