Tafuta

Tunapomtengenezea nafasi Bwana ambaye anatuokoa kutokana na utoshelevu wetu, tunaweza kujifungua kwa kila kiumbe. Tunakuwa njia za maisha na upendo wa Baba. Tunapomtengenezea nafasi Bwana ambaye anatuokoa kutokana na utoshelevu wetu, tunaweza kujifungua kwa kila kiumbe. Tunakuwa njia za maisha na upendo wa Baba.  (Vatican Media)

Papa Francisko:mafungo ya Kikristo,siyo likizo ya ustawi ni kipindi cha kuzaliwa upya

Tunachapisha utangulizi wa Papa katika kitabu: “Kuwa wa Mungu kwanza”cha Austen Ivereigh.Papa anaandika:“kuzorota kwa nyumba yetu ya pamoja na mienendo ya watu wengi ni ishara za mgogoro wa kutokuwa wa mtu wa Mungu.”Mafungo ya kiroho ni kuchaji tena betri zetu,kati ya shinikizo kubwa na mivutano ya jamii yenye ushindani wa kupindukia.

PAPA FRANCISKO

Shukrani kwa uzoefu wake wa maisha, Mtakatifu Ignatius wa Loyola alitambua kwa uwazi mkubwa kwamba kila Mkristo anahusika katika mapambano ambayo hufafanua maisha yake. Ni pambano kushinda jaribu la kujifungia ndani, ili upendo wa Baba uweze kujiimarisha ndani yetu.  Tunapomtengenezea nafasi Bwana ambaye anatuokoa kutokana na utoshelevu wetu, tunaweza kujifungua kwa viumbe vyote na kwa kila kiumbe. Tunakuwa njia za maisha na upendo wa Baba. Na hapo ndipo tunaweza kutambua maisha ni nini hasa: zawadi kutoka kwa Baba ambaye anatupenda sana na anataka tuwe mali yake na ya kila mmoja wetu. Pambano hili tayari limeshashinda kwa ajili yetu na Yesu, kupitia kifo chake cha aibu pale Msalabani na kufufuka kwake. Kwa njia hii baba alitufunulia mara moja na kwa wote na kwa wakati wote kwamba upendo wake una nguvu zaidi kuliko nguvu yoyote katika ulimwengu huu. Lakini hata hivyo, kukumbatia ushindi huu na kuufanya kuwa halisi bado ni changamoto: tunaendelea kujaribiwa kujifunga wenyewe kwa neema hiyo, kuishi kwa njia ya kidunia kwa udanganyifu wa kuwa na uhuru na kujitegemea.

Migogoro hii yote mbaya ambayo inatuzingira ulimwenguni kote, kuanzia na  shida ya kiikolojia hadi vita, hadi dhuluma kwa maskini na dhaifu, ina mizizi katika kukataa huku kuwa mali ya Mungu na ya kila mmoja. Kanisa hutusaidia kwa njia nyingi kupambana na jaribu hili. Mapokeo na mafundisho yake, mazoea ya sala na maungamo na adhimisho la kawaida la Ekaristi ni “njia za neema” zinazotufungua ili kupokea zawadi ambazo Baba anataka kumimina juu yetu. Miongoni mwa mapokeo haya kuna mafungo ya kiroho na kati ya hayo kuna mazoezi ya kiroho ya Mtakatifu Ignatius wa Loyola. Mafungo ya kiroho ili kuchaji tena betri zetu,  yamekuwa maarufu sana, kati ya shinikizo kubwa na mivutano ya jamii yenye ushindani wa kupindukia. Lakini mafungo ya Kikristo ni tofauti sana na likizo ya ‘ustawi.’ Kiini cha tahadhari sio sisi bali ni Mungu, Mchungaji Mwema ambaye, badala ya kututendea kana kwamba sisi ni mashine, anajibu mahitaji ya ndani kabisa ya watoto wake wapendwa.

Mafungo ni wakati ambapo Muumba anazungumza moja kwa moja na viumbe vyake, akiwasha roho zetu kwa “upendo na sifa zake” ili tuweze “kumtumikia Mungu vyema wakati ujao,” kama maneno ya Mtakatifu Ignatius (ES 15). Upendo na huduma: hizi ndizo nguzo mbili za Mazoezi ya Kiroho. Yesu anakuja kukutana nasi, anavunja minyororo yetu ili tuweze kutembea pamoja naye kama wanafunzi na washirika. Ninapofikiria matunda ya Mafungo, ninamwona Yesu mbele yangu akimwambia yule aliyepooza kwenye kidimbwi cha Bethzatha: “Simama, chukua kitanda chako uende!” (Yoh 5, 1-16). Ni amri inayopaswa kutii lakini, wakati huo huo, ni mwaliko wake wa fadhili na upendo zaidi. Mtu huyo alikuwa amepooza ndani. Alijihisi kushindwa katika ulimwengu wa wapinzani na washindani. Alijawa na chuki na uchungu kwa kile alichoamini kuwa amenyimwa, amenaswa katika mantiki ya kujitosheleza, akiamini kwamba kila kitu kinategemea yeye na nguvu zake pekee.

Na alipoona kwamba wengine walikuwa na nguvu na kasi zaidi kuliko yeye, alikata tamaa. Na ilikuwa ni wakati huo huo ndipo Yesu alipomwendea kwa huruma yake na kumsihi atoke ndani yake mwenyewe. Mara tu alipokuwa wazi kwa uwezo wa kuokoa wa Yesu, kupooza kwake - kwa ndani na nje - kunaponywa. Aliinuka na kutembea, akimtukuza Mungu na kufanya kazi kwa ajili ya Ufalme wake, akiwa huru kutoka na ana historia ya kujitosheleza na kujifunza kila siku kutegemea zaidi neema yake. Na ni kwa njia hiyo ndipo anakuwa mfuasi, mwenye uwezo wa kukabiliana vyema zaidi na si tu changamoto za ulimwengu huu, bali pia kutoa changamoto kwa walimwengu ili kutenda kulingana na mantiki ya zawadi na upendo.

Kama Papa, nilitaka kuunga mkono  juu ya kuwa kwanza wa Mungu na kisha kwa ajili ya  uumbaji na kwa ndugu wanadamu wenzetu, hasa wale wanaotulilia. Hii ndiyo sababu nilitaka kukumbuka migogoro miwili mikubwa ya wakati wetu: kuzorota kwa nyumba yetu ya pamoja na uhamiaji,  kuhama kwa watu wengi. Hizi ni dalili mbili za mgogoro wa kutokuzingatia uliolekezwa katika kurasa hizi. Kwa sababu hiyo hiyo nilitaka kutia moyo Kanisa ligundue tena  zawadi ya utumaduni wake wa mapokeo ya kisinodi, kwa sababu linapojifungua kwa Roho huyo anenaye ndani ya Watu wa Mungu, Kanisa lote huinuka na kutembea, likimsifu Mungu na kuchangia kuja kwa Ufalme wake. Nina furaha kuona jinsi mada hizi zilivyo katika “Kuwa kwanza wa Mungu”, zikihusishwa na tafakari za Mtakatifu Ignatius ambazo zimenifunda kwa miaka mingi. Austen Ivereigh amefanya kazi nzuri ya kuleta pamoja tafakari katika mafungo ambayo nilihubiri miongo mingi iliyopita na mafundisho yangu kama Papa. Kwa njia hiyo anaruhusu zote mbili kuaakisi na kuangazwa na mafungo ya kiroho ya Mtakatifu Ignatius.

Huu sio wakati wa kurudi nyuma na kufunga mlango. Ninaona wazi kwamba Bwana anatuita tutoke ndani yetu, tuinuke na tutembee. Anatuomba tusigeuze kisogo mbali na mateso na machozi ya wakati wetu, bali tuingie ndani yao, kufungua njia za neema yake. Kila mmoja wetu, kwa sababu ya ubatizo wetu, ni mojawapo ya njia hizi. Hatua ni kuzifungua - na kuziweka wazi. Ninatumaini kwamba siku hizi nane ambazo unaweza kufurahia upendo Wake zitakusaidia kuhisi wito wa Mungu wa kuwa chanzo cha uzima, tumaini na neema kwa wengine, na kwa njia hii kugundua furaha ya kweli ya maisha yako. Ninatumaini mtapata mafundisho yale  ambayo Mtakatifu Ignatius anazungumza kwamba ‘zaidi ambayo anatuita kugundua kina cha upendo wa Mungu katika mchango mkubwa zaidi wa sisi wenyewe. Na tafadhali, kila wakati mnapokumbuka, msisahau kuniombea, ili niweze kusaidia kila wakati kuwa kwanza kuwa mali ya Mungu.

Dibaji ya Papa kuhusu mafungo ya kiroho
13 February 2024, 11:50