Tafuta

Papa Francisko amemteua Balozi wa Vatican nchini  Papua Guinea Mpya Papa Francisko amemteua Balozi wa Vatican nchini Papua Guinea Mpya  (AFP or licensors)

Papa amemteua Balozi wa Vatican nchini Papua Guinea Mpya

Ijumaa tarehe Mosi Machi 2024,Baba Mtakatifu Francisko amemteua Balozi wa Vatican nchini Papua Guinea Mpya, Monsinyo Mauro Lalli, ambaye hadi uteuzi alikuwa ni Mshauri wa Ubalozi kwa kumwinua hadhi ya Uskofu Mkuu. Pausula

Vatican News

Ijumaa tarehe Mosi Machi 2024, Baba Mtakatifu Francisko amemteua Balozi wa Vatican nchini PapuaGuinea mpya Monsinyo Mauro Lalli,  aliyekuwa Mshauri wa Ubalozi kwa kumwinua  moja kwa moja hadhi ya  Uskofu Mkuu kuwa na kupewa makao ya Pausula.

Wasifu wake

Monsinyo Mauro Lalli alizaliwa huko Atessa (Chieti) nchini Italia mnamo tarehe  17 Septemba 1965. Alipewa daraja takatifu la upadre baada ya majiundo yake mnamo tarehe 14 Julai 1990, kwa ajili ya Jimbo katoliki la  Chieti – Vasto, Italia.

Ana shahada ya Sheria ya Haki kwa pande zote mbili. Alijiunga katika Huduma ya Diplomasia ya Vatican mnamo tarehe 1 Julai 1999,  baadaye kuendelea na shughuli katika uwakilishi wa Ubalozi wa Kipapa nchini Guatemala, Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo (DRC), Msumbiji, Romania, Kroazia, India, Iraq, Yordan na  Cyprus. Lugha anazofahamu ni Kiingereza, kifarasnsa, Kireno na Kihispania.

01 March 2024, 16:53