Tafuta

2024.02.28 Uwakilishi wa Kongamano la Wanawake katika Kanisa. 2024.02.28 Uwakilishi wa Kongamano la Wanawake katika Kanisa. 

Wanawake kumi waliojenga Kanisa,mifano ya mazungumzo na heshima

Tarehe 7 na 8 Machi,Chuo Kikuu cha Santa Croce kitakaribisha mkutano kati ya vyuo vikuu kuhusu baadhi ya takwimu za wanawake magwiji wa ubinadamu ambao kwa ushuhuda wao wanaeleza kwa njia inayong'aa maana ya maisha,ya uhusiano na watu na ulimwengu.Bi Gambino:kutumia anthropolojia mbili na kushughulikia mada bila upinzani au madai.

Antonella Palermo na Angella Rwezaula – Vatican.

Maabara ya kiutamaduni ya kutafakari juu ya wanawake kumi wa ajabu, wa kidini, wamisionari, lakini pia walei, walioolewa na akina mama ambao katika mabara tofauti wamepanda Neno la Mungu kwa kuishi imani yao kikamilifu katika ulimwengu wa mara kwa mara mbaya na katika hali zisizo za kibinadamu. Hivi ndivyo inasikikia mbiu ya Kongamano la Vyuo Vikuu  litakaloongozwa na mada ya: “Wanawake Kanisani: magwiji wa ubinadamu” linalotarajiwa kufanyika tarehe 7 na 8 Machi 2024 katika Chuo Kikuu cha Kipapa cha Msalaba Mtakatifu (Santa Croce) na ambalo liliwasilishwa Jumatano tarehe 28 Februari 2024 katika Taasisi ya Baba wa Kanisa Augustinianum,mjini Roma.

Wanawake kumi Watakatifu

Hili ni tukio ambalo ni matokeo ya mtandao unaofumwa kati ya taasisi mbalimbali za kitaaluma kuanzia na: Chuo Kikuu katoliki cha Avila (UCAV), Chuo Kikuu cha Kipapa cha Urbaniana, Chuo Kikuu cha Kipapa cha Msalaba Mtakatifu(Santa Corce), Taasisi ya Mafunzo ya Juu ya Wanawake ya Chuo Kikuu cha Kipapa ya Regina Apostolorum na Kitivo cha Kipapa cha Taalimungu cha  Teresianum cha Roma. Mpango huu unaofanyika kila baada ya miaka miwili kwa mwaka wa 2024 unalenga kutafakari juu ya wanawake kumi watakatifu, ambao ushuhuda wao utatolewa na wazungumzaji wengi na kuzingatiwa katika maeneo matano kama vile: Hadhi, mazungumzo na amani, upendo wa elimu, upendo wa sala, moyo wa huruma, kuzaa matunda  ya zawadi. Kwa njia hiyo kuna Mtakatifu Josephine Bakhita (bahati), Msudani, aliyeuzwa utumwani na kuteswa, ambaye alikuja kuwa msimamizi wa Afrika. Halafu kuna Magdeleine de Jesus mtumishi wa Mungu na  mwanzilishi wa Udugu wa Dada Wadogo wa Yesu, ambaye hapo awali aliwekwa wakfu kwa ajili ya watu wa Kiislamu tu, wanaoishi na wahamaji wa jangwa la Sahara ya Algeria, kisha kufunguliwa kwa ulimwengu wote.

Na tena Mtakatifu Elizabeth Ann Seton, mkuzaji hamasishajiwa mipango mingi ya upendo  kwa ajili ya maskini, hasa wajane wenye watoto wadogo, Mmarekani wa kwanza kutangazwa kuwa mtakatifu, kama vile Mtakatifu Mary Mackillop alivyokuwa wa kwanza nchini Australia, mwanzilishi wa Shirika la Masista wa Mtakatifu Joseph wa Moyo Mtakatifu wa Yesu, Mtakatifu Laura wa Mtakatifu Catherine wa Siena, mzaliwa wa Maria Laura Montoya ya Upeguí, ni raia wa Colombia; Mtakatifu Catherine Tekakwitha, Mzaliwa wa kwanza wa Amerika Kaskazini kutangazwa kuwa mtakatifu. Mtakatifu Teresa wa Calcutta, mmoja wa watu mashuhuri zaidi duniani, mtumishi wa watumishi wa maskini, kisha Rafqa Ar-Rayès, mtawa wa Lebanon ambaye alikuwa wa  Shirika la  ya Wamaroniti  ya Antonia. Na hatimaye Mwenyeheri Maria Beltrame Quattrocchi, mke wa Luigi, wote wawili wakiwa wanandoa na Mtumishi wa Mungu Daphrose Mukansanga, wa Jumuiya ya Emmanuel, ambaye pamoja na mumewe waliuawa mnamo mwaka 1994 na watoto sita kati ya kumi, katika familia ya kweli ya Kikristo ambayo ililipa gharama ya mivutano ya kikabila kwa kufukuzwa huko Rwanda.

Mada ya wanawake katika mwanga wa anthropolojia mbili

Mkutano huo hautakusanya sana tafakari za kinadharia lakini, kwa mtindo wa mazungumzo, utataja maisha yao ili kuelewa jinsi wanavyoweza kuhamasisha maisha ya leo katika utakatifu wa maisha ya kila siku.  Je, tunawezaje kuchochea maslahi ya watu kwa maana hii? Hii ndiyo changamoto iliyotolewa na Profesa Cristina Reyes, makamu kitivo cha  kitaaluma wa Chuo Kikuu cha Kipapa cha Santa Croce. Sio juu ya kufanya tofauti za kijinsia au kushughulikia ulimwengu wa kike pekee.

Gambino: Kuunda mazungumzo ya ufanisi ndani na nje ya Kanisa

Bi Gabriella Gambino, Katibu Mkuu wa Baraza la Kipapa la  Walei, Familia na Maisha, alieleza kwa vyombo vya habari vya Vatican kuwa na matumaini, ya kwamba mkutano huo utaleta uelewa wa kina kutokana na mtazamo wa kikanisa wa jinsi ya kutoa nafasi kwa asili ya kike ili kuimarisha Kanisa. Wanawake hawa ni wafasiri wa wa kiinjili ambayo kwayo tunaweza kuelewa vyema maisha, ulimwengu, watu, shukrani kwa zawadi ya anga ya kiroho ambayo wameweza kuunda. Ninaamini kwamba leo kuzungumzia suala la wanawake kana kwamba ni nyanja yenyewe ni jambo ambalo halieleweki kikamilifu. Ni muhimu kushughulikia mada ya wito wa kike katika Kanisa kuhusiana na ule wa kiume. Anthropolojia mbili, ambayo Edith Stein na Yohane Paulo II walizungumzia na  ni ya msingi leo hii kwa ajili ya kuunda mazungumzo ya ufanisi na yenye ufanisi ndani na nje ya Kanisa.”

Kuna haja ya usawa kati ya mwanaume na mwanamke

Na kwa upande wa  Profesa Lorella Congiunti, wa Chuo Kikuu cha Kipapa cha Urbaniana,  alisema “Kuna haja ya kuwa na usawa kati ya mwanamume na mwanamke na ukamilishano unaohitajika na kuhakikisha kwamba katika Kanisa miito yote inaweza kujieleza kadiri ya karama na karama zao wenyewe, kama zilivyogawiwa na Mungu. Na kwa hiyo akiakisi hitaji la kushinda aina yoyote ya madai ya mgawo: “Wanaume na wa kike kwa pamoja wanatambua kikamilifu ubinadamu na mfano wa sura ya Mungu katika kiwango kisicho kawaida,”

Kuwa na ujasiri wa kugawana majukumu

Tunaweza, kwa mfano, kuwa ujasiri katika mchakato wa kugawa majukumu ya juu katika nyanja za kitaaluma, kama vile ukurugenzi wa wanawake wa kawaida, lakini maendeleo mengi yamepatikana, Congiunti alifafanua zaidi, akieleza kuwa, katika suala hili, hakuna makatazo ya kisheria au chuki, wakati mwingine, kama ilivyo kwa Urbaniana, pia ni suala la kuzingatia utofauti wa tamaduni za wanafunzi kwa kutathmini fursa ya kuchagua wanaume au wanaume. wanawake katika uongozi wa vyuo vikuu.  Aliyehusika kwenye mada hiyo alikuwa pia Maria del Rosario Saez Yuguero, Mkurgenzi wa Chuo Kikuu cha Avila, ambaye alionesha kwa ufupi uzuri wa kutumia nafasi kama hiyo, kwa ushirikiano kamili na wenzake wa kiume. Katika mkutano wa 2022, hatimaye alikumbuka, taasisi tatu za mafunzo kwa wasichana nchini Lebanon ziliungwa mkono, taasisi za ibada za Kilatini, Kigiriki-Melkite na Maronite. Mwaka huu msaada huo unalenga watoto na familia huko Aleppo, Siria. Njia ambayo Kamati ya Kisayansi inakusudia kuunganisha imani na kazi, kufuatia ushuhuda wa wanawake waliojadiliwa katika makongamano.

Kongamano kuhusu wanawake 10 watakatifu 7 na 8 Machi 2024
29 February 2024, 17:28