Tafuta

2021.02.25 Mtakatifu Gregorio wa  Narek 2021.02.25 Mtakatifu Gregorio wa Narek  

27 Februari ni Kumbu kumbu kiliturujia ya Mt.Gregory wa Narek

Kwa mujibu wa msemaji wa Baraza la Kipapa kwa ajili ya Makanisa ya Mashariki na Baraza na Kupapa la kuhamasisha Umoja wa Kikristo,wamebainisha juu ya kuwekwa Kumbu kumbu mpya kiliturujia ya Mtakatifu Gregory wa Narek,Abati na Mwalimu wa Kanisa.

Na Sr. Angela Rwezaula – Vatican.

Kwa mujibu wa Kalenda ya Kirumi, baada  ya Kuchapishwa kwa Hati ya Papa Francisko kuhusu  kuwekwa rasimi kila tarehe 27  Februari,  kuwa kumbu kumbu ya kiliturujia ya Mtakatifu Gregorio wa  Narek, Abate na Mwalimu wa Kanisa, Baraza la Kipapa kwa ajili ya Makanisa ya Mashariki na Baraza la  Kipapa la kuhamasisha Umoja wa Kikristo, wameandaa maadhimisho mjini Vatican  Jumamosi tarehe 27 Februari  2021 kwa ushirikiano na Ubalozi wa Jamhuri ya Armenia jijini Vatican.

Maadhiisho ya misa takatifu hiyo itaongozwa na Kardinali Leonardo Sandri, Rais wa Baraza la Kipapa la Makanisa ya Masharikia, asubuhi saa 4.30, katika Kanisa kuu la Mtakatifu Petro na kufuata  baadaye sala ya kiekumene mbele ya sanamu ya Mtakatifu Gregory wa Narek iliyobarikiwa na Papa Francisko mnamo 2018 katika bustani za Vatican.

Pamoja na Kardinali wanatashiriki  misa hiyo, Askofu mkuu Lévon Bogos Zékyian, wa  Istanbul ya Kiarmeni na Mwakilishi wa Kipapa wa Shirika la Kiarmenia pamoja na Askofu Mkuu Brian Farrell, Katibu wa Baraza la Kipapa kwa ajili ya Umoja wa Kikrsito. Katika Sala ya kikumene itaongozwa na mhemimiwa Khajag Ian,  ambaye ni Mwakilishi wa Kanisa la kitume la Kiarmenia, Roma  kwa uwepo wa Kardinali Kurt Koch,  Rais wa Baraza la Kipapa la Uhamasishaji wa Umoja wa Kikristo.

26 February 2021, 14:13