Tafuta

2019.03.12 watoto nchini Siria katika maisha ya vita na migogoro 2019.03.12 watoto nchini Siria katika maisha ya vita na migogoro 

Unicef:bado mauaji ya watoto nchini Siria yanaendelea kutokana na mashambulizi

Msemaji wa Unicef nchini Italia Bwana Bwana Iacomini amesema kwamba hata baada ya miaka 10 ya mzizozo,bado mauaji ya watoto yanaendelea nchini Siria.Msichana wa miaka 12 ameuwawa kutokana na mashambulio Jumapili tarehe 31 Januari 2021 na watoto wengine 3 waliuwawa siku mbili zilizopita.

Na Sr. Angela Rwezaula – Vatican.

Kulingana na ripoti kutoka ofisi za UNICEF,  kuhusiana na nyanja hiyo msichana wa miaka 12 aliuawa Jumapili tarehe 31 Januari  katika shambulio huko Azaz, kaskazini mwa eneo la vijijini  la Aleppo. Watoto wengine wawili ni miongoni mwa makumi ya waliojeruhiwa, mmoja wao akiwa chini ya mwaka mmoja. Siku mbili zilizopita, watoto watatu walifariki katika mlipuko katika mji wa Afrin, pia kaskazini mwa eneo la vijijini la Aleppo. Amesema hayo Bwana Andrea Iacomini, msemaji wa UNICEF nchini Italia.

Kwa mujibu wa msemaji huoyo amesema “Mashambulio haya ya hivi karibuni, kwa huzuni yanatukumbusha kuwa vurugu zinaendelea nchini Sria na kwamba watoto wanaendelea kuwa katika hatari siku baada ya siku. Tangu mwanzo wa mwaka huu, watoto wasiopungua 22 wameuawa. Ni mauaji ya kusikitisha ambayo yamedumu muda mrefu miaka 10”.

Kwa mara nyingine, UNICEF inawakumbusha wahusika wote kwenye mzozo majukumu yao ya kulinda watoto wakati wote na kujiepusha na vurugu katika maeneo ya raia. Miaka kumi baada ya kuanza kwa mzozo, watoto wanaendelea kuathiriwa zaidi na uharibifu usiokuwa wa kawaida, makazi yao na vifo. Wamepoteza maisha, nyumba na utoto. Wakati umefika sasa wa ghasia nchini Siria kuisha, amehitimisa msemaji huyo.

01 February 2021, 13:56