Hija ya kitume ya Papa Francisko Slovakia:habari katika picha
Na Sr. Angea Rwezaula - Vatican.
Katika ibada ya kimungu ya kibizantino Prešov, Papa Francisko amewaonya waamini wasishabikie ukristo wa ushindi bila msalaba na wawi wa kidunia ba tasa.Amewakumbuka hata wale waliokufa nchini Sloovakia kwa sababu ya jina la Yesu. Ni katika kukumbuka siku kuu ya Kutukuka kwa Msalaba. Papa Francisko kabla ya kwenda Kosice, amesimama na kuwasalimia ndugu zake wa Shirika lake la Kijesuit katika Nyumba ya mafungo ya kiroho na wapishi na watawa ambao wanaandaa vyakula vya maaskofu kwa Prešov. Katika ziara hii ya papa Francisko watu wanafuatilia kwa furaha kubwa hatua kwa hatua na maneno yake ya kuwatia moyo. Video na picha vinaelezea hatua zake muhimu za ziara hii ya kitume nchini Slovakia.
Papa Francisko amekuwa mhujaji katika uwanja wa Rybné námestie, mahali penye manara wa kuwakumbuka zaidi ya wayahudi 105 waliuwawa wakati wa ubaguzi ‘Shoah’. Katika hotuba yake amebainisha juu ya kilio cha uchungu kwa sababu ya unyama uliotekelezwa na utawala wa mabavu na amesisitiza kufanya jitihada ili isitokee tena kashfa ya sura ya Mungu kupitia maisha ya kibinadamu. Katika wito wake umehusu kudhibiti kila aina ya ubaguzi na kuwa na matumaini katikati ya ukosefu wa maelewano yanayochafua ulimwengu na vile vile wao wawe washuhuda wa imani.
Picha nzuri sana ni ile ya Papa Francisko mhujaji wa kituo cha Ulaya: Mkutano na Rais wa Slovakia Bi Zuzana Čaputová, mamlaka ya raia na wanadiplomasia, mkutano wa maaskofu, mapadre, watawa na makatekista. Baadaye alisalimia watawa wamisionari wa Upendo na wageni wao katika “nyumba ya Bethlehemu na kukumbatia jumuiya ya kiyahudi wa eneo hilo. Picha zimepighwa na vyombo vya habari Vatican vinavyoambatana na Papa.
Wito wa ufungamanisho, maelewano na ukarimu vimesikika katika maneno ya Papa Francisko wakati wa mkutano huko Bratislava, na viongozi wakuu wa nchi na wanadilomasia katika Ikulu. Papa amesema kuwa "Slovakia iwe behewa kwa ajili ya Ulaya ya mshikamano".