Tafuta

Papa Francisko amekutana na kuzungumza na Rais wa Madagascra Andry Rajoelina, 17 Agosti 2023. Papa Francisko amekutana na kuzungumza na Rais wa Madagascra Andry Rajoelina, 17 Agosti 2023. 

Papa Francisko amekutana na Rais Rajoelina wa Madagascar

Rais wa Jamhuri ya Madagascar amekutana na papa na ambaye mara baada ya mkutano huo amekutana na Monsinyo Miroslaw Wachowski,Katibu msaidizi wa Vatican kwa ajili ya Mahusiano na Nchi.Katika mazungumzo yao wameonesha uhusiano mzuri kati ya nchi hizi mbili na jitihada za utafutaji wa ujenzi wa amani.

Na Angella Rwezaula, - Vatican.

Baba Mtakatifu Francisko tarehe 17 Agosti 2023, amekutana na Bwana Andry Nirina Rajoelina, Rais wa Jamhuri ya Madagascar ambaye mara baada ya mkutano huo amekutana na Monsinyo Miroslaw Wachowski, Katibu msaidizi wa Vatican kwa ajili ya Mahusiano na Nchi.  

Rais wa Madagascar akipokelewa katika Jumba la Kitume
Rais wa Madagascar akipokelewa katika Jumba la Kitume

Kwa mujibu wa Taarifa kutoka Ofisi ya Vyombo vya habari vatican imeeleza kuwa  Rais wa Madagascar alifika saa 5.00 kamili na kuhitimisha mazungumzo saa 5.20, wakati huo huo  mkutano wote umemalizika saa 5.30. Katika mazunguzmo yao na Katibu Msaidizi wa Vatican viongozi hawa, wamepongezana kuhusu uhuasiano wao chanya uliopo kati ya nchi hizi mbili, ikiwa ni pamoja na mchango wa Kanisa Katoliki katika sekta nyingi za jamii ya Madagascar.

Papa na Rais wa Madagascar
Papa na Rais wa Madagascar

Katika mwendelezo wa mazungumzo hayo, walijikita pia juu ya  masuala mbalimbali ya kitaifa na kimataifa, ikiwa ni pamoja na vita vya Ukraine na matokeo yake ya kimataifa, hali ya mgogoro inayoathiri bara la Afrika na uwezekano wa kuendelea na utafiti wa kuandaa rasimu ya makubaliano baina ya nchi hizo mbili kama ishara zaidi ya ushirikiano wa heshima.

Picha ya Pamoja na Uwakilishi
Picha ya Pamoja na Uwakilishi

Kama kawaida ya ugeni huo na  mkutano huo wa faragha kati ya Baba Mtakatifu Francisko na Rais wa Madagascar, mara baadaye Baba Mtakatifu amekaribisha ujumbe uliomsindikiza Rais na kupiga picha pamoja wakiwa mbele ya picha ya Meli ambayo  Papa alizawadiwa wakati wa Hija yake ya Kitume nchini Madagascar. Baadaye wamesali pamoja mbele ya picha ya Maria aliyozawadiwa na Maaskofu wa Madagascar, na kuhitimisha akiwabariki.

Mkutano wa Rais na Katibu Msaidizi wa Vatican wa Masuala ya Ushirikano na Mataifa
Mkutano wa Rais na Katibu Msaidizi wa Vatican wa Masuala ya Ushirikano na Mataifa

Katika kupeana zawadi, Baba Mtakatifu ametoa Hati za kipapa ambazo ni: Ujumbe wa Amani kwa mwaka 2023, Hati za kipapa na Kitabu cha Statio Orbis kunachelezea Njia ya Msalaba ya tarehe 27 Machi 2020,katikati ya Janga la Uviko, kilichaoandaliwa na nyumba ya vitabu ya Vatican(LEV). Na zawadi ya Sanamu ya shaba yenye ujumbe: “Kuweni Wajumbe wa Amani”

Kubadilishana zawadi kati ya Rais na Papa Francisko
Kubadilishana zawadi kati ya Rais na Papa Francisko

Kwa upande wake  Rais wa Madagascar, Bwana Andry Rajoelina amemzawadia  Papa Mchoro unaoonesha mandhari ya maisha ya wakulima wa Malagashi na Mchezo wa 'Solitaire', wenye marumaru yaliyotengenezwa kwa mawe mahalia.

Papa akutana na Rais wa Madagascar
17 August 2023, 15:56