Tafuta

2024.03.22 Tafakari ya Neno la Mungu( Lectio Divina) na Maskini katika ngzo za Mtakatifu Petro. 2024.03.22 Tafakari ya Neno la Mungu( Lectio Divina) na Maskini katika ngzo za Mtakatifu Petro.  #SistersProject

Neno la Mungu kati ya watu maskini katika safari ya Pasaka kwenye nguzo za Mtakatifu Petro

Kulikuwa na wakati wa toba kwa kuzingatia siku kuu ya Pasaka ulioandaliwa kwa watu wasio na makazi katika eneo la Vatican karibu na nguzo.Mpango huo imeandaliwa na watawa wa Klaretia ambao wamejitolea kwa muda mrefu kwa utunzaji wao wa kimwili na wa kiroho.Kuna historia nyingi za kuzaliwa upya baada ya kukutana na Neno la Mungu,wanabainisha uzoefu wao

Na Benedetta Capelli – Vatican

Kati ya vitanda vya kubahatisha, kwenye mabox ya makaratasi yatafutwayo na uchafu unaoweza kuonekana kwenye Uwanja wa Mtakatifu Petro pembeni nyakati za usiku, nguvu ya Ufufuko wa Yesu inafika hata hapo na ujumbe wake wa amani na matumaini usiomtenga mtu yeyote bali ambao unamwimarisha na kuhuisha mioyo wa wenye  huzuni zaidi. Huo ni utume ambao watawa wa Klaretian wanautekeleza wakihuishwa na karama iliyochapishwa au kuanzishwa  na mwanzilishi wa Shirika lao, Mtakatifu Antonio Maria Claret inayojikita katika shauku ya uinjilishaji na ujasiri wa kimisionari. Siku ya Jumanne tarehe 26 Machi 2024 iliwaona watawa hao katika toba na maskini kwa matazamio ya Siku Kuu ya  Pasaka, Ufufuko wa Bwana.

No wakati wa kujiandaa na kusikiliza neno la Mungu
No wakati wa kujiandaa na kusikiliza neno la Mungu

Njia inayoongoza kwenye maombi ya pamoja

“Ili kufikia mpango huo ni muhimu kutazama hatua za  nyuma.” Haya yalisemwa na Sista Elaine Lombardi, mmisionari wa Mtakatifu Anthony Maria Claret, ambaye alikumbuka jinsi miaka iliyopita katika parokia ya Torresina Roma, iliyowekwa wakfu kwa Mtakatifu Faustina Kowalska wa Huruma ya Mungu, baadhi ya vijana walianza safari muhimu kuanzia Tafakari ya Neno la Mungu (Lectio Divina) na kisha kukamilishwa na hamu kubwa ya kutaka kusaidia wengine na kwa hivyo na usambazaji wa chakula cha jioni kila siku ya Jumanne. “Tulianza chini ya Nguzo na novena ya Noeli  na  mwishoni watu wengi maskini wanaoishi huko walituomba tuendelee na mpango huo wa Tafakari na wasio na makazi mara moja kwa mwezi.  Tunashiriki Neno la Mungu ambalo kiukweli hugeuka kuwa kushiriki maisha ya mtu, jambo kuu ni kwamba watalii wengi pia husimama na kuomba pamoja nasi,” alisisitiza Sr. Elaine.

Hata mahema madogo yanaonekana katika nguzo za Mtakatifu petro wakati wa Usiku
Hata mahema madogo yanaonekana katika nguzo za Mtakatifu petro wakati wa Usiku

“Siwezi kusoma Biblia…”

Kuna historia nzuri sana ambazo tumekusanya” alisema Sr   Eliane kwa hisia. “Mmoja wao, Francis, ambaye ana historia  fulani ya maisha na anaishi mitaani, alianza kushiriki katika Tafakari ya Neno la Mungu na alikuwa na huzuni kutokana na matatizo ambayo alikuwa akikutana nayo kila siku. Siku moja, mwisho wa maombi, alinikaribia kuniomba Biblia na nikampatia ile niliyokuwa nayo mkononi na tuliyoitumia kwa ajili ya Tafakari hiyo, iliwekwa kwenye madhabahu ndogo tunayotengeneza kwa kutumia moja ya vitabu hivyo, masanduku ya maskini na mavazi tunayobeba. Aliipokea lakini Juma lililofuata akaja kuzungumza nami ili kuniambia kuwa hajui kusoma.”  Fransis alipata mtu anayemfikiria, anayemsikiliza na ambaye anaingia naye katika uhusiano na kwa sababu hiyo hakusita kumwambia mtawa huyo kwamba nyakati za maombi alizopitia na Neno la Mungu limefanya shauku ya kutaka kujua Injili na kwa hiyo kujifunza kukua ndani yake na kusoma. “Tulichukua hatua mara moja na kutafuta mahali ambapo angeweza kukuza hamu yake hii. Nadhani hii ni nzuri sana na imenigusa sana.

Ni hali hali halisi katika mji wa Roma ambapo kuna watu wengi wasio na makazi na wanasindikizwa kiroho
Ni hali hali halisi katika mji wa Roma ambapo kuna watu wengi wasio na makazi na wanasindikizwa kiroho
27 March 2024, 17:43