Tafuta

Papa anabainisha kuwa ni wanawake wangapi wamelemewa na uzito na janga la ukatili dhidi yao. Papa anabainisha kuwa ni wanawake wangapi wamelemewa na uzito na janga la ukatili dhidi yao. 

Papa,wanawake wasiwe vigezo vya kuvutia wengine na kuwatawala

Papa Francisko ametoa ombi lake la kuondoa mizizi ya vurugu dhidi ya wanawake katika ujumbe wa Kampeni ya kitaifa dhidi ya aina zote za unyanyasaji na kwamba kiwango chetu cha ubinadamu kinadhihirishwa na jinsi tunavyowatendea wanawake, katika nyanja zao zote.

Na Angella Rwezaula, - Vatican.

Baba Mtakatifu Francisko, ametuma ujumbe wake  kwa ajili ya kampeni ya kitaifa dhidi ya vurugu kwa wanawake iliyoandaliwa na  na Radio I Rai na Cadmi D.I.Re. Katika ujumbe huo, Papa Francisko anawashukuru wahamasishaji wa mpango huo wa   "Masafa ya  muda mrefu dhidi ya unyanyasaji wa wanaume juu ya wanawake", ambao unatuwezesha kutafakari juu ya suala la juu sana. Kwa hakika, unyanyasaji dhidi ya wanawake ni gugu lenye sumu ambalo linasumbua jamii yetu na ambayo lazima liondolewe kutoka katika mizizi. Na mizizi hii ni ya kiutamaduni na kiakili, ambayo hukua katika udongo wa ubaguzi, umilki, na udhalimu. Katika maeneo mengi na hali nyingi sana wanawake huwekwa nyuma, huchukuliwa kuwa "duni", kama vitu: na ikiwa mtu amepunguzwa kwa kitu, basi hadhi yake haionekani tena, inachukuliwa kuwa mali ya mtu ambayo inaweza kutumika katika kila kitu, hata kufikia hatua ya kukandamiza.

Wanawake wengi wanaelemewa na uzito wa janga la ukatili

Baba Mtakatifu amekazia kusema kuwa ni wanawake wangapi wamelemewa na uzito na janga la ukatili! Ni wangapi wanaoteswa vibaya, wananyanyaswa, wanafanywa watumwa, waathriwa wa kiburi cha wale wanaofikiri wanaweza kudhibiti miili yao na maisha yao, kulazimishwa kujisalimisha kwa uchoyo wa wanadamu. Kwa bahati mbaya, vyombo vya habari bado vina jukumu lisiloeleweka katika hili. Kwa upande mmoja wanakuza heshima na kuhamasisha wanawake; lakini kwa upande mwingine wanaendelea kusambaza ujumbe mwingi unaoegemezwa juu ya matangazo ya kibiashara na utumiaji, ambao mifano yao, ya kiume na ya kike, inatii vigezo vya mafanikio, kujithibitisha, ushindani, uwezo wa kuvutia wengine na kuwatawala.

Upendo hauna kifungo

Baba Mtakatifu amebainisha kuwa pakini palipo na kutawaliwa kuna unyanyasaji! Sio upendo unaohitaji wafungwa. Papa amebainisha kuwa Bwana anatutaka tuwe huru na katika hadhi kamili! Kwa kukabiliwa na janga la unyanyasaji wa kimwili na kisaikolojia kwa wanawake, kuna haja ya haraka ya kugundua kwa upya aina za mahusiano ya haki na usawa, kulingana na kuheshimiana na kutambuliwa. Masharti ya kila aina lazima yakabiliwe na hatua za kielimu ambazo, kuanzia kwenye familia, na  zinamweka mtu huyo na utu wake katikati. Ni jukumu letu, jukumu la kila mtu, kutoa sauti kwa dada zetu wasio na sauti: wanawake ambao ni waathriwa wa unyanyasaji, unyonyaji, kutengwa na shinikizo lisilofaa. Tusibaki kutojali! Ni muhimu kuchukua hatua mara moja, katika ngazi zote, kwa uamuzi, uharaka na ujasiri.

Kiwango cha binadamu kinapimwa jinis tunavyowatendea wanawake

Baba Mtakatifu Francisko amekazia kusema kuwa ni kutoka katika moyo na mwili wa mwanamke wokovu ulikuja ulimwenguni. Na kwa njia hiyo  kiwango chetu cha ubinadamu kinafichuliwa kwa  jinsi tunavyowatendea wanawake, katika nyanja zake zote. Ni Matumaini ya Baba Mtakatifu kwamba kampeni ya masafa ambayo yameanza  ni marefu sana na yanaweza kuchangia mabadiliko ya fikra. Amewabariki na kuwahimiza wasonge mbele katika ahadi hiyo. Amewapongeza  kwa kazi hiyo nzuri na kuhitimisha ujumbe wake.

Papa katika ujumbe wa kampeni ya wanawake anasema kipimo cha mwanadamu kinapimwa kwa jinsi tunavyowatendea wanawake
09 November 2023, 14:40