Tafuta

Maaskofu wa Mabararaza ya Maaskfo Afrika kusini Maaskofu wa Mabararaza ya Maaskfo Afrika kusini 

Kanisa la Afrika ya Kusini na Botswana kupata maaskofu!

Papa amemteua askofu msaidizi wa Jimbo Katoliki la Cape Town Afrika Kusini P. Sylvester David, O.M.I aliyekuwa katibu Mkuu wa Jimbo la Durban na kumchagua Askofu Franklyn Atese Nubuasah, S.V.D. aliyekuwa askofu wa Francistown kuwa wa Jimbo la Gaborone nchini Botswana

Na Sr. Angela Rwezaula

Baba Mtakatifu Francisko tarehe 6 Juni 2019  ametangaza Askofu msaidizi wa Cape Town Afrika ya Kusini Mheshimiwa sana Padre Sylvester David, O.M.I., ambaye hadi uteuzi wake alikuwa ni Katibu Mkuu wa Jimbo Kuu la Durban,na kumpatia makao rasmi ya uaskofu huko Gunugo. Na wakati huo Baba Mtakatifu amemtangaza pia Askofu wa Jimbo la Gaborone Botswana, Askofu Franklyn Atese Nubuasah, S.V.D., ambaye hadi uteuzi huo alikuwa ni Askofu wa  Francistown.

 

06 June 2019, 12:50