Tafuta

Tafakari ya VI ya Kipindi cha Kwaresima kwa Curia Romana 15 Machi 2024 Tafakari ya VI ya Kipindi cha Kwaresima kwa Curia Romana 15 Machi 2024  (Vatican Media)

Cardinali Cantalamessa:Tumaini ubadilisha kila kitu kuanzia ndani!

Kardinali Cantalamessa mhubiri Mkuu wa Nyumba ya Kipapa alitoa mahubiri ya IV ya Kwaresima mbele ya Papa na Curia Romana:kutumaini ni kama kuwa na nanga na tanga katika uzambazaji wa maisha.Huipatia mashua usalama na kuweka imara kati ya mawimbi ya bahari.Pili tumaini linakufanya usonge mbele.

Na Angella Rwezaula – Vatican.

Miujiza ya kila siku ya matumaini ilikuwa katikati ya mahubiri ya IV ya Kwaresima, yaliyofanywa na Kardinali Raniero Cantalamessa Mhubiri Mkuu wa Nyumba ya Kipapa, asubuhi, ya Ijumaa tarehe 15 Machi 2024  katika Ukumbi wa Paulo VI, mjini Vatican mbele ya Baba Mtakatifu Francisko na Washirika wake wa  Curia Romana. Kardinali Cantalamessa akiendeleza mzunguko wa kutafakari kwa makini juu ya  Mimi ni wa Kristo kutoka Injili ya Yohane, alikazia sura ya 11, iliyojikita na tukio la ufufuko wa Lazaro. Matokeo yake yalikuwa sifa ya tumaini la Kikristo kama mtenda miujiza mkuu, anayeweza kuweka maelfu ya vilema vya kiroho na waliopooza miguuni, alisema hayo, huku akirejea kipindi  kilichosimuliwa katika Matendo ya Mitume.

Kardinali Cantalamessa alisema kuwa kinachoshangaza zaidi kuhusu tumaini ni kwamba uwepo wake hubadilisha kila kitu, hata kama kwa nje hakuna kinachobadilika, akikumbuka jinsi inavyoelezwa kupitia picha zinazohusishwa na ulimwengu wa uzambazaji  kwa mfano wa nanga au tanga. Ikiwa ya kwanza ndiyo inayoipatia usalama mashua na kuiweka utulivu kati ya mawimbi ya bahari;  ya pili ndiyo inayoifanya isonge mbele. Na kwa njia zote mbili zinafanya kazi kwa habari ya mashua ambayo ni Kanisa;  na katika zile za mashua ya maisha yetu, inakusanya upepo na bila kelele huku ikibadilisha kuwa nguvu ya kuendesha au mikononi mwa baharia mzuri,  anayeweza kutumia upepo wowote, kutoka upande wowote, kuelekea upande anaotaka. Kwa hakika, Kardinali alisema kwamba “kwanza kabisa tumaini hutusaidia katika safari yetu ya kibinafsi ya utakaso kuwa katika wale wanaoitumia, kanuni ya maendeleo ya kiroho. Daima kuwa macho ili kugundua fursa za wema mpya zinazoweza kufikiwa. Kwa hiyo halituruhusu kutulia katika uvuguvugu na uvivu."

Mahubiri ya Kwaresima
Mahubiri ya Kwaresima

Zaidi ya hayo, sio tabia nzuri na ya ushairi wa ndani ambao unakufanya uote na kujenga ulimwengu wa kufikirika. Kinyume chake, ni halisi sana na ya vitendo. inatumia muda wake kila wakati kuweka kazi za kufanya mbele yako. Zaidi ya hayo, kila mara hugundua kitu ambacho kinaweza kufanywa ili kuboresha hali: kufanya kazi kwa bidii zaidi, kuwa mtiifu zaidi, mnyenyekevu zaidi, mwenye huzuni zaidi. Na inapoonekana kuwa hakuna chochote cha kufanya, tumaini bado linatuonesha kazi kwa kupinga hadi mwisho na kutopoteza uvumilivu ambapo Kardinali Cantalamessa, akimnukuu mfalsafa Kierkegaard, aliendelea kusema kuwa hata hivyo tumaini lina uhusiano wa pendeleo, katika Agano Jipya, pamoja na ssubira. Ni kinyume cha kukosa subira, haraka, kwa  kila kitu sasa. Ni dawa ya kukata tamaa. Inaweka hamu hai. Tumaini pia ni mwalimu mkuu, ambaye haoneshi kila kitu mara moja, lakini inaweka uwezekano mmoja mbele yako kwa wakati mmoja. Linatoa mkate wa kila siku tu.

Tumaini linasambaza juhudi na hivyo kuruhusu kufikiwa." Kwa sababu hiyo, Kadinali Cantalamessa alisema kwamba tumaini linahitaji dhiki sawa na vile miale ya moto inahitaji upepo ili kujiimarisha yenyewe. Sababu za kidunia za tumaini lazima zife, moja baada ya nyingine, kwa sababu ya kweli, isiyotikisika ambayo ni Mungu hujitokeza." Kidogo kama kile kinachotokea wakati meli inazinduliwa. Ni muhimu kwamba kiunzi kiondolewe na vifaa mbalimbali viondolewe moja baada ya nyingine, ili iweze kuelea na kusonga mbele kwa uhuru juu ya maji. Kwa hakika, “dhiki hutuondolea kila “mshiko” wetu na hutuongoza kumtumaini Mungu pekee” ikiongoza kwenye “hali ile ya ukamilifu inayojumuisha kuendelea kumtumaini kwa kumtumaini Yeye, hata wakati sababu ya mwanadamu kuwa na matumaini imetoweka. Kama ilivyokuwa kwa Maria chini ya msalaba, ambaye kwa hiyo anaalikwa kumcha Mungu wa Kikristo kwa jina la Mater Spei, yaani Mama wa matumaini".

Kilichochochea mawazo kama hayo juu ya nguvu ya tumaini igeuzayo ilikuwa, kama ilivyotajwa, kipindi cha ufufuo wa Lazaro, ambacho kilisababisha hukumu ya kifo cha Yesu; huku sehemu ya poili  kwa zamu huleta ufufukoo wa yeyote anayemwamini. Hapa ndipo kuna maana halisi ya ufufuko wa Kristo, tofauti na ule wa Lazaro au mwana wa mjane wa Naini, aliyefufuka ili kufa mara ya pili, kama Mtakatifu Augustino anavyofundisha. "Sembuse ni ufufuko wa kiroho na uwepo, kulingana na nafasi za kitaalimungu kama ule wa Bultmann ambao sasa umepitwa na wakati. Kinyume chake, Kardinali Cantalamessa alisema: "Yohana anajikita katika  sura mbili nzima za Injili yake kwa ufufuko halisi na wa kimwili wa Yesu, huku akitoa habari fulani ya kina kuhusu ufufuko huo. Kwake, kwa hiyo, si tu sababu ya Yesu yaani, ujumbe wake, ambao umefufuka kutoka kwa wafu, bali nafsi yake!

Mahubiri ya Kipindi cha kwaresima
Mahubiri ya Kipindi cha kwaresima

Ufufuko wa sasa hauchukui nafasi ya ufufuko wa mwisho wa mwili, lakini ni dhamana yake. Haibatilishi au kufanya ufufuko wa Kristo kutoka kaburini kuwa bure, lakini una msingi wake hasa. Kwa uhakika kwamba Yesu mwenyewe alikuwa ameonesha ufufuko wake kama ishara ya ubora wa uhalisi wa utume wake. Kwa hiyo, anavunja upendeleo uliopo kwa wasioamini kuelekea imani, ambayo sio chini ya kile wanacholaumu waamini. Kwa hakika, wanakosoa kwamba hawawezi kuwa na lengo, kwa kuwa imani inawalazimisha, tangu mwanzo, hitimisho wanalopaswa kufikia, bila kutambua kwamba kitu kimoja kinatokea kati yao. Ikiwa tunaanza kutoka kaitka dhana kwamba Mungu hayupo; kwamba nguvu isiyo ya kawaida haipo na kwamba miujiza haiwezekani, hitimisho pia linatolewa tangu mwanzo, kwa hiyo, halisi, hukumu ya awali.

Na ufufuko wa Kristo ni mfano wa kuigwa zaidi wa hii, ikizingatiwa kwamba hakuna tukio la zamani linaloungwa mkono na ushuhuda mwingi kama huu ambao unahusishwa na watu wa kiwango cha kiakili cha Sauli wa Tarso, ambaye hapo awali walipigana dhidi ya imani hii. Kwa hakika, Mtume alitoa orodha ya kina ya mashahidi, ambao baadhi yao bado wako hai, ambao kwa hiyo wangeweza kumkana kwa urahisi”. Kwa hiyo ufufuko ni kuzaliwa upya kwa tumaini,  neno ambalo halipo katika mahubiri ya Yesu kwa ajabu.

Injili zinaripoti mengi ya maneno yake juu ya imani na upendo, lakini hakuna juu ya tumaini - kardinali alifafanua - hata kama mahubiri yake yote yanatangaza kwamba kuna ufufuo kutoka kwa wafu na uzima wa milele. Kinyume chake, baada ya Pasaka, tunaona wazo na hisia za tumaini zikilipuka kihalisi katika mahubiri ya Mitume. Mungu mwenyewe anafafanuliwa kuwa “Mungu wa tumaini”. Maelezo ya kutokuwepo kwa maneno kuhusu tumaini katika Injili ni rahisi: Kristo alipaswa kufa kwanza na kufufuka. Kwa kufufuka tena, alifungua chanzo cha matumaini; alizindua kitu chenye matumaini ambacho ni maisha na Mungu zaidi ya kifo", alihitimisha.

Tafakari ya IV ya Kwaresima
16 March 2024, 18:08