Tafuta

2023.05.13 Hii ni Picha ya wakati wa Rozari Takatifu katika Uwanja wa Mtakatifu Pietro tarehe 6 Mei 2023. 2023.05.13 Hii ni Picha ya wakati wa Rozari Takatifu katika Uwanja wa Mtakatifu Pietro tarehe 6 Mei 2023. 

Kila Jumamosi ya Oktoba ni Rosari aux flambeaux katika Uwanja wa Mt.Petro

Kila Jumamosi ya mwezi Oktoba 2023 kutakuwa na sala ya Rosari katika Katika uwanja wa Mtakatifu Petro kwa maandamano na wakiwa wameshikilia mishumaa.Washiriki wa Sinodi wanaombwa uwepo wao na kuwaalika waamini wote na wote wenye mapenzi mema kushiriki sala hii kwa kumuomba Mama Maria.

Na Angella Rwezaula, -Vatican.

Mwezi wa kumi kama ilivyo mwezi wa tano wa kila mwaka ni mwezi wa Mama Maria, mwezi wa kusali Rosari, kumuomba Mama Maria, Mama wa Yes una Mama wa Mungu amani ya dunina na kwa watoto wake, wanahohitaji ulinzi wake. Ni katika muktadha huo ambapo Jumamosi tarehe 7 Oktoba 2023 katika kumbukizi ya Bikira Maria wa Rosari, Matendo ya Rosari aux flambeaux na maandamano na mishumaa mikubwa katika Uwanja wa Mtakatifu Petro itafanyika kuanzia saa 3.00 kamili usiku ambayo ni moja ya mipango wa sala ya Kanisa Kuu la  Mtakatifu Petro katika kipindi chote cha mkutano Mkuu wa XVI wa Sinodi ya Maaskofu ulioanza tarehe 4 Oktoba na utahitimishwa tarehe 29 Oktoba 2023.

Washiriki mkutano huo wanaalikwa kushiriki sala hiyo na watu wotr wenye mapenzi mema. Hata hivyo taarifa inabainisha kuwa kila Jumamosi, usiku kwa mwezi wote wa Oktoba, sala ya Rosari itafanyika katika Uwanja wa Mtakatifu Petro mjini Vatican. Atakayeongoza Rosari ya Jumamosi 7 Oktoba 2023  ni Kardinali Mario Grech, Katibu Mkuu wa Sekretarieti Kuu ya Sinodi.

Nyote mnaalikwa kushiriki kiroho au kimwili kusali.

Tusali Rozari
07 October 2023, 15:27