Tafuta

2023.11.07 Papa alitoa sakramenti ya Ubatizo kwa mtoto wa familia moja ya Ukraine. 2023.11.07 Papa alitoa sakramenti ya Ubatizo kwa mtoto wa familia moja ya Ukraine. 

Papa Francisko abatiza mtoto wa Kiukreni huko Mtakatifu Marta

Jina lake ni Zakhariy mwenye umri wa miezi mitatu,mtoto wa mwisho kati ya watoto kumi wa wanandoa wa Kiukraine.Ibada hiyo ya Sakramenti ya ubatizo ilifanyika Jumatatu tarehe 6 Novemba 2023 katika kikanisa cha Myumba ya Mtakatifu Marta mjini Vatican.

Vatican News

Ulikuwa ni wakati wa furaha kubwa katika kipindi kigumu kweli. Hivi ndivyo wazazi vijana wa Kiukraine wa Zakhariy, mtoto wa miezi mitatu aliyebatizwa na Papa Francisko katika kikanisa  cha Nyumba ya Mtakatifu Marta alasiri ya Jumatatu tarehe 6 Novemba 2023 walibainisha. Jina la kijana baba wa mtoto ni Vitaly, mwenye umri wa miaka 37, na jina lake mama wa  mtoto ni Vita, mwenye umri wa miaka 35, na mtoto mdogo ni wa mwisho kati ya watoto kumi, wavulana saba na wasichana watatu. Wanaishi Kamianets-Podilskyi, magharibi mwa Ukraine, katika eneo lililo salama kutokana na vita vilivyoanzishwa na Urussi  tangu mwezi Februari 2022.  Wazazi hawa wako kwenye harakati ya Waneokatekumenali na katika miaka ya hivi karibuni wamepata uzoefu mkubwa wa utunzaji  katikati ya shida nyingi za kifamilia, zilizozidishwa zaidi baada ya uvamizi wa Urusi.

“Tunakabili kila jambo kwa shukrani kwa Mungu, kwa sababu sikuzote Mungu huitunza familia yetu,” alisema mama wa mtoto mdogo: “Kuna vita nchini” na “ni vigumu sana. Kila mtu anasali kwamba vita hivi viishe hivi karibuni, kwamba wafungwa wote warudi nyumbani na kwamba hakutakuwa na mauaji tena. Kwa ubapande wa tukio hlo wamesema Ubatizo wa tarehe 6 Novemba  ulikuwa zawadi kubwa kwa familia yao na kwamba  "Sikuweza hata kuota kwamba tungeweza kuwa na Baba Mtakatifu na kwamba angeweza kumbatiza mtoto wetu. Lakini Mungu anafanya historia na sisi ya ajabu sana, ambayo bado hatuelewi kikamilifu."

Pia alikuwepo katika ibada hiyo Monsinyo Leon Dubrawski, Askofu wa Kamianets-Podilskyi ya Walatini, ambaye alikumbuka jinsi upendo wa Mungu unavyopitishwa kutoka kizazi hadi kizazi kupitia familia. Alikuwa askofu aliyewasindikiza  wanandoa hao vijana hadi mjini Vatican. Papa Fransisko anaendelea kuukumbusha ulimwengu  juu ya janga la watu wa Kiukreni walioteswa": Ubatizo wa Zakhariy mdogo ni tumaini jipya kwa familia hii changa na kubwa ambayo haiwezi kusahau vita lakini inaendelea kuwa na imani katika siku zijazo za amani.

Papa alitoa ubatizo kwa mtoto wa miezi 3 wa kumi kati ya ndugu zake
08 November 2023, 16:39