Tafuta

2021.11.25 Papa amekutana na Waziri Mkuu wa Lebano na familia yake 2021.11.25 Papa amekutana na Waziri Mkuu wa Lebano na familia yake 

Papa Francisko:Lebanon ina ujumbe mzuri wa kuweza kuamka tena na kuanza upya!

Baba Mtakatifu Francisko akikutana na Waziri Mkuu wa Lebanon,Bwana Mikati, amemwakikishia ukaribu wa Nchi ijulikanayo ya Mwerezi.Katika mazungumzo na Katibu wa Vatican wamejikita kutazama hali ya sasa ya watu wa Lebanon wanayoishi hasa kwa mtazamo wa mgogoro wa kisiasa na hali za kiuchumi kijamii.

Na Sr. Angella Rwezaula – Vatican.

Baba Mtakatifu FranciskoAlhamisi tarehe 25 Novemba 2021 amekutana na Waziri Mkuu nchini Lebanon Bwana  Najib Mikati, ambaye mara baada ya mazungumo  yao amewakilisha familia yake katika ukumbi wa Clementina na kubadilishana  zawadi.  Mara baada ya kubadilisha zawadi hizo  Papa amesema maneno machache kuwa Nchi ya Lebanon inajieleza  ujumbe wake wa ahadi na kwa maana hiyo lazima kuupambania.

Mkutano wa Papa na Waziri Mkuu wa Lebanon
Mkutano wa Papa na Waziri Mkuu wa Lebanon

Baba Mtakatifu ameongeza kusema kwamba Lebanon inapitia vipindi vibaya sana na vigumu na amewakikishia sala zake, ukaribu wake na jitihada zake ili nchi hiyo iweze kuwa na  nguvu za pamoja  katika kusaidia nchi hiyo ipata kuamka tena.   Katika hilo Papa amekumbusha kifungu cha sehemu ya Injili ambayo Yesu alikwenda katika nyumba ya Gairo, aliyekuwa na mtoto amekufa na  kumshika mtoto akisema “ hamka” na kwa kufananisha na hiyo amesema “Bwana anashika mikono ya Lebanon na kusema “amka”.

Mkutano wa Papa na Waziri Mkuu wa Lebanon
Mkutano wa Papa na Waziri Mkuu wa Lebanon

Kabla ya kuagana, Papa Francisko amewaalika wote waliokuwamo kufanya muda mfupi wa sala ya ukimya na baadaye Waziri amekwenda kukutana na Katibu wa Vatican, Kardinali Pietro Parolin huku akisindikizwa na Askofu Mkuu Paul Richard Gallagher, Katibu wa Vatican kwa ajili ya Uhusiano na Ushirikiano na Nchi. Katika mchakato wa mazungumzo yao kwa mujibu wa taarifa za Msemaji wa vyombo vya habari Vatican, wamesisitiza juu ya uhusiano  mwema wa kihistoria uliopo kati ya Vatican na Lebanon na umuhimu wa nafasi ya Kanisa katoliki katika shughuli zake zinazoifunika nchi hiyo. Vile vile wamegusia suala la sasa ambao watu wa Lebanon wanaishi hasa kwa mtazamo wa mgogoro wa kisiasa na hali za kijamii, kiuchumu, wakiwa na matashi mema kwamba haki na ulazima wa kuwa na  magezuo na msaada wa Jumuiya ya kimataifa unaweza kwa dhati kusaidia kutatua matatizo yaliyo jitokeza kwenye Nchi hiyo ya Mwerezi.

Mkutano wa Papa na Waziri Mkuu wa Lebanon
Mkutano wa Papa na Waziri Mkuu wa Lebanon

Na hatimaye viongozi hawa wamezungumzia juu ya umuhimu wa kuhamasisha mukatadha wa uraia  wa kila Mlebanon na kusisitiza umuhimu wa kuishi kwa amani ili nchi ya  Lebanon iendelee kuwa ni jumbe wa amani na udugu ambao unahitajika katika nchi zote za Mashariki ya Kati. Ikumbukwe hata hivyo katika kubadilishana zawadi, WazirioMkuu amemzawadia Papa Francisko Picha ya Kanisa la Kimelkita la Mtakatifu Salvatore ambalo limeharibiwa vibaya  wakati wa mlipuko wa moto mnamo tarehe 4 Agosti 2020. Picha ya ya Papa aliyomzawadia Waziri Mkuu inaonesha  shamba la mizabibu, ambao kuna andiko:“ Tunda la mizabibu na kazi ya binadamu iwe kwetu kinywaji cha wokovu”; Kikasha ndani mwake chenye mkusanyiko wa hati za kipapa ambazo ni ujumbe wa amani wa wa 2021, Hati ya Udugu wa Kibinadamu na Kitabu kuhusu Statio Orbis la 27 Machi 2020, lilichoandaliwa na LEV.

25 November 2021, 17:33