Tafuta

Utume wa Kardinali Zuppi mara baada ya Ukraine, Urussi na Moscow ni Nchini China. Utume wa Kardinali Zuppi mara baada ya Ukraine, Urussi na Moscow ni Nchini China. 

Kard.Zuppi,China kwa mazungumzo na Li Hui:njia za amani na usalama wa chakula

Kardinali Matteo Zuppi mjumbe wa Papa katika ujumbe wa amani ulioanza nchini Ukraine,Urussi na Marekani,alipokelewa katika Wizara ya Mambo ya Nje ya Jamhuri ya Watu wa China na mwakilishi wa masuala ya Ulaya na Asia.Vatican ilisisitiza kuwa ni hitaji kuchanganya juhudi za kuhimiza mazungumzo na kuelezea matumaini kwamba usafirishaji wa nafaka.

Vatican News

Kardinali Matteo Maria Zuppi, Askofu Mkuu wa Jimbo Kuu Katoliki la Bologna  na Rais wa Baraza la Maaskofu Italia (CEI) alianza ziara yake huko Beijing Nchini China, kama mjumbe wa Papa Francisko kwa ajili ya utume  wa amani ya  Ukraine inayoteswa ambayo ilimwona akitembelea Kyiv, Ukraine, Moscow, Urussi na Washington, Marekani kati ya mwezi Juni na Julai 2023. Taarifa kwa vyombo vya habari kutoka Vatican ililipoti kwamba Kardinali huyo alipokelewa katika mji mkuu wa China katika Wizara ya Mambo ya Nje ya Jamhuri ya Watu wa China na Li Hui, na mwakilishi maalum wa Masuala ya  Ulaya na Asia.

Kutafuta suluhishi hata za nafaka kwa walio hatarini

Mkutano huo kwa mujibu wa   taarifa ya Vatican iliarifu  kuwa ulifanyika katika mazingira ya wazi na ya kirafiki na ulijitolea kwa kutazama vita vya Ukraine na matokeo yake makubwa, ukisisitiza haja ya kuunganisha juhudi za kuhimiza mazungumzo na kutafuta njia zinazoongoza kwa amani. Tatizo la usalama wa chakula pia lilishughulikiwa, kukiwa na matumaini kwamba uuzaji wa nafaka nje ya nchi unaweza kuhakikishwa hivi karibuni, hasa kwa nchi zilizo katika hatari zaidi.

Mjembe wa Papa nchini China
15 September 2023, 16:52