Tafuta

Mji wa Rozari nchini Argentina umekumbwa na vurugu ya biashara ya madawa ya kulevya. Mji wa Rozari nchini Argentina umekumbwa na vurugu ya biashara ya madawa ya kulevya. 

Papa ahimiza chunguza ufisadi na utapeli wa pesa huko Rozari nchini Argentina

Papa ametuma ujumbe wa video kwa wakazi na taasisi za mji wa Argentina ambao umekuwa eneo la mauaji na uhalifu mwingine wa wauzaji wa dawa za kulevya kwa juma:”Tunahitaji kufanyia kazi usambazaji na mahitaji ya madawa ya kulevya kupitia sera za kuzuia na usaidizi.Ukimya wa Serikali katika uwanja huu unawezesha kukuza matumizi na biashara ya dawa za kulevya."Papa analiomba Kanisa kusindikiza familia za wahanga,wagonjwa,wafungwa na wale wanaopatwa na janga la utumiaji wa dawa hizo.

Na Angella Rwezaula – Vatican.

Baba Mtakatifu Francisko Jumanne tarehe 26 Machi 2024 ametuma ujumbe kwa njia ya video kwa waamini wa Mji wa Rozari nchini Argentina ambao umekumbwa na mlipuko wa vurugu kuhusu zinazohusiana na madawa ya kulevya. Katika ujumbe huo Baba Mtakatifu amebainisha kuwa inamjia akilini  wakati huo huo aya ya Injili ya Matayo isemayo: “Heri wahudumu wa amani”(Mt 5,9). Ni heri. Katika kipindi cha mgogoro kama kile wanachoishi mji wa Rosari, ni kuelewa uhitaji wa uwepo wa nguvu za usalama ili kuleta utulivu wa jumuiya. Hata hivyo tunajua kuwa katika safari ya amani lazima kupitia majibu magumu na fungamani, kwa ushirikiano wa taasisi zote ambazo zinaunda maisha ya jamii. Ni lazima kuongeza nguvu ya jumuiya.  Kila mtu anazo ndani yake zana za kushinda kile kinachotishia uadilifu wake, maisha ya watoto wake dhaifu. Dhidi yenu ambao ni makini, tunahitaji kuimarisha jumuiya. Hakuna mtu mwenye mapenzi mema anayeweza kuhisi au kutengwa na kazi kubwa ya kuhakikisha kwamba Rosari ni mahali ambapo kila mtu anaweza kujisikia kama ndugu.

Ni lazima kutathimini upya siasa 

Papa amesisitiza kuwa "Bila ushiriki wa sekta ya nguvu za kisiasa, mahakama, kiuchumi, kifedha na polisi haingewezekana kufikia hali ambayo mji wa Rosari unajikuta.  Ni lazima kutathimini upya wa siasa ambazo ni wito wa juu sana, ni mojawapo ya aina za thamani zaidi za upendo, kwa sababu inatafuta manufaa ya wote'(Fratelli Tutti 180). Sekta zote za kisiasa zinaitwa kutembea njia kuu ya maafikiano na mazungumzo ili kuzalisha sheria na sera za umma zinazoambatana na mchakato wa kurejesha mfumo wa kijamii. Ubadilishaji wa tawala lazima usaidie mwendelezo wa michakato ya mabadiliko. Tunahitaji kufanya kazi sio tu kwenye usambazaji lakini pia juu ya mahitaji ya dawa za ulevya, kupitia sera za kuzuia na usaidizi. Ukimya wa serikali katika nyanja hii hufanya  ionekane ya asili tu na kuwezesha utangazaji wa matumizi ya dawa za kulevya na uuzaji wao wa kibiashara."

Hakuna uchumi mzuri bila mjasiriamali mzuri

Baba Mtakatifu amebainisha kuwa "Ujasiriamali ni kielelezo cha msingi cha kila uchumi mzuri: hakuna uchumi mzuri bila mjasiriamali mzuri. Kwa bahati mbaya, hakuna hata uchumi mbaya bila ushirikiano wa sehemu ya sekta binafsi. Mjasiliamali ni sura msingi. Kwa hiyo kazi kubwa iko mbele yetu katika sekta ya biashara, si tu kwa kuzuia ushirikiano katika biashara na mashirika ya kimafia, lakini pia kwa kujihusisha kijamii. Kuna mifano mizuri ya hili katika maisha ya ujasiriamali wa Argentina, ikiwa ni pamoja na ya Enrique Shaw. Hakuna mtu anayejiokoa mwenyewe, hata katika vitongoji vya kibinafsi mnaweza kupata ukosefu wa usalama na tishio la matumizi kwa watoto wenu. Amani ni shughuli inayohitaji ubunifu na kujitolea kwa wale wote ambao wana zawadi ya biashara na uvumbuzi, na mnajua jinsi ya kuifanya. Asante kwa hilo."

Kila mfumo wa kimafia masikini ni nyenzo inayotupwa

Askofu wa Roma aidha amekazia kusema kuwa "Kwa kuzingatia kwamba, katika kila mfumo wa kimafia, maskini ni nyenzo zinazoweza kutupwa, ninawakaribisha kufanya juhudi na kuunganisha juhudi ili Serikali na taasisi za kati ziweze kutoa nafasi za jamii katika vitongoji hatarishi. Na mnaweza pia kuunda hali kwa watoto, vijana na vijana kuwa na maendeleo muhimu ya binadamu kwa maisha bora ya baadaye kuliko wazazi na babu na babu zao. Sisi sote - taasisi za kijamii, za kiraia na za kidini - lazima tuwe na umoja kufanya kile tunachofanya vyema zaidi: kuunda jumuiya. Mji wa Rozari unaweza kutegemea utajiri mkubwa wa taasisi katika huduma ya wengine. Ni utajiri mlio nao. Sote tunaweza kushirikiana na kushiriki katika nafasi za michezo, elimu na jumuiya. Hofu daima hujitenga, hofu hupooza. Lazima msiogope kujihusisha pamoja na wengine ili kuwa na jibu la amani na la kutia moyo. Kaka na dada, Kanisa, kama Mama na Msamaria, daima linaalikwa kuzisindikiza kiroho na kimaumbile familia za wahanga waliopoteza maisha kutokana na ukatili, kuwasindikiza wagonjwa, kuwasindikiza wale wanaokumbwa na janga la utumiaji wa madawa ya kulevya na familia zao, kuwasindikiza wale walio gerezani na kisha kuhitaji njia ya kuunganishwa tena, kuwasindikiza wale wanaoishi katika mazingira magumu sana."

Parokia ni Kanisa lililokaribu na jumuiya ya kila mtu ijisikie kupendwa

Hatimaye ametoa ushauri mkuu kwamba "Parokia ni Kanisa ambalo linakuwa karibu, ni jumuiya ambayo kila mtu anaweza kujisikia kupendwa. Kwa watoto wengi, vijana na vijana walio katika mazingira magumu labda itakuwa uzoefu pekee wa familia ambao watapata fursa ya kuijua. Katika nyakati hizi, upendo na hisani vitakuwa tangazo la wazi zaidi la Injili kwa jamii inayohisi kutishiwa. Wapendwa kaka na dada wa Rozari, niko karibu nanyi. Bikira wa Rozari huwaombea watoto wake wote mchana na usiku, zaidi ya yote, kama kawaida ya akina mama, kwa uangalifu maalum kwa wale ambao ni dhaifu zaidi. Mungu awabariki. Ninawakumbatia.” Ujumbe wa Papa Francisko unahitimishwa hivyo.

Papa ametuma ujumbe wa Mji wa Rozari nchini Argentina kutokana na vurugu zinazohusiana na uhalifu
26 March 2024, 16:20