Tafuta

Makao  ya Umoja wa Mataifa jijini Geneva. Makao ya Umoja wa Mataifa jijini Geneva.  (BENEDETTA BARBANTI)

Askofu Nwachukwu:kipaumbele cha Elimu na mabadiliko ya tabianchi

Katika hotuba kwenye Makao ya Umoja wa Mataifa na Mashirika Mengine ya Kimataifa,Mwakilishi wa Kudumu wa Vatican amehutubia kuhusu ulinzi wa haki za Binadamu kwenye muktadha wa mabadiliko ya tabianchi na haki ya Elimu.

Na Angella Rwezaula – Vatican.

Mwakilishi wa Kudumu wa Vatican  katika Makao ya Umoja wa Mataifa na Mashirika Mengine ya kimataifa jijini Geneva alitoa hotuba  mnamo tarehe 23 Juni katika Kikao cha 50 cha Baraza la Haki za Binadamu kuhusu ulinzi wa haki za binadamu katika muktadha wa mabadiliko ya tabianchi na  haki ya elimu. Askofu Mkuu Fortunatus Nwachukwu akizingumza kuhusu haki ya elimu alisema Vatican inazingatia Ripoti  ambayo inazingatia athari za elimu ya kidijitali juu ya haki ya elimu. Kama ilivyooneshwa katika kipindi cha janga la uviko, teknolojia za kidijitali zina jukumu linaloongezeka kila wakati katika elimu ya watoto. Ingawa teknolojia kama hizo ziliwawezesha mamilioni ya watoto duniani kote kuendelea na masomo yao kupitia masomo ya masafa, watoto wengine wasiohesabika, hasa katika nchi zilizoendelea na zinazoendelea, hawakuweza kupata uwezekano huo, na hivyo kusukuma  katika athari halisi ya teknolojia ya kidijitali na kuleta mgawanyiko wa kufurahia haki ya elimu.

Wakati huo huo, ni lazima kusisitizwa kwamba kujifunza  kwa masafa kamwe kusiwe suluhisho  la muda mrefu, badala yake ni hasa elimu ya ana kwa ana. Kwa hakika, elimu haiwezi kupunguziwa katika kupata ujuzi tu bali lazima ionekane katika muktadha wa maendeleo kamili na shirikishi ya mwanadamu. Kama  ilivyoonesha katika ripoti hiyo, mazingira ya elimu huwapa watoto mwingiliano muhimu wa kibinadamu ambao ni wa msingi kwa ukuaji wa kihisia, maadili na kisaikolojia wa mtu huyo. Kuhusiana na hilo, Baraza Kuu pia lingependa kusisitiza jukumu la msingi la wazazi katika malezi na malezi ya watoto wao, ikiwa ni pamoja na haki ya kuchagua shule kwa ajili ya watoto wao, kwa kuzingatia imani au maadili yao. Mwaka 2019 Papa Francisko alizindua Mkataba wa Kimataifa wa Elimu ili kuhamasisha kujitoa upya kwa elimu ya watoto na vijana sio tu darasani, lakini pia katika familia na jamii. Kwa hakika, kama Papa Francisko anavyothibitisha, lengo letu la pamoja ni kuhakikisha kwamba kila mtu anapata elimu bora inayoendana na hadhi ya binadamu na wito wetu wa pamoja kwa udugu [...] Na tudumishwe na imani kwamba elimu, huzaa ndani yake mbegu ya matumaini. Ni  tumaini la amani na haki; tumaini la uzuri na wema na tumaini la maelewano ya kijamii”.

Katika hotuba yake ya kuhusiana na mabadiliko ya Tabianchi, Askofu Mkuu Fortunatus Nwachukwu, alibanisha jinsi ambavyo Vatican inazingatia kuhusiana na Ripoti maalum iliyotolewa ya uhamasishaji na ulinzi wa haki za binadamu katika mazingira ya mabadiliko ya tabianchi. Leo hii kuliko wakati mwingine wowote,  alisema mabadiliko ya tabianchi yanaleta hatari kubwa ambazo zinaweza kuathiri vibaya ukuzaji na ulinzi wa haki za binadamu na hadhi ya binadamu. Ingawa majanga mengi ya haraka yanaikabili jumuiya ya kimataifa, ni lazima mtu asipuuze au kudharau umuhimu wa kushughulikia matokeo mabaya ya utoaji wa hewa ukaa na unyonyaji hovyo wa rasilimali kwenye nyumba yetu ya pamoja.

Mgogoro wa tabianchi una uso wa mwanadamu. Madhara yake tayari ni ukweli kwa umati wa watu duniani kote. Ingawa matokeo mabaya ya mabadiliko ya tabianchi yanaathiri familia nzima ya binadamu, yana athari zisizo sawa kwa maskini na wale walio katika mazingira magumu. Ingawa nchi zenye maendeleo duni na nyingine zinazoendelea zimechangia katika sehemu ndogo tu ya kuongezeka kwa gesi chafuzi, mara nyingi ndizo za kwanza kukumbwa na matokeo yake mabaya, ikiwa ni pamoja na majanga ya asili, mafuriko na ukame.

Mwakilishi wa Kudumu, Askofu Mkuu aliongeza kusema kwamba “hii ni kweli hasa kwa Nchi za visiwa vidogo zinazoendelea ambazo mara nyingi hulazimika kutumia rasilimali kubwa kujenga upya baada ya majanga kama haya ambayo yanazidi kuwa ya mara kwa mara. Ni kupitia tu juhudi za pamoja katika ngazi zote, katika roho ya mshikamano wa kimataifa, tutaweza kutekeleza ipasavyo masuluhisho ya kudumu kwa mzozo wa hali ya hewa. Kama Papa Francis alivyosema, “suala la hili. […] Kwa hivyo inasumbua kwamba, pamoja na muunganisho mkubwa wa shida, tunaona mgawanyiko unaokua wa suluhisho.

HOTUBA ZA MWAKILISHI WA KUDUMU WA VATICAN KATIKA UN HUKO GENEVA
24 June 2022, 16:00