Tafuta

2023.11.08  Tuombee amani duniani. 2023.11.08 Tuombee amani duniani.  (Vatican Media)

Papa atoa wito wa kuacha vita.Kuna mateso makubwa!

Mara baada ya katekesi yake Papa amerudia kutoa wito tena wa kuwaombea watu wanaoteseka kutokana na migogoro mbalimbali,akikumbuka hasa Ukraine inayoteswa na Waisrael na Wapalestina.Wanakabiliwa na maumivu yanayoteseka na watoto,wazee,wagonjwa na vijana."Vita daima ni kushindwa na tusisahau hilo."

Na Angella Rwezaula, - Vatican.

Mara baada ya tafakari ya Katekesi ya Papa Francisko, Jumatano tarehe 8 Novemba 2023, ametoa mwaliko wake tena, wakati akisalimia waamini kwa lugha ya kitaaliano baada ya tafakari yake iliyojikita katika sura ya Madeleine Delbrêl, Mfaransa mtafakari fumbo, mfanyakazi wa kijamii, mwandishi wa insha na mshairi na kusema kuwa, Tufikiri na kuwaombea watu wanaoteseka na vita. Tusiisahau Ukraine iliyoteswa na kuwafikiria Wapalestina na Waisrael: Mungu atuongoze kwenye amani ya haki. Tunateseka sana: watoto wanateseka, wagonjwa, wazee wanateseka na vijana wengi wanakufa. Vita daima ni kushindwa: tusisahau hili. Daima ni kushindwa.

Waamini mbali mbali waliofika katika katekesi
Waamini mbali mbali waliofika katika katekesi

Papa Francisko akiendelea amesema anavyowakaribisha kwa moyo mkunjufu mahujaji wanaozungumza Kiitaliano, hasa kwa wamini wa Altamura, Mtakatifu Salvatore Telesino na Petronà. Amewakaribisha  kikundi cha kujitolea cha  Unitalsi cha Emilia-Romagna, kikundi kutoka Hospitali kuu ya Milano na  Sanaa ya Muziki Mtakatifu kwa upendo maalum. Na kama kawaidia amewasalimia vijana, wazee, wagonjwa na wanandoa wapya .

Papa akisalimiana na makundi yaliyofika katika katekesi
Papa akisalimiana na makundi yaliyofika katika katekesi

Baba Mtakatifu Francisko amekumbusha  hata hivyo litutujia ya Kanisa kuhusu Kutabaruku Basilika ya Mtakatifu Yohane , Laterano ambayo hufanyika kila ifikapo tarehe 9 Novemba ya kila mwaka na ambalo ni  Kanisa kuu la Roma, Kanisa kuu la Papa, kama askofu wa Roma. Kwa hiyo Papa ameongeza kusema kuwa  Tukio hili na liamshe kwa kila mtu hamu ya kuwa mawe yaliyo hai katika utumishi wa Bwana.

Makundi ya mahujaji wakisalimia Papa
Makundi ya mahujaji wakisalimia Papa

Baba Mtakatifu akiendelea katika salamu zake kwa lugha mbali mbali zaidi ya hayo, baraza ziliwaendea wanaozungumza Kiarabu, ambapo Papa ameomba ulinzi dhidi ya uovu wote na amemwomba Bwana Yesu hasa kwa zawadi ya Ujasiri wa kufanya kazi pamoja na wale wote wanaofanya kazi duniani ili kuikomboa dunia dhidi ya uovu na kuirudisha kwenye wema wake wa awali.

Papa katika katekesi
Papa katika katekesi

Papa Francisko akiwageukia  kati ya vikundi vingine vya mahujaji, wanaozungumza Kifaransa, aliwasalimia washiriki wa Jumuiya ya Kitaifa ya Jumuiya za Familia za Kikatoliki. Kisha aliongeza kutoa mwaliko kuwa: Tukiwa tunakabiliana na ulimwengu wetu wa kiulimwengu, tusilalamike, bali tuone ndani yake wito wa kuthibitisha imani yetu na mwaliko wa kuwasilisha furaha ya Injili kwa wale wote wenye kiu ya Mungu. Tumwombe Bwana neema ya kushuhudia kwa imani yetu kila siku na udugu na urafiki wa uzoefu na kila mmoja.

Hatimaye, Mrithi wa Petro hakukosa kutaja, katika salamu zake kwa mahujaji wa Kipoland, kumbukumbu ya karibu ya kurudiwa kwa uhuru wa Poland, ambayo itaadhimishwa tarehe 11 Novemba. Baba Mtakatifu amesema Sikukuu hii inawahimiza kuwa na shukrani kwa Mungu, na kuongeza kusema hasa kwa: kurithisha historia yao kwa vizazi vipya.

Wito wa Papa 8 Novemba 2023 baada ya katekesi
08 November 2023, 13:24