Tafuta

2023.12.22  Kardinali Krajewski katika kituo cha Yatima huko Betlehemu nchi Takatifu. 2023.12.22 Kardinali Krajewski katika kituo cha Yatima huko Betlehemu nchi Takatifu. 

Kard.Krajewski:hali halisi ya Gaza ni ngumu

Mwakilishi wa Papa aliyetumwa na Baba Mtakatifu katika Nchi Takatifu,ameviambia vyombo vya habari vya Vatican kuhusu siku nzima aliyotumia kati ya watu na hali halisi ya kikanisa ya Bethlehemu katika migogoro ya Ukanda:"Nilizungumza na baadhi ya vijana waliotoroka,msichana alipoteza wanafamilia 12 na waliomba kwa uchungu lakini sio bila tumaini.”

Vatican News

Inahitajika kuwa na moyo mkuu wa  kutoa nafasi ya maumivu na kuyafunika kwa tumaini wakati kila kitu, nyumba, mapenzi, maisha yamepoteza haki ya  joto na hali ya hatari iliyojaa hofu kuwa kawaida. Baada ya ziara nyingi katika eneo la vita katika kambi za vita vya Kiukraine, wakati umefika kwa Kadinali Konrad Krajewski kupeleka mkumbatio wa Papa na usaidizi wa Noeli  kwenye eneo jingine ambalo ni  Ukanda wa Gaza na Nchi Takatifu ambapo tangu 7 Oktoba 2023 wamefunikwa na giza la mkasa mwingine. Habari za mwakilishi wa Papa Francisko kwenye vyombo vya habari vya Vatican, zinaanzia Bethlehem, ambapo alifika huko  asubuhi 22 Desemba na kujikuta amepiga magoti katika Kanisa Kuu la Kuzaliwa kwa Bwana, mapema asubuhi na mara baada ya kuanza ziara ya mji huo na Padre wa Parokia ya Gaza.

Kardinali Krajewski akiwa katika kituo cha Yatima huko Bethlehemu
Kardinali Krajewski akiwa katika kituo cha Yatima huko Bethlehemu

Katika kueleza siku yake alisema "Tulikwenda kwenye vituo vitatu vya watoto yatima, ambako hata watoto wachanga wanaotolewa nje ya barabara wanatunzwa,  na watoto wawili walioletwa hivi karibuni  tu na watawa.” Alisema Kardinali na kwamba alikaa nao kwa muda ili kusali pamoja na kwamba: “Pia niliwaachia msaada wa Baba Mtakatifu aliowatumia kwa sababu wanaishi kwa shida sana.” Kisha alibaki kwa chakula cha mchana katika seminari ya Upatriaki wa Bethlehemu, ambapo waseminari 38 wanaishi. Alasiri ndiyo wakati wa mkutano mgumu sana. Kardinali Krajewski alizungumza kuhusu watu wanne, vijana kabisa, waliokuja kuzungumza naye. Walipata bahati ya kuondoka Gaza kabla ya kuanza mikasa. Kwa sababu hiyo, alisisitiza.  “Wanafamilia wao wote walibaki, ila msichana alipoteza wanafamilia 12. Walikuja kueleza jinsi mambo yalivyo, kuweza kumwambia Baba Mtakatifu hali ngumu yote iliyopo, kwamba hakuna maji, hakuna umeme, kwamba watu wanaozunguka kanisa ni karibu watu 600. Tulisali pamoja, kwa hakika tulihuzunishwa sana lakini hatukukosa tumaini”.

Kardinali aliendelea kusema kuwa "Siku nzima nilipitia katika nchi ambayo Yesu alizaliwa na ambapo leo hii tunapitia polepole na chini ya udhibiti mkali. Tungeweza kuingia kutoka upande mmoja, mlango pekee, kwa sababu Wapalestina hawawezi kuondoka Bethlehemu, wanapaswa kukaa mjini. Kesho, tutaona ni wapi tunaweza kwenda kusaidia jumuiya mbalimbali za kidini, mapadre wanaofanya kazi katika hali hii ngumu sana.” Kardinali Krajewski alisema pia kuwa alikutana na Askofu wa Kikatoliki wa Ugiriki na kwamba: “Tulizungumza kuhusu jinsi tunaweza kuongeza misaada. Kwa sababu katika Noeli ya mwaka huu bila taa mwanga unaopasha joto na kuonesha mwelekeo ni ule wa ukaribu tu."

Kardinali Krajewski yuko Nchi Takatifu
Kardinali Krajewski yuko Nchi Takatifu
23 December 2023, 18:07