Tafuta

WATU ASILIA WANASHIRIKI KATIKA COP28 HUKO DUBAI WATU ASILIA WANASHIRIKI KATIKA COP28 HUKO DUBAI  (AFP or licensors)

COP28:Caritas inaakisi umuhimu wa kupitishwa Mfuko wa fidia ya Hasara na Uharibifu

Wakati viongozi wa dunia,mashirika ya kiraia na makundi ya kidini wakikusanyika huko Dubai katika Mkutano wa 28 wa Wanachama kushughulikia mzozo wa Tabianchi,Katibu Mkuu wa Caritas Internationalis alizungumza juu ya matumaini ya Mkutano huo hasa muhimu uliotekelezwa na juhudi za Caritas zilizofaulu za kuweka Mfuko wa fidia ya Hasara na Uharibifu kwenye ajenda ya COP28.

Na Linda Bordoni na Angella Rwezaula, - Vatican.

Akihutubia na kukiri kwa kiasi fulani mtazamo wa pamoja wa mikutano ya COP kama "maduka ya  mazungumzo kwa watu wenye nguvu," Alistair Dutton, Katibu Mkuu wa Caritas Internationalis, aliakisi maendeleo ya kweli katika kushughulikia masuala ya Mabadiliko ya Tabianchi yaliyoonekana katika matukio kama hayo yaliyotangulia, hasa ile ya kihistoria  ya COP15 mjini Paris. Hayo aliyathibisha mwakilishi wa Caritas Internationalis, katika mahojiano na Radio Vatican katika maandalizi ya tukio hilo, akiwa huko Dubai kama "Mtazamaji"  yaani  mmoja wa wadau wasio wa chama katika kilele cha Mkutano ambao una jukumu muhimu katika kufikia malengo ya mabadiliko ya hali ya tabicha duniani. "Kwetu sisi kama waangalizi (...) ninadhani tunaenda sana kwa matumaini ya kushawishi wazungumzaji na kujaribu kupata maendeleo makubwa" alisema. Kwa mujibu wake Dutton alibainisha kuwa Ni wazi, COP huko Paris ilikuwa wakati muhimu sana ambao viongozi wa dunia walifikia makubaliano ya kimataifa ya kujaribu kuweka viwango vya juu vya joto chini ya digrii moja na nusu, ambacho ni "kigezo cha COP zote tangu".

COP28 inakuja baada ya Laudato si na Laudate Deum

Mkutano huo ulikuja kufuatia na uchapishaji wa Waraka wake Laudato Si,( Laudato Si,) wa Papa Francisko na wakati huu unakuja baada ya Waraka mweningine wa Laudate Deum (Laudate Deum.) Kwa hiyo "Kama Laudato sì alikuwa na  mwito wa kuchukua hatua juu ya mabadiliko ya hali ya Tabianchi akisema jinsi tatizo lilivyokuwa kubwa, kuchanganyikiwa kwa Papa Francisko katika Laudate Deum kunaonekana kabisa," aliongeza. "Ikiwa Laudato sì alikuwa na mwito wa kuchukua hatua juu ya mabadiliko ya hali ya tabianchi  akisema jinsi shida ilikuwa kubwa, na kufadhaika kwa Papa Francisko lwa Laudato Deum kunaonekana kabisa." Tunashiriki katika Mkutano huu, "tukiangalia kiukweli kujaribu kuongeza mara mbili juu ya ahadi ambazo zimefanywa hapo awali na kuhakikisha kuwa serikali zinatimiza ahadi hizo na kuweka rasilimali zinazohitajika,"Katibu Mkuu  wa Caritas Internationalis alieleza.

Mfuko wa Hasara na Uharibifu

Katika mwanzo mzuri mnamo Alhamisi,  tarehe 30 Novemba, COP28, ilianza kupata ushindi wa mapema na wajumbe kupitisha hazina mpya ya kusaidia mataifa maskini kukabiliana na majanga ya hali ya tabianchi ya gharama kubwa. Kupitishwa kwa Mfuko wa  kufiada Hasara na Uharibifu ilikuwa kati ya vipaumbele vya Dutton katika Mkutano huo na alielezea jinsi  ambavyo amekuwa akihusika katika kukuza na kuanzisha kama jibu la lazima kwa baadhi ya vipengele vya mgogoro wa hali ya  tabianchi. Alikumbuka kuwa miaka miwili iliyopita alipokuwa Caritas Scotland (SCIAF) alihudhuria COP huko Glasgow. Pamoja na "Stop Climate Chaos Scotland" (muungano tofauti wa zaidi ya mashirika 60 ya kiraia yanayofanya kampeni pamoja juu ya mabadiliko ya hali ya tabianchi nchini Scotland), na pamoja na serikali ya Scotland, alisema walifanikiwa kupata suala la Mfuko wa fidia ya Hasara na Uharibifu sana kwenye ajenda. “Mwaka huu tunatarajia kuwa Mfuko wa Hasara na Uharibifu uanzishwa na utaratibu wa watu kupata fidia hiyo inayohitajika,” alisema.

Kupunguza matumizi ya nishati ya mafuta

Suala jingine muhimu Dutton alisema anatumai litapata maendeleo makubwa kuhusiana na kupunguzwa kwa matumizi ya mafuta ambayo ni "muhimu kabisa katika kudhibiti utoaji wa kaboni dioksidi na gesi zingine chafuzi." "Kwa hivyo inaweza kuonekana kama 'duka la kuzungumza' kutoka mbali, lakini nadhani inabidi tuingie katika hili tukiwa na matumaini na kudhamiria kwamba tutaona maendeleo makubwa," alishangaa. "Lazima tuingie katika hili tukiwa na matumaini na kudhamiria kwamba tutaona maendeleo makubwa."

Mabadiliko ya Tabianchi na migogoro

Dutton pia aliakisi muunganisho wa mabadiliko ya hali ya tabinchi na migogoro, akisisitiza kwamba matukio yote mawili yanaathiri kila mmoja. Aliashiria tukio ndani ya Mkutano huo uliopangwa kufanyika tarehe 3 Desemba 2023 ambalo linajumuisha "Amani" iliyounganishwa na sera ya mabadiliko ya hali ya tabianchi. Ni mara ya kwanza katika historia ya mkutano wa mabadiliko ya hali ya tabianchi wa kila mwaka ambapo watoa maamuzi wanaitwa kuzingatia uhusiano huu na kushughulikia changamoto muhimu. Kiongozi huyo wa Caritas alisema ni fursa kwa wakati mwafaka ya kuongeza ufahamu na kuchukua hatua kwani ni wazi kwamba migogoro na mabadiliko ya tabia nchi yana uhusiano mkubwa: "Unakwenda pande zote mbili: migogoro huzalisha mabadiliko ya hali ya tabianchi na mabadiliko ya hali ya tabianchi huleta migogoro."

Ripoti ya Caritas ya watu waliofukuzwa kutokana na mabadiliko ya tabianchi

Kwa upande wake amekazia kuwa  Caritas Internationalis imetoka tu kuchapisha ripoti kuhusu watu ambao wamefukuzwa kutoka katika makazi yao na kuhama kutokana na mabadiliko ya hali ya tabianchi, akibainisha kuwa "tunapoona hali ya hewa inazidi kuwa mbaya zaidi na isiyo ya kawaida, tunapoona zaidi na zaidi machafuko makubwa zaidi yanayohusiana na hali ya tabianchi, watu wengi zaidi wanalazimika kuacha nyumba zao na kuhama. Kwa hiyo "kadiri watu wanavyosonga, kunakuja ushindani mkubwa wa rasilimali, ambapo uwezekano mkubwa wa migogoro hutokea," alisema. "Tunahitaji kuzungumza juu ya hilo na tunahitaji viongozi wa dunia kuchukua hatua sasa ili kudhibiti Mabadiliko ya Tabianchi ili tusije kuona uhamiaji wa siku zijazo na migogoro ya siku zijazo inayotokana na ushindani wa rasilimali. Tunahitaji kuzungumza juu ya hilo, na tunahitaji viongozi wa ulimwengu kuchukua hatua sasa kudhibiti Mabadiliko ya Tabianchi ili tusione uhamiaji wa siku zijazo na migogoro ya siku zijazo inayotokana na ushindani wa rasilimali. "

Mafundisho ya Papa: Nguvu ya kimaadili ya mabadiliko

Uchapishaji wa  Waraka wa Laudate Deum, kabla  ya Mkutano huo,  Dutton alisema, ni uthibitisho wa jinsi Papa anavyojali kuhusu suala la mabadiliko ya hali ya tabianchi na matokeo yake kwa makazi yetu ya kawaida na wakaazi wake. Amezungumza kwa sauti kubwa kuhusu suala hilo mara nyingi, aliongeza, akionesha wakati dhahiri wa kutambua ni katika Laudato sì,” na alikumbuka pia jumbe nyingi alizotuma kwa viongozi wa dunia mara nyingi. Papa Francisko alilazimika ktukuwepo kwake kuliokuwa kumepangwa kufanyika katika Mkutano huo kwa sababu za kiafya, lakini anatarajiwa kutuma ujumbe kwa washiriki.  Dutton alisema anatarajia Papa kuwaambia viongozi wa dunia kwamba "tunapaswa kuchukua hatua sasa kwa manufaa ya ubinadamu, kwa manufaa ya sayari, kujali vizazi vya sasa na vijavyo." "Lazima tuchukue hatua sasa kwa faida ya ubinadamu, kwa faida ya sayari, kutunza vizazi vya sasa na vijavyo."

Ushirikiano wa dini mbalimbali

Hatimaye, Mkuu wa  Caritas Internationalis aliankisi dhamira ya Papa ya maelewano na ushirikiano wa dini mbalimbali, ambayo, alisema, inaleta uzito mkubwa kwa wito kama wa  kwaya wa haki ya hali ya tabianchi. "Nafikiri na ninatumaini kwamba atawatia moyo viongozi wa imani, imani tofauti kukusanyika pamoja na kuweka wazi kuwa watu wa dini zote wanajali jambo hili na wanaelewa uharaka wake," alisema, huku akibainisha kuwa idadi kubwa ya watu ulimwengu ni watu wa imani. “Tunasahau hilo, ninadhani, katika nchi za Magharibi za ulimwenguni pote, lakini watu wengi ni watu wa imani, na wanaelewa wajibu na uhitaji wa kufanya jambo fulani kulihusu.” Papa Francisko, sio tu atakuwa na ujumbe wazi sana juu ya haki ya hali ya tabianchi kwa kila mtu, nadhani jukumu lake na jukumu la vikundi vya kidini katika kusisitiza msingi wa maoni ya ulimwengu litakuwa muhimu katika kusaidia kusonga hatua kwa kiwango chochote. Jukumu la Papa na jukumu la vikundi vya kidini katika kusisitiza msingi wa maoni ya ulimwengu itakuwa muhimu katika kusaidia kusongesha kwa kiwango chochote mbele. zaidi,” Katibu Mkuu wa Caritas Internationalis.

02 December 2023, 13:04