Tafuta

2023.08.16 Kardinali  Paroli,Katibu wa Vatican akiwa Malakal huko Sudan Kusini akiwa kwenye mtumbwi unaowapeleka wakimbizi. 2023.08.16 Kardinali Paroli,Katibu wa Vatican akiwa Malakal huko Sudan Kusini akiwa kwenye mtumbwi unaowapeleka wakimbizi. 

Sudan Kusini:Askofu wa Malakal amesema Kard.Parolin ameleta matumaini

Askofu Stephen Nyodho alimkaribisha Katibu wa Vatican baada ya kuwasili katika jimbo lake.Kardinali yuko nchini Sudan Kusini hadi 17 Agosti.Akiwa Malakal alikutana na wakimbizi waliokimbia vita nchini humo.Askofu anakiri jinsi ambavyo hawana kitu na anatoa wito kwa jumuiya ya kimataifa na watu wenye mapenzi mema.

Na Angella Rwezaula, - Vatican.

Tangu tarehe 14 Agosti, Katibu wa Vatican, Kardinali Pietro Parolin yuko Nchini Sudan Kusini hadi tarehe 17 Agosti 2023. Katika  ziara yake ya tarehe 15 Agosti alikwenda katika Jimbo la Malakal . Katika fursa hiyo Askofu Stephen Nyodho Ador Maiwok wa Jimbo  Katoliki la  Malakal,  amefafanua juu ya matumaini ambayo anafikiri yanabaki kwa waamini na watu wenye mapenzi mema ambao walifika na kumwona Kardinali Pietro Parolin.  Hayo yamethibitishwa wakati akizungumza na mwandishi wa habari wa Radio Vatican/Vatican news ambapo  Askofu Stephen alisema: “Uwepo wa Kardinali Parolin huko Malakal kwa hakika ni muhimu sana, ni ziara inayotoa matumaini, inayoleta upendo wa Kanisa, ziara inayodhihirisha ukaribu na mshikamano wa Kanisa Katoliki kwa watu wanaoteseka".

Kardinali Parolin amefanya uzoefu wa kuona wakimbizi wanaokimbia kutoka Sudan na mtumbwi
Kardinali Parolin amefanya uzoefu wa kuona wakimbizi wanaokimbia kutoka Sudan na mtumbwi

Askofu wa Jimbo la Malakal aidha alisema "Ziara ya Kardinali itawasaidia watu kuelewa kwamba kufanya kazi kwa pamoja, kwa umoja kati ya jumuiya mbalimbali, kutawapa nguvu kubwa ya kwenda mbele, kujenga nchi yao na  jimbo lao.”  Kardinali Parolin akiwa huko asubuhi tarehe 16 Agosti  2023 aliwakaribisha wakimbizi waliokimbia vita nchini Sudan na ambao walifika kwa mtumbwi na kuongozana nao kwenye mtumbwi huo hadi kituo cha mapokezi.

Katika siku kuu ya Bikira Maria Mpalizwa Mbinguni tarehe 15 Agosti, Kardinali  Parolin akiwa huko  Malakal, aliongoza misa Takatifu  katika Kanisa kuu na baadaye alikutana na wakimbizi katika kituo cha mapokezi. Hadi sasa huko Malakal, kaskazini mashariki mwa Sudan Kusini  ambapo Jimbo la Malakal linajumuishwa ndani ya Wilaya ya Upper Nile, Jonglei na Unity, zaidi ya watu 42,000 wamewasili, na takriban 35,000 wamehamishwa, na mara nyingi katika maeneo ambayo kuna baadhi ya wanafamilia. Wakimbizi wengi ni raia wa Sudan Kusini ambao wamehamia Khartoum kwa miaka mingi. Kwa ujumla kuna Wasudan Kusini milioni 1.5 ambao wamewasili Sudan,  na wengi wao sasa wanarejea kutokana na kutoroka vita vinavyoendelea vya wenyewe kwa wenyewe.

Kardinali Parolin akiwa katika Mtumbwi na wakimbizi huko Sudan Kusini
Kardinali Parolin akiwa katika Mtumbwi na wakimbizi huko Sudan Kusini

Nchini Sudan Kusini yote inakadiriwa kuwa karibu watu 200,000 wamewasili. Wakimbizi hao wanapowasili, karibu kila mara wameibiwa kila kitu, wengi huchukuliwa kutoka mpakani hadi Malakal kwa mtumbwi wa mizigo ya Jimbo ambao kwa kawaida husafirisha nafaka, lakini ambayo sasa inatumika kwa ajili ya  watu, kati ya 400 na 800 kwa safari moja. Na hivyo  takriban siku 2-3. Mtumbwi huo huo ambao Kadinali Parolin alipanda  tarehe 16 Agosti 2023. Na kufika hadi sasa ni watu 3,000 ambao wamesafirishwa na mfumo huo. Kwa mujibu wa Askofu  Nyodho Ador Maiwok katika maelezo kwa Vatican New,  amethibitisha kuwa  Jimbo hilo ni mojawapo ya walioathirika zaidi na majanga ya asili na pia imeharibiwa na vita. Jimbo hilo sasa linapokea maelfu ya watu wanaokimbia vita nchini Sudan. Kwa hiyo Jimbo la  Malakal, lilikuwa  moja ya  kuanza  kuingilia kati na kuunda daraja la kuwaleta wakimbizi kutoka mpaka na Sudan hadi Malakal.

“Watu hapa wanahitaji amani na upatanisho, wanahitaji umoja, kama Papa alivyoonesha alipokuja mwezi  Februari uliopita. Na ziara ya Kardinali sasa ina maana kubwa sana kwetu, itasaidia watu kuelewa kwamba ni lazima tuwe wamoja, tuwe na nguvu ya kusonga mbele, hata kama si rahisi, maana ni wale wale waliogombana wenyewe kwa wenyewe ambao waliua kila mmoja, na hivyo inachukua muda mrefu kuwaleta pamoja. Ilikuwa ni ziara ya Papa ambayo ilitupatia nguvu kubwa na matumaini makubwa ya upatanisho kati ya watu wa Nile, ambayo ni muhimu sana,” alisema Askofu wa Malakal.

Kardinali Parolin akiwa katikati ya wakimbizi huko Malakal , Sudan Kusini
Kardinali Parolin akiwa katikati ya wakimbizi huko Malakal , Sudan Kusini

Askofu Nyodho Ador Maiwok,  akiendelea alisema “Vita vilileta uharibifu na uporaji,  na hakuna chochote kilichosalia hapa, watu wanaokuja nyumbani kwako wanawezaje kusaidiwa katika hali hii? Mfano anaoufanya Kardinali ni wa huruma kwani safari moja ya kuleta watu kutoka mpaka hadi Malakal inagharimu  dola elfu 7 hadi nane, kwa ajili ya mafuta tu, baada ya hapo unapaswa kutoa chakula, makazi, na sasa magonjwa pia yanalipuka.” Kwa kuongeza amesema “Hatuwezi kubaki tumeketi, ndiyo maana tunajaribu kusonga mbele, ili kufanya kile tunachoweza, kulingana na uwezo wetu. Wito ni kwa jumuiya ya kimataifa, kwa washirika, kwa watu wenye mapenzi mema, kwa sababu hali hapa inahitaji watu wenye mapenzi mema, inahitaji ubinadamu, ili tuweze kusaidia.

Akiwa Malakal, Kardinali alivalishwa nguo za kiutamaduni
Akiwa Malakal, Kardinali alivalishwa nguo za kiutamaduni

Kwa kuhitimisha Askofu wa Malakal maelezo yake ni ya  kusikitisha kwamba, “kumekuwa na mateso na wanaendelea kuteseka sana. Mvua inanyesha siku hizi, ni msimu wa mvua, na watu hawana chochote cha kujifunika, na watoto na wazee wanahitaji msaada mkubwa.”

Kardinali parolin Malakal, Sudan Kusini
16 August 2023, 15:49