Tafuta

Papa Francisko wakati wa katekesi yake 28 Februari 2024 Papa Francisko wakati wa katekesi yake 28 Februari 2024  (VATICAN MEDIA Divisione Foto)

Papa amekwenda Gemelli ya Kisiwa cha Tiberina kwa uchunguzi zaidi

“Mara baada ya katekesi, Papa Francisko amekwenda katika Hospitiali ya kisiwa cha Tiberina Gemelli kwa ajili ya ucunguzi.Na hatimaye amerudi mjini Vatican.”Hayo ni kwa mujibu wa Msemaji wa vyombo vya habari vya Vatican kwa waandishi wa Habari.Ikumbukwe hivi karibun Papa alikuwa na homa.Na hata katika Katekesi alielezea kuwa na mafua.

Vatican News

Kwa mujibu wa taarifa uliyotolewa kutoka Ofisi ya Vyombo vya Habari vya Vatican, Jumatano tarehe 28 Februari 2024 imebainisha kuwa: “Baada ya Katekesi yake, Papa Francisko alikwenda katika Hospitali ya ‘Isola Tiberina - Gemelli Isola’ kwa ajili ya vipimo vya uchunguzi. Mwishowe alirudi Vatican."”

Kama inavyojulikana, Papa  Francisko amekuwa kwa siku hizi akiahirisha ratia za vikao vilivyokuwa vimepangwa kwa sababu ya afya yake. Kwa njia hiyo asubuhi ya tarehe 28 Februari 2024  pia, mwanzoni mwa  katekesi yake kuu, aliwaeleza wamini na mahujaji waliohudhuria katika Ukumbi wa Paulo VI mjini Vatican  kwamba: “bado yuko mafua kidogo” na kumuomba mmoja wa washirika wake, Monsinyo Filippo Ciampanelli, kusoma katekesi yake. Mara tu baada ya tukio hilo  kwa hiyo,  alikwenda kwenye ukaguzi katika hospitali ya Roma, iliyopo hatua chache kutoka mjini Vatican.

Papa alikwenda hospitali kwenye vipimo na baadaye kurudi mjini Vatican
28 February 2024, 16:42