Tafuta

2024.02.03 Ubatizo. 2024.02.03 Ubatizo.  (© Antonio Gravante - www.studio-fotograv.com)

Kwa uhalali wa sakramenti,kanuni na mambo hayawezi kurekebishwa

Kwa kukabiliwa na uendelezwaji wa ukiukwaji wa kiliturujia,katika Ujumbe wa ‘Gestis verbisque wa Baraza la Kipapa la Mafundisho Tanzu ya Kanisa unabainisha kwamba maneno na vipengele vilivyowekwa katika ibada muhimu ya kila sakramenti haviwezi kubadilishwa kwa sababu katika mantiki hiyo sakramenti haipo tena.

Vatican News

Ujumbe kutoka Baraza la Kipapa la Mafundisho Tanzu ya Kanisa uliochapishwa Jumamosi tarehe 3 Februari 2024 unaitwa( Gestis verbisque la Nota del Dicastero per la Dottrina della Fede). Ni hati iliyojadiliwa na kuidhinishwa na makadinali na wajumbe wa  maaskofu katika Mkutano Mkuu wa hivi karibuni wa Baraza la Kipapa hilo na kwa hiyo kupitishwa na Papa Francisko, ambalo linasisitizwa tena kwamba kanuni na vipengele vya muundo vilivyoanzishwa katika ibada muhimu ya sakramenti haviwezi kubadilishwa kwa utashi  jina la ubunifu. Kwa kufanya hivyo, kiu kweli, sakramenti yenyewe si halali, kwa hiyo haijawahi kuwepo.

Uwasilishaji wa Fernández

Katika uwasilishaji wa hati hiyo, Kadinali Victor Fernández, Mwenyekiti wa Baraza la Kipapa la Mafundisho Tanzu ya Kanisa, anaelezea mwanzo wake, yaani, “kuzidisha kwa hali ambazo mtu alilazimika kuhakikisha ubatili wa sakramenti zinazoadhimishwa”, na marekebisho ambayo “yalisababisha haja ya kuwafuatilia watu wanaohusika ili kurudia ibada ya ubatizo au kipaimara na idadi kubwa ya waamini wameeleza vya kutosha wasiwasi wao.” Mabadiliko ya kanuni ya ubatizo yanatajwa kuwa mfano, kwa mfano: “Ninakubatiza kwa jina la Muumba...” na “Kwa jina la baba na mama ... tunakubatiza.” Hali ambazo pia ziliwahusu baadhi ya mapadre ambao “wakiwa wamebatizwa kwa kanuni za aina hii, waligundua kwa uchungu ubatili wa kuwekwa wakfu kwao na sakramenti zilizoadhimishwa hadi wakati huo.” Kardinali anaeleza kwamba “wakati katika maeneo mengine ya utendaji wa kichungaji wa Kanisa kuna nafasi ya kutosha kwa ajili ya ubunifu”, katika muktadha wa kuadhimisha sakramenti hii “badala yake inabadilika kuwa utashi ya kudanganywa.” Fernandez anahitimisha kwa kukumbusha kwamba “sisi wahudumu tunatakiwa kuwa na nguvu ya kushinda kishawishi cha kujisikia kama wamiliki wa Kanisa” na kwamba “waamini wana haki, nao, kuwapokea jinsi Kanisa linavyoweka.”

Kipaumbele cha utendaji wa  Mungu

“Kwa matukio na maneno yaliyounganishwa kwa karibu - tunasoma katika Dokezo la  Baraza la Kipapa la Mafundisho kuwa - Mungu anafichua na kutekeleza mpango wake wa wokovu kwa kila mwanamume na mwanamke.” Kwa bahati mbaya “lazima ieleweke kwamba adhimisho la kiliturujia, hasa lile la sakramenti, si mara zote linafanyika kwa uaminifu kamili kwa taratibu zilizowekwa na Kanisa.” Kanisa, kwa hakika, lina wajibu wa kuhakikisha kipaumbele cha utendaji wa Mungu na kulinda umoja wa Mwili wa Kristo katika matendo yale ambayo hayana kifani kwa sababu ni matakatifu ya “ubora” na ufanisi unaohakikishwa na utendaji wa kikuhani, Kristo.” Kanisa pia “linajua kwamba kusimamia neema ya Mungu haimaanishi kuidhinisha, bali kuwa chombo cha Roho katika kusambaza zawadi ya Kristo wa Pasaka. Linajua, hasa, kwamba Ukuu wake  kuhusu sakramenti husimama mbele ya kiini chake” na kwamba “katika ishara za sakramenti lazima ilinde ishara za wokovu ambazo Yesu amemkabidhi.”

Vitu  na taratibu

Kwa hiyo Ujumbe unaeleza kwamba “Kitu cha cha  kisakramenti ni tendo la kibinadamu ambalo Kristo anatenda. Wakati mwingine kitu cha nyenzo kipo ndani yake (maji, mkate, divai, mafuta), wakati mwingine ishara ya wazi (ishara ya msalaba, kuwekewa mikono, kuzamishwa, kuingizwa, kibali, upako).” Ushirika ambao “ni wa lazima kwa sababu unatia mizizi sakramenti sio tu katika historia ya mwanadamu, lakini pia, kimsingi zaidi, katika mpangilio wa mfano wa Uumbaji na kuurudisha kwenye fumbo la Umwilisho wa Neno na Ukombozi ulioletwa na Yeye.” Kuhusu namna ya sakramenti, “inaundwa na neno, ambalo linatoa maana ipitayo maumbile ya jambo, likibadilisha maana ya kawaida ya kipengele cha nyenzo na maana ya kibinadamu ya kitendo kilichofanywa. Neno hili daima huvuta msukumo kwa viwango tofauti kutoka katika Maandiko Matakatifu, lina mizizi yake katika Mapokeo ya kikanisa hai na limefafanuliwa kwa mamlaka na Majisterio ya Kanisa.” Kwa hivyo vitu na umbo havijawahi kutegemea na haviwezi kutegemea utashi wa mtu mmoja au jumuiya moja.”

Haiwezi kubadilishwa

Hati hiyo inasisitiza tena kwamba “kwa sakramenti zote, kwa vyovyote vile, utunzaji wa vitu na kanuni daima vimekuwa vikihitajika kwa uhalali wa maadhimisho, kwa ufahamu kwamba marekebisho ya kiholela ya moja na/au nyingine – ambao mvuto na nguvu yake ya kulemaza lazima ijulikane mara kwa mara - kuhatarisha utoaji mzuri wa neema ya sakramenti, na uharibifu dhahiri kwa waamini.” Kinachosomwa katika vitabu vya kiliturujia vilivyotangazwa lazima kizingatiwe kwa uaminifu bila “kuongeza, kuondoa au kubadilisha chochote.” Kwa sababu maneno au jambo likibadilishwa, sakramenti haipo tena. Katika suala hili, katika maelezo ya kipengele 31 cha hati hiyo,  tofauti kubwa inafanywa kati ya uhalali na usio halali, ikieleza kwamba “marekebisho yoyote ya Kanuni ya sakramenti siku zote ni kinyume cha sheria,  hata kama ni kitu kidogo ambacho hakibadili maana yake asilia na hakifanyi kuwa batili. Mabadiliko ya vipengele muhimu vya kuadhimisha sakramenti pia yanaleta “mashaka juu ya nia halisi ya mhudumu, na kubatilisha uhalali wa sakramenti inayoadhimishwa”.

Sanaa ya kuadhimisha

Liturujia inaruhusu aina mbalimbali zinazohifadhi Kanisa kutokana na ‘usawa thabiti.’ Kama ilivyoelezwa katika  Katiba ya Mtaguso ya Sacrosanctum Concilium. Lakini aina hii na ubunifu unaopendelea kueleweka zaidi kwa ibada na ushiriki hai wa waamini hauwezi kuhusika na kile ambacho ni muhimu katika kuadhimisha sakramenti. “Inaonekana inazidi kuwa muhimu kukuza sanaa ya kusherehekea ambayo, huweka mbali kutoka katika mafundisho magumu na mawazo yasiyo ya kawaida, husababisha nidhamu kuheshimiwa, hasa ili kuwa wanafunzi wa kweli.” Kukumbusha  maandishi yana nukuu hiyo  kutoka kwa Papa Francisko kwamba: “Sio suala la kufuata kanuni za kiliturujia: ni “nidhamu.” Kwa maana iliyotumiwa na Guardini - ambayo, ikizingatiwa kwa uhalisi, hutuunda: ni ishara na maneno ambayo huleta utaratibu katika ulimwengu wetu wa ndani kwa kutufanya tupate hisia, mitazamo na  tabia. Si matamshi ya jambo bora ambalo tunajaribu kujitia moyo nalo, bali ni tendo linalohusisha mwili katika ukamilifu wake, yaani, kuwa umoja wa nafsi na mwili.”

Kulinda utajiri wa sakramenti

“Sisi... tunayo hazina hii katika vyombo vya udongo, ili ionekane ya kuwa uwezo huu usio wa kawaida ni wa Mungu, wala hautoki kwetu” (2Kor 4:7). Katika hitimisho, hati ya ya Baraza la Kipapa la Mafundisho Tanzu ya Kanisa linanukuu maneno ya Mtakatifu Paulo, kipingamizi kinachotumiwa “kusisitiza jinsi utukufu wa uweza wa Mungu unavyofunuliwa kupitia udhaifu wa huduma yake kama mtangazaji na pia kinaelezea vizuri kile ambacho hutokea katika sakramenti. Kanisa zima linaitwa kulinda utajiri uliomo ndani yake, ili kwamba ukuu wa tendo la Mungu la kuokoa katika historia usifichwe kamwe, hata katika upatanisho dhaifu wa ishara na ishara mfano wa asili ya mwanadamu.”

Hati ya Baraza la Kipapa kuhusu ubatizo
03 February 2024, 16:33