Tafuta

Watu wakiwa wamevaa barakoa kujilinda katika mji wa QOM nchini Iran. Watu wakiwa wamevaa barakoa kujilinda katika mji wa QOM nchini Iran. 

Iran#coronavirus:Barua kwa Papa kutoka kwa mkuu wa chuo kikuu Qom!

Mkuu wa Chuo Kikuu cha Qom nchini Iran, Alireza Alafi amemtumia Papa Francisko akisisitza kuwa mbele ya janga la corona ni kuungana kwa pamoja katika kutoa huduma ya ubinadamu.

Na Sr. Angela Rwezaula – Vatican

Shukrani kubwa kwa Papa Francisko ambaye amejionesha kujali maskini na watu wenye kuhitaji katika kipindi hiki cha janga la virusi vya corona, mapendekezo ya kina na ushirikiano, ubadilishano wa uzoefu katika taasisi katoliki kwa namna ya kuunda jumuia ya dini za mbingu katika kutoa huduma kwa ubinadamu. Ndiyo ujumbe uliomo katika barua ya Ayatollah wa Iran, Alireza Arafi, Mkuu wa Chuo kikuu cha Kimataifa cha  Qom, aliyo mtumia Papa kwa niaba ra wanachuo ambao ni Jumuiya ya wanafunzi wa Shiiti nchini Iran, Yeye ni kiongozi na porfesa maarufu.

Ubaya wa virusi vya corona na mateso

Ubaya wa kuenea kwa corona umesababisha mateso kwa nchi na mataifa yote, pia unasikitisha wasomi na viongozi wa dini. Waalimu wa dini na wanafunzi wao, wa Qom na nchini Iran, anaandika Ayatollah kuwa, wanaomba huruma ya Mungu kwa wote ambao wamepoteza maisha na uponyaji kwa wale ambao ni wagonjwa na wanatoa shukrani zao kwa Papa Francisko  na kwa wale wote wanaojali wanyonge na wahitaji huku  akisisitiza umuhimu wa kufuata mipango iliyoainishwa na mapendekezo ya wataalam na wanasayansi.

Mateso yanaleta utambuzi

Kwa mujibu wa mantiki ya dini zilizofunuliwa, ujumbe unaendelea  kupitia Shirika la Habari za Kimisionari Fides kuwa, majanga ya asili ni matukio ya mshtuko ambayo yanajaribu ubinadamu na pia yanawakilisha hali ambayo hukuza  mtu na kumpa  uwezekano wa kufufuliwa ambamo inawezekana  roho kuzaa matunda ya  huruma na kujitoa  bila kujibakiza.

Mbinu sahihi mbele ya janga kama hili  ni lazima kuepuke uwongo kati ya sayansi na dini, na lazima pia zitoe vikundi vya uongozi wa kuhamasisha na  kukuza mshikamano wa kijamii. Viongozi wa kidini na wataalimungu wana jukumu la ziada la kuimarisha misingi ya imani yao ya kulinda jamii kutokana na machafuko na migogoro, huku wakikumbuka nguvu ya milele ya Mwenyezi Mungu, katika kukuza sala na dua mbele ya Mungu, kukutana na dharura zingine za kisasa kama zile za dhuluma, ubaguzi, vikwazo vya kibinadamu, machafuko ya mazingira, vita, ugaidi, utengenezaji wa vyombo vya uharibifu.

Dhihirisho la mshikamano na uhamasishaji

Aidha Ayatollah Alireza Arafi anaongeza kuandika, katika siku hizi “tumeshuhudia dhihirisho lisiloelezeka la mshikamano maarufu na uhamasishaji ambao umeunganisha taasisi za serikali na watu wa vikundi vyote vya kidini, na umewaona wauguzi madaktari, wanafunzi, wasomi na vijana wengi, chini ya uongozi wa viongozi wakuu wa Mapinduzi ya Kiislam wakishimana na kushirikiana katika harakati za mapambano na virusi vya corona.

07 April 2020, 12:36