Tafuta

Kardinali José Tolentino Mendonça,Mwenyekiti wa Baraza la Kipapa la Utamaduni na Elimu Kardinali José Tolentino Mendonça,Mwenyekiti wa Baraza la Kipapa la Utamaduni na Elimu 

Uwasilishaji wa kazi ya kishairi ya Kardinali de Mendonça katika Chuo Kikuu Katoliki

Tukio hilo litafanyika Jumatatu 12 Februari 2024,saa 12.00 jioni huko Milano,Italia katika ukumbi wa Pio XI kwenye Chuo Kikuu Katoliki cha Moyo Mtakatifu.Lina Bolzoni,profesa mstaafu katika Shule ya Sekondari ya Piza,atajadiliana na Mwenyekiti wa Barazala Kipapa la Utamadunia na Elimu Vatican.

Vatican News

Kitabu kinaitwa ‘Estranei alla terra’ na ni kitabu kinachokusanya: ‘Strada bianca - Njia nyeupe(2005)’ na Teoria della frontiera -Dhana ya mpaka (2017)’, vitabu viwili muhimu vya mashairi ya Kadinali José Tolentino Mendonça, Mwenyekiti wa Baraza la Kipapa la Utamaduni na Elimu. Kitabu hicho, kilichochapishwa na nyumba ya uchapishaji ya Crocetti, kitawasilishwa mjini Milano siku ya Jumatatu tarehe 12 Februari 2024, saa kumi na mbili jioni, katika Ukumbi wa Pio XI wa Chuo Kikuu Katoliki  cha Moyo Mtakatifu.

Katika mazungumzo na Lina Bolzoni

Baada ya salamu za kitaasisi kutoka kwa mkuu wa Chuo Kikuu cha Kikatoliki Franco Anelli, Kardinali Mendonça atazungumza na Lina Bolzoni, profesa aliyestaafu katika Sekondari ya Pisa. Alessandro Zaccuri, mkurugenzi wa Mawasiliano ya Chuo Kikuu, atasimamia mjadala huo, huku usomaji wa maandishi ya mashairi ukikabidhiwa kwa mwigizaji Christian Poggioni. Katika vitabu viwili vya mashairi cha Strada bianca na Teoria della frontiera vinafanana, na sasa vinawasilishwa kwa msomaji wa Kiitaliano katika kitabu kimoja chenye jina Estranei alla terra, ni ushuhuda wa mwandishi anayejitambua katika hali ya ‘mshairi mtoro’ na kuakisi hali halisi hapa chini kila mara aina mpya na zinazoonekana kupingana, zinazovutia  kwa wahusika wakuu kama  Simone Weil, Pier Paolo Pasolini na Mtakatifu  Teresa wa Avila wanafurahia haki sawa ya uraia.

Kazi ya Kardinali

José Tolentino Mendonça alizaliwa  mnamo mwaka wa 1965 huko Funchal, kwenye kisiwa cha Madeira nchini Ureno. Mnamo 1990, akapewa Daraja la Upadre  na alianza  ushairi wake wa kwanza na mkusanyiko wa O dias contados, ambao ulifuatiwa na majina mengine mengi ambayo hivi karibuni yalimfanya kuwa moja ya sauti asilia ya kizazi chake na fasihi ya kisasa ya Ureno. Msomi wa Biblia na mwandishi wa kazi nyingi zisizo za uongo na za kiroho, alishikilia nyadhifa muhimu katika Chuo Kikuu Katoliki cha Lisbon. Mwaka 2018 aliteuliwa kuwa Kardinali na Baba Mtakatifu Francisko na baada ya kushika wadhifa wa Mkutubi na Mtunza Nyaraka Vatican mnamo, Septemba 2022 aliteuliwa kuwa Mwenyekiti wa Baraza la Kipapa la Utamaduni na Elimu. Nchini Italia vitabu vyake vimechapishwa na Vita na Pensiero, na vilevile na Mtakatifu  Paolo na Paoline.

Mnamo 2022, mkusanyiko wa kitabu cha  The Poppy and the Monk ulitolewa katika matoleo ya Qiqajon, na insha ya utangulizi ya Lina Bolzoni. Mnamo 2023 Crocetti alichapisha kitabu cha ‘Estranei alla terra’, na tafsiri kutoka kwa lugha ya  Kireno na Teresa Bartolomei. Katika mwaka huo huo mwandishi alitunukiwa tuzo ya kimataifa ya mafanikio ya maisha ya “LericiPea - Golfo dei Poeti.”

Kwa kushiriki katika tukio hilo, unaweza kujiandikisha hapa link.

09 February 2024, 12:29