Tafuta

Wakimbizi wa Sudan wakielekea Chad. Wakimbizi wa Sudan wakielekea Chad. 

Wasiwasi wa Vatican kuhusu ghasia nchini Sudan

Tamko la Utume uwakilishi wa kudumu wa Vatican katika Umoja wa Mataifa na mashirika mengine ya kimataifa huko Geneva wakati wa Kikao cha 36 Maalumu cha Baraza la Haki za binadamu kuhusu Mktadha wa haki za binadamu katika mgogoro unaoendelea nchi za Afrika hasa Sudan.Inahitajika dhamana msingi na misaada ya kibinadamu kwa watu wanaoteseka

Na Angella Rwezaula, - Vatican.

Katika Ujumbe kutoka kwa Mwalikishi wa Kudumu wa Vatican katika Ofisi za Umoja wa Mataifa huko Geneva ameonesha wasiwasi wake mkubwa kutokana na hali  mbaya ya migogoro na vurugu inayoendelea nchini Sudan. Katika hotuba yake iliyotolewa tarehe 11 Mei 2023, katika Kikao Maalum cha 36 cha Baraza la Madiwani kuhusu athari za haki za binadamu za vita vinavyoendelea katika nchi ya  Kiafrika, na ongezeko la mateso ya watu,  Vatican  inapenda kuhakikisha ukaribu wake wa kiroho, sala zake na mshikamano wake na watu wa Sudan, hasa waliohamishwa na wakimbizi.”

Kwa hiyo Wasiwasi mkubwa hasa ni atahari za  kibinadamu za mzozo na hivyo  Vatican inatoa  mwaliko unaoelekezwa kwa wahusika wote, kusimamisha mashambulizi ya silaha na kuhakikisha upatikanaji wa zana  msingi na muhimu kwa raia, popote zinapohitajika, ambayo inajumuisha uwezekano wa kusambaza usaidizi wa kibinadamu wa usalama. Kuhusiana na hilo hata hivyo Vatican ina matumaini ya  kwamba makubaliano yanaweza kurefushwa na kuheshimiwa kikamilifu na kwamba mazungumzo kati ya wawakilishi wa pande zote zinazozozana na kuweza  kuleta makubaliano yenye tija kwa usitishaji vita na masuluhisho ya amani na ya kudumu, kwa maslahi ya idadi ya watu wa Sudan, pamoja na kuepuka hatari ya kuenea kwa ghasia katika nchi jirani, na kudhoofisha amani na usalama wa kikanda.

Kwa kuhitimisha ujumbe  wake mwakilishi wa Kudumu wa Vatican anabainisha  uhakika wake  kwamba “mazungumzo, katika roho ya udugu, yanaweza kuleta muafaka wa amani ya haki na ya kudumu. Kwa hiyo, ombi la Papa Francisko linasisitizwa tena  la kuombe kweka sialaha chini na kuanza tena njia ya amani na maelewano pamoja.

12 May 2023, 16:25