Tafuta

Bendera ya Umoja wa Nchi za Ulaya. Kila tarehe 9 Mei ya kila Mwaka ni Siku ya Ulaya. Bendera ya Umoja wa Nchi za Ulaya. Kila tarehe 9 Mei ya kila Mwaka ni Siku ya Ulaya. 

Siku ya Ulaya,Askofu Crociata:kushinda vita na kushinda amani

Rais wa Tume ya Mabaraza ya Maaskofu wa Jumuiya ya Umoja wa Ulaya,(Comece) Askofu Mariano Crociata,amehimiza kutafutwa kwa umoja na kuhakikishia kujitolea kwa maaskofu wa Ulaya katika kuunda dhamiri zinzohimiza kuwajibika wakati wa kuishi.Amesema hayo katika Siku ya Ulaya iadhimishwayo kila mwaka ifikapo tarehe 9 Mei.

Na Angella Rwezaula, - Vatican.

Mwaka huu 2023 katika Siku ya Ulaya,  bado inafanyika katika mazingira ya kutisha ya vita katika ardhi ya Ulaya, na mateso ya kutisha ya kimwili, nyenzo na kiroho kwa watu wa Ukraine, na hivyo lazima kufanya hitaji la umoja na amani kuwa la haraka zaidi. Hayo yameandikwa katika taarifa, wakati wa fursa ya  Siku ya Ulaya  iadhimishwayo kila ifikapo tarehe 9 Mei ya k la mwaka na rais wa Tume ya Mabaraza ya Maaskofu wa Jumuiya ya Umoja wa Ulaya, (COMECE) Askofu  Mariano Crociata, ambaye anakumbuka jinsi, miaka 73 baada ya tamko la Robert Schuman, mmoja wa wabunifu wa Muungano wa Umoja, kwamba  kuanguka kiuchumi,  madhara ya mzozo yanazidisha sehemu dhaifu zaidi za idadi ya watu.

Kwa hiyo mbele ya kukabiliwa na  mada ya kutisha ya sasa   na sababu zilizosababisha kuzaliwa kwa Umoja, baada ya Vita vya Pili vya Dunia, pamoja na vifo na uharibifu wake, Askofu Crociata ametoa wito wa kurejesha sababu na nia ya kufuata kwa dhamira mpya ya Ulaya ambao ni umoja na amani, kama ilivyo ahadi ambayo Comece inaitafsiri na ambayo inakusudia kuchangia kupitia kuunda dhamiri inayofahamu na kuwajibika katika wakati tunamoishi.

Kujitolea kwa Maaskofu wa Ulaya kufanya kazi kwa umoja ndiyo  himizo kuu kwa Maaskofu wa  Nchi za Umoja wa Ulaya (EU) ambapo wametakiwa  kwahimize na kushirikiana na juhudi zote zitakazofanywa ili kutafuta umoja, kuondokana na migogoro na kutafuta amani, ujenzi muhimu kwa ajili ya kufanya ukuaji uwezekane kwa wote ndani ya Umoja wa Ulaya na nje ya mipaka yake.

Siku ya Ulaya
09 May 2023, 17:56