Tafuta

2023.11.17.Askofu Mkuu Peña Parra, katika uzindizu wa maonesho katika Madhabahu ya mashahidi huko Seosomun, Seul- Korea Kusini. 2023.11.17.Askofu Mkuu Peña Parra, katika uzindizu wa maonesho katika Madhabahu ya mashahidi huko Seosomun, Seul- Korea Kusini. 

Seoul,Askofu Mkuu Peña Parra kwa waseminari:ikumbatieni imani kw

Katibu Msaidizi wa Sekretarieti ya Vatican alihitimisha ziara ya Korea Kusini kwa Misa na salamu kwa seminari kuu ya mji mkuu: kuwa wachungaji wenye mizizi katika maisha ya watu na mapadre "wazi, wenye furaha na wanaopatikana.

Osservatore Romano

Mapadre wanaitwa kwanza kabisa kuleta furaha ya Injili kwa kila mtu, si kwa maneno tu bali zaidi ya yote kwa kutoa maisha yao yenyewe. Askofu Mkuu Edgar Peña Parra, Katibu Msaidizi wa  Sekretarieti Vatican, aliyasema hayo katika salamu zake Jumamosi tarehe 18 Novemba 2023, kwa jumuiya ya seminari kuu ya Seoul wakati wa kuhitimisha misa aliyoiadhimisha. Hiki kilikuwa ni kitendo cha mwisho cha ziara yake nchini  Jamhuri ya Korea iliyoanza  tarehe 17 Novemba 2023, ambapo Askofu Mkuu Parra alishiriki katika matukio mbalimbali ya Kanisa la mahali hapo, akikutana pamoja na mambo mengine, Rais wa Baraza la Maaskofu Katoliki nchini Korea (CBCK) , Askofu  Matthias Ri Iong-hoon, wa Suwon, na kisha Baraza la Kudumu la  Baraza hilo hilo.

Askofu Mkuu Parra akihutubia wakati wa uzinduzi wa maonesho katika Madhabahu ya Mashaidi huko Seosomun
Askofu Mkuu Parra akihutubia wakati wa uzinduzi wa maonesho katika Madhabahu ya Mashaidi huko Seosomun

Akiendelea Askofu Mkuu alisema kuwa, “Zawadi ya thamani ya wito wa ukuhani, ni kukumbuka historia yenu, ya mashahidi wengi ambao wameikubali imani kwa ujasiri, ya safari ile ya watu ambayo wito wa ukuhani ulizaliwa na kukomaa. Mzizi huu katika ukweli halisi utawasaidia kuwa wachungaji waliofanyika mwili katika maisha ya watu na makuhani ambao, kwa shauku juu ya utangazaji wa Injili, wazi, furaha na kupatikana, wanajua jinsi ya kuwa wachungaji wenye huruma kama Yesu, wanaoweza kuwa na ukaribu na ubinadamu."

Askofu Mkuu Parra akitembelea maonesho katika madhabahu ya mashahidi huko Seosomun
Askofu Mkuu Parra akitembelea maonesho katika madhabahu ya mashahidi huko Seosomun

Askofu Mkuu Peña Parra akikumbuka maneno ya Papa Francisko,  kuhusu Mtakatifu Andrew Kim alisema "alikuwa na anabakia kuwa shuhuda fasaha wa bidii kwa ajili ya kutangaza Injili." Kiukweli, "hata ndani ya usiku wa giza wa mateso ambayo Peninsula ya Korea imepitia furaha ya Injili imetiririka kama mto uliojaa wa maji safi na imerutubisha ardhi hii, ikizalisha jumuiya ya Kikristo yenye bidii katika imani na yenye kutia moyo katika mioyo ya vijana wengi kama nyinyi ni wito wa kumfuata Bwana katika njia ya kuwekwa wakfu maalum.

Mahubiri ya Askofu Mkuu Pena Parra huko Seul , Korea Kusini
20 November 2023, 17:00