Tafuta

Mfalme wa Ubelgiji amemwandikia Rais wa Congo DRC barua ya masikitiko ya madhara ya ukoloni nchini mwao katika maadhimisho ya miaka 60  tangu nchi ipatte uhuru wake. Mfalme wa Ubelgiji amemwandikia Rais wa Congo DRC barua ya masikitiko ya madhara ya ukoloni nchini mwao katika maadhimisho ya miaka 60 tangu nchi ipatte uhuru wake. 

Ubelgiji:Masikitiko ya Mfalme wa Ubelgiji kuhusu ukoloni dhidi ya Congo DRC!

Mfalme wa Ubelgiji Philip kwa mara ya kwanza katika historia ya nchi hiyo amewasilisha masikitiko yake ya kina ya majeraha yaliyosababishwa wakati wa ukoloni wa Ubelgiji nchini Congo DRC, barua aliyomtumia Rais wa nchi katika fursa ya maadhimisho ya miaka 60 ya uhuru wa nchi hiyo.

Na Sr. Angela Rwezaula – Vatican

Mfalme Philip wa Ubelgiji ameelezea maskitiko yake kwa madhara yaliyosababishwa na ukoloni wa nchi yake dhidi ya nchi ya Congo DRC  ikiwa ni mara ya kwanza katika  utawala wa Ubelgiji kutamka kauli kama hiyo. Katika barua yake aliyompelekea Rais Felix Tshisekedi, tarehe 30 Juni 2020   katika siku ambayo Congo inaadhimisha miaka 60 tangu kumalizika kwa ukoloni wa Ubelgiji, nchini mwao  Mfalme Phillip amesema anajutia majeraha ya kale ambayo maumivu yake yapo hadi leo kutokana na ubaguzi unaoendelea kwenye jamii.

Hata hivyo wanahistoria wanasema mamilioni ya Wakongo waliuawa, kukatwa viungo vyao ama kufa kwa maradhi wakati wakifanyishwa kazi  za suruba kwenye mashamba ya mipira yaliyokuwa yakimilikiwa na Mfalme Leopold II wa Ubelgiji. Bila ya kumtaja babu yake huyo mkuu kwa jina, Mfalme Philip ameandika kwenye barua hiyo kwamba matendo ya ukatili na unyama yaliyofanywa wakati huo ni sehemu kubwa ya kumbukumbu za pamoja kati ya Congo na Ubelgiji.

Vile vile sanamu kadhaa za Leopold II, aliyetawala kati  ya mwaka 1865 na 1909, zimechafuliwa kwa rangi au kuvunjwa na waandamanaji nchini Ubelgiji katika siku za hivi karibuni, hasa katika wimbi la hasira kubwa iliyochochewa na mauaji ya George Floyd mmarekani mweusi  mwezi uliopita katika  mikononi mwa polisi wa Minneapolis, Marekani. Suala ambalo bado linaendelea kuleta vurugu na machfuko nchini humo na kwingineko.

30 June 2020, 15:49