Tafuta

Kardinali Cantalamessa akitoa tafakari ya Pili ya Majilio 22 Desemba 2023. Kardinali Cantalamessa akitoa tafakari ya Pili ya Majilio 22 Desemba 2023.  (Vatican Media)

Kard.Cantalamessa:Tengenezeni Njia ya Bwana na Yohane na Mama wa Kristo

Katika Tafakari ya Pili ya Majilio iliyofanyika katika Ukumbi wa Paulo VI mjini Vatican,tarehe 22 Desemba 2023 kwa kuongozwa na Kardinali Cantalamessa,Mhubiri Mkuu wa Nyumba ya Kipapa kwa Sekretarieti Kuu ya Vatican kwa uwepo wa Baba Mtakatifu amejikita na mada:“Tengenezeni njia za Bwana.Kuelekea Noeli kwa kusindikizwa na Mtangulizi na Mama wa Kristo.”

Na Angella Rwezaula, - Vatican.

Katika mwendelezo wa Tafakari ya Pili ya Majilio iliyofanyika katika Ukumbi wa Paulo VI mjini Vatican, Ijumaa tarehe 22 Desemba 2023 kwa kuongozwa na Kardinali Raniero Cantalamessa, Mhubiri Mkuu wa Nyumba ya Kipapa kwa Sekretarieti Kuu ya Vatican kwa uwepo wa Baba Mtakatifu Francisko amejikita na mada ya: “Tengenezeni njia za Bwana. Kuelekea Noeli kwa kusindikizwa na Mtangulizi (Yohane) na Mama wa Kristo.” Upyaisho wa Elimu ya Maria(Mariology) shukrani kwa Mtaguso, ulileta ugunduzi wa mwelekeo mpya wa imani ya Maria, ambaye, kama Mtaguso wa II wa Vatican unavyosema, kuwa alisonga mbele katika hija ya imani. Maria, kwa maneno mengine, hakuamini mara moja tu, bali alienenda katika imani na kuendelea katika hiyo. Kama Mtakatifu Yohane  Paulo II alivyosema katika Waraka wa  Redemptoris Mater,  kuwa "Maneno ya Elizabeti hayatumiki kwa wakati fulani tu wa Matamshi: Utukufu ni wakati wa kilele cha  imani ya Maria, lakini pia ni mahali pa kuanzia ambayo  ni safari yake ya pete ya harusi."

Mahubiri ya Kard Cantalamessa 22 Desemba 2023
Mahubiri ya Kard Cantalamessa 22 Desemba 2023

Kardinali Cantalamessa alisema kuwa "baada ya Kupashwa na Malaika, Maria, kwa imani alimwakilisha Yesu hekaluni, kwa imani alimfuata na kubaki kando, kwa imani alisimama chini ya Msalaba, kwa imani alisubiri Ufufuko wake. Chini ya Msalaba, hasa, Maria hana nguvu kabla ya kifo cha imani ya Mwanawe, lakini anakubali kwa upendo. Ni kielelezo cha janga la Ibrahimu, lakini ni ya kudai sana!" Pamoja na Ibrahimu Mungu alisimama, lakini si pamoja naye. Chini ya Msalaba anamtoa Mwanawe kwa Baba, katika imani yake isiyotikisika aliamini, akitumaini dhidi ya matumaini yote na hivyo anakuwa mama wa watu wote. "Maria aliamini na kile alichoamini kilitimia, aliandika Mtakatifu Augustino, ambaye mamlaka yake yaliwasukuma mababa wa Baraza kuweka hotuba juu ya Maria ndani ya hotuba ya Kanisa, katika katiba ya Lumen Gentium. Kardinali Raniero Cantalamessa, alisema: “Hatari kubwa zaidi ya imani ni ile ya kukashifiwa na unyenyekevu na ubinadamu wa Kristo." Akimtaja Pascal na barua ya kitume iliyotolewa Papa Francisko kwa ajili ya kumbukumbu ya miaka 400 ya kuzaliwa kwake, Kadinali alisema kwamba kwa mwanafalsafa wa Kifaransa hatari kubwa zaidi ni "kuweka Yesu Kristo katika mabano".

Papa alikuwapo kwenye tafakari la II la Majilio
Papa alikuwapo kwenye tafakari la II la Majilio

Katika mijadala ya sasa juu ya kuwepo au vinginevyo kwa Mungu, Kardinali Cantalamessa alishutumu kuwa: "jina la Yesu Kristo karibu halijatamkwa kamwe, kana kwamba halikuwa la majadiliano juu ya Mungu. Ulimwengu na vyombo vyake vya habari hufanya kila kitu, na kwa bahati mbaya kufaulu, kuweka jina la Kristo tofauti au kimya katika kila mjadala unaofanywa kuhusu Kanisa. Sisi, hata hivyo, lazima tufanye kila kitu ili kumwacha awepo, kwa sababu bila Yesu kila kitu ulimwenguni ni bure. Kama Pascal anavyofundisha, "Mungu huhisiwa kwa moyo, kashfa iliyosababishwa na hotuba ya Mtakatifu Paulo kwa Areopago, leo  hii ni ya chini sana lakini haipo kidogo kati ya wasomi, na athari mbaya zaidi juu ya kukataliwa ya unyenyekevu na ubinadamu wa Kristo ni ukimya juu yake." 

Katika ulimwengu ulio jaa malimwengu unataka kuondoa moyo wa Pango la Kuzaliwa kwa Bwana

Kardinali Cantalamessa alisema "Noeli ya  mwaka huu inaadhimisha miaka 800 tangu kuunda  kwa mara ya kwanza Pango la  Kuzaliwa kwa Yesu huko Greccio. Ni ya kwanza kati ya karne tatu za Wafransiskani. Itafuatwa ya mnamo 2024, na ile ya kupata madonda kwa Mtakatifu mnamo 2026, na ile ya kifo chake. Hali hii inaweza pia kutusaidia kurudi moyoni. Mwandishi wake wa kwanza wa wasifu wake, Tommaso wa Celano, anaripoti maneno ambayo(Poverello) yaani Maskini alielezea mpango wake kwamba: Ningependa, kumwakilisha Mtoto aliyezaliwa Bethlehemu, na kwa njia fulani kuona kwa macho ya mwili wangu ugumu ambao yeye alijikuta kwa kukosa vitu muhimu kwa ajili ya mtoto mchanga, jinsi alivyowekwa kwenye kitanda cha kulala na jinsi alivyolala kati ya ng'ombe na punda." Kardinali Cantalamessa aliongeza: “lakini kwa bahati mbaya, baada ya muda, pango la kuzaliwa kwa Yesu limeondolewa kutoka kwa kile lilichowakilishwa na Francis. Mara nyingi imekuwa aina ya sanaa au burudani ambayo mtu anavutiwa na mazingira ya nje, badala ya maana ya fumbo lenyewe. Hata hivyo, inatimiza kazi yake kama ishara na itakuwa ni upumbavu kuiacha. Katika ulimwengu wetu wa magharibi, mipango inaongezeka ili kuondoa kila marejeo ya kiinjili na kidini kutoka katika sherehe za  Noeli, na kuifanya kuwa sherehe safi na rahisi ya wanadamu na familia, na historia nyingi za hisotria na wahusika waliobuniwa badala ya wale halisi. Wengine wangependa hata kubadilisha jina la sikukuu.”

Kardinali Cantalamessa katika tafakari la II la Majilio 22 Desemba 2023
Kardinali Cantalamessa katika tafakari la II la Majilio 22 Desemba 2023

Kardinali Cantalamessa kadhalika alifafanua vizingizio vya bure kwamba: “moja ya sababu za hili ni kuhimiza kuishi pamoja kwa amani na wamini wa dini nyingine, kivitendo na Waislamu. Kwa uhalisia, hiki ni kisingizio cha ulimwengu fulani wa kidunia ambao hautaki ishara hizi, sio za Waislamu. Ndani ya Quran kuna Sura inayohusu kuzaliwa kwa Yesu ambayo inafaa kujulikana.  Kwa kuinukuu Kardinali ameongeza kusema kuwa Sura hiyo inasema: “Malaika wakasema: “Ewe Mariamu! Mwenyezi Mungu anakubashirieni neno litokalo kwake, jina lake ni Masihi Isa bin Marimu ataheshimika duniani na Akhera, Naye atakuwa miongoni mwa walio karibu zaidi na Mwenyezi Mungu. Na atazungumza na watu katika utoto wake na katika utu uzima wake na atakuwa miongoni mwa watu wema. Mariamu akashangaa, “Bwana wangu! Ninawezaje kupata mtoto wakati hakuna mwanaume aliyewahi kunigusa?” Malaika akajibu, “Ndivyo itakavyokuwa. Mwenyezi Mungu huumba apendavyo. Anapohukumu jambo, huliambia tu, ‘Kuwa!’ Na huwa!

Ushuhuda wa Maria kuwepo katika Kitabu kitukufu cha Quran

Kardinali Mkapuchini alielezea tukio fulani la kweli kwa kutoa mfano kuhusu hilo kwamba: "Wakati fulani, Jumamosi jioni, nilikuwa nikitafakari juu ya Injili ya Dominika  kwenye televisheni ya Italia (RAI)" na nilifanya sura hii isomwe na mwanamume wa Kiislamu ambaye alisema anafurahi kuchangia kwa njia hii ili kuondoa kutokuelewana ambayo inawadhuru, kwa kisingizio cha kuwapendelea." Ibada ambayo Quran inakumbuka kuzaliwa kwa Yesu na mahali ambapo Bikira Maria anakaa ndani yake ilipata utambuzi usiotarajiwa na wa kushangaza miaka michache iliyopita. Mfalme wa Abu Dhabi aliamua kuweka wakfu msikiti huo mzuri. Wa Uarabuni  ambapo hapo awali ilikuwa na jina la mwanzilishi wake, Sheikh Mohammad Bin Zayed, kwa Maria, Umm Eisa,  yaani “Maria Mama wa Yesu.” Kwa hivyo Pango la kuzaliwa kwa Yesu ni mila muhimu na nzuri, lakini hatuwezi kuridhika na matukio ya asili ya nje. Ni lazima tuweke pango  tofauti, ile ya moyo. Corde creditur: kwa moyo unaamini. “Kristo akae mioyoni mwenu kwa imani,” asema Mtume huyo huyo (Waefeso 3:17)."

Mahali ambapo Mungu huzaliwa, mwanadamu hufa

Maria na mume wake Yosefu wanaendelea kubisha hodi kwa njia isiyoeleweka, kama walivyofanya usiku huo huko Bethlehemu. Katika Ufunuo ni Yeye aliyefufuka mwenyewe ambaye anasema: “Tazama, nasimama mlangoni na kubisha” (Ufu 3:20). Hebu tufungue mlango wa mioyo yetu. Wacha tuifanye kuwa utoto kwa Mtoto Yesu, na kumfanya ahisi, katika baridi ya ulimwengu, joto la upendo wetu na shukrani zetu zisizo na kikomo! Hii si tu historia nzuri ya kishairi; ni kazi ngumu zaidi maishani. Katika mioyo yetu kuna nafasi kwa wageni wengi, lakini kwa bwana mmoja tu. Kumzaa Yesu kunamaanisha kuruhusu ubinafsi wa mtu kufa, au angalau kufanya upya uamuzi wa kutoishi tena kwa ajili yetu wenyewe, bali kwa ajili yake Yeye aliyezaliwa, akafa na kufufuka kwa ajili yetu (taz. Rm 14:7-9). “Mahali ambapo Mungu huzaliwa, mwanadamu hufa,” umekuwa uthibitisho wa imani fulani ya kutokuwepo kwa Mungu. Ni kweli! Anayekufa, hata hivyo, ni utu wa kale, ulioharibika na unaokusudiwa hata hivyo kuishia katika kifo, huku yule anayezaliwa ni “utu mpya, ulioumbwa katika njia ya Mungu katika haki na utakatifu wa kweli” (Efe 4:24 ) na kuandikiwa kuishi milele. Hii ni ahadi ambayo haitaisha na Noeli, lakini inaweza kuanza nayo. Mama wa Mungu ambaye alimchukua mimba Kristo ndani ya moyoni wake kabla ya kuchukua mimba katika mwili wake, atusaidie kutambua pendekezo letu. Heri ya kuzaliwa kwa Yesu  na Noeli Njema kwenu nyote: Baba Mtakatifu mpendwa Papa Francisko, Mababa, kaka na dada waheshimiwa! Alihitimisha.

22 December 2023, 16:47