Tafuta

Papa ameteua Jimbo jipya na kumteua Askofu wa Kwanza wa Jimbo la Koumra nchini Chad Papa ameteua Jimbo jipya na kumteua Askofu wa Kwanza wa Jimbo la Koumra nchini Chad 

Chad:Papa amemteua Mhs,Padre Tibinger kuwa askofu wa kwanza wa Koumra

Papa amechagua Jimbo jipya la Koumra,eneo lililogawanya kutoka Jimbo la Sarh, kama sehemu ya Jimbo Kuu la N'Djaména nchini Chad na kumteua Askofu wake wa kwanza,Mhashimiwa Padre Samuel Mbairabé Tibingar, wa Jimbo Kuu la N'Djaména.

Na Angella Rwezaula,- Vatican.

Baba Mtakatifu Francisko amechagua Jimbo jipya la Koumra, lenye eneo lililotengwa na jimbo la Sarh, na kulifanya kuwa jimbo kutoka katika  Jimbo kuu la N'Djaména na wakati huo huo Jumamosi tarehe 12 Agosti 2023, Baba Mtakatifu amemteua askofu wa kwanza wa Jimbo jipya la Koumra, Mhashamiwa Samuel Mbairabé Tibingar, wa  N'Djaména, ambaye hadi uteuzi huo alikuwa ni makamu jimbo hilo hilo. Askofu mteule Samuel Mbairabé Tibingar alizaliwa huko Sarh tarehe 27 Julai 1972 na akapewa daraja la Upadre mnamo  tarehe 26 Novemba 2005. Baada ya masomo yake ya Sekondari alijunga na Seminari Kuu Shirikishi ya Mtakatifu Luc de Bakara huko N'Djaména (1997-2004).

Masomo ya juu

Alipata leseni ya Maandiko Matakatifu katika Taasisi ya Kipapa ya Kibiblia huko Roma (2007-2011) na udaktari katika Kitivo cha Taalimungu nchini Italia ya Kati huko Firenze kati ya(2011-2016). Aidha ameshika nyadhifa zifuatazo: Paroko msaidizi wa Kanisa Kuu la N'Djaména (2005-2006), Paroko wa Mtakatifu Paul de Kabalaye huko N'Djaména (2006-2007); Mshiriki wa Parokia ya Watakatifu Martinona Giusto huko Lucardo Alto, huko Flirenze; Mkufunzi katika Seminari Kuu Shirikishi  ya Sarh na kisha Gambera (2017). Tangu 2021 amekuwa Makamu wa Jimbo Kuu la N'Djaména.

Takwimu za Jimbo jipua la Koumara

Jimbo jipya la Koumra nchini Chad linaendana na Wiklya ya  kiraia ya Mandoul, ambalo jiji la Koumra ni mji mkuu wake. Mkowa una wilaya 6, zilizogawanywa katika tarafa 15, na inashughulikia eneo la kilomita za mraba 17,330, na idadi ya watu wapatao 900,000. Jiji lilikuwa kituo cha utume na parokia zote zinazozunguka zilikua nje yake. Kwa kugawanya  Jimbo kuu la N'Djaména, makao ya jimbo jipya ni mji wa Koumra. Kanisa kuu la Mzunguko mpya wa Kikanisa ni Kanisa la sasa la Parokia ya Mtakatifu Teresa wa Mtoto Yesu, huko Koumra.

12 August 2023, 14:23