Tafuta

2023.08.17 Kardinali Parolini amekaribishwa katika Jimbo la Rumbek mahali ammbapo ameadhimisha misa kwa ajili ya amani na mapatano 2023.08.17 Kardinali Parolini amekaribishwa katika Jimbo la Rumbek mahali ammbapo ameadhimisha misa kwa ajili ya amani na mapatano 

Sudan Kusini:Kard.Parolin akaribishwa jimbo Rumbek na kuadhimisha Misa

Kardinali Parolin,Katibu wa Vatican,ikiwa ni siku yake ya mwisho ya Ziara yake nchini Sudan,Alhamisi 17 Agosti amekwenda Jimbo la Rumbek mahali ambapo amekaribishwa na kuadhimisha Misa Takatifu.Ametoa mwako kwa kila mtu kutembea kwenye njia za amani na upatanisho kwa manufaa ya nchi.

Na Angella Rwezaula, - Vatican,

Katibu wa Vatican, Kardinali Pietro Parolin tangu tarehe 14 Agosti 2023 alisafiri kwenda Nchini Sudan Kusini ambapo siku yake ya nne na ya mwisho, tarehe 17 Agosti 2023 ilimpeleka katika Jimbo la Rumbek asibuhi, baada ya kutembelea Jimbo la Malakal lenye wakimbizi wengi kutoka Sudan, na ambao wamejaribiwa na mikasa kadhaa ya vita ikiwemo hata mikasa ya asili kama mafuriko.

Misa kwa ajili ya kuombea amani na mapatano nchini Sudan Kusini
Misa kwa ajili ya kuombea amani na mapatano nchini Sudan Kusini

Katibu wa Vatican, Kardinali Pietro Parolin, akiwa huko ameadhimisha Ibada ya Misa Takatifu katika mji wa Rumbek, Sudan Kusini ikiwa ni kuhitimisha ziara yake nchini Sudan Kusini, ambapo Kardinali ametoa mwaliko kwa watu wote kutembea katika njia za amani na upatanisho kwa manufaa ya nchi.

Misa ya Asubuhi huko Rumbek iliyoongozwa na Kardinali Parolin
Misa ya Asubuhi huko Rumbek iliyoongozwa na Kardinali Parolin

Hata hivyo Kardinali Parolin baada ya kupokelewa aliwasalimia wote na kushukuru sana mkuu wa mkoa kwa maneno ambayo aliyasema mara alipofika hapo Rumbek. Kwa njia hiyo alieleza furaha yake kuwa hapo na wao. Kama wanavyojua, hiyo ilikuwa ni ziara ya tatu nchini Sudan. Na hivyo Kardinali aliongeza kusema: “Ninakuwa sasa  raia wa Sudan Kusini, ziara ya nne. Lakini daima ni furaha kuwa hapa.” Akiendelea ameeleza lengo lake la kufuata njia ya Papa Francisko ambaye alikwenda  jijini Juba, Sudan Kusini, mwezi  Februari uliopita kama wanavyokumbuka vizuri.

Hii ni picha ya pamoja mara baada ya Misa Takatifu na Kardinali Parolin
Hii ni picha ya pamoja mara baada ya Misa Takatifu na Kardinali Parolin

Kardinali alisema: “Ilikuwa ni ziara ya kiekumeni na askofu mkuu wa Canterbury na Msimamizi wa Kanisa la Presbyterian la Scotland ili tu kukuza, kuimarisha, mchakato wa amani, upatanisho na amani nchini Sudan Kusini.” Amesema. Kwa kuongeza: “Basi na hilo pia ndilo dhumuni la ziara yangu hapa kufuatia maelekezo ya  Baba Mtakatifu”.

Kwaya wakati wa misa na Kardinali Parolin huko Rumbek
Kwaya wakati wa misa na Kardinali Parolin huko Rumbek

Aidha Kardinali alieleza  alivyokuwa huko Malakal, ambao  ulikuwa mwaliko wa Askofu kwa “sababu ya shida ya watu waliohamishwa na wakimbizi ni muhimu sana huko. Binafsi ameona kinachoendelea huko”. “Lakini bila shaka, Askofu Christian alipojua kuhusu kuja kwangu Sudan, alisema: “mbona ni safari fupi  kufika Rumbek?” na kwa hiyo anikasema basi, ninafuraha hata mwaliko wako. Na hii ndiyo sababu niko hapa ili  kushiriki nanyi wakati huu wa imani, wa sala, wa ushirika katika Kanisa Asante sana .” Alihitimisha kwa kuwatakia kila la heri.

Kard Parolin huko Rumbek Kusini Sudan
17 August 2023, 15:15