Tafuta

Watu wakiwa wanatembea kwenye mahofu mara baada ya kimbunga na mvua kali huko Derna nchini Libya. Watu wakiwa wanatembea kwenye mahofu mara baada ya kimbunga na mvua kali huko Derna nchini Libya. 

Papa atoa wito kwa ajili ya Nchi ya Libya na Morocco katika mikasa

Papa Francisko akisalimia waamini wa lugha ya kiitaliano mara baada ya katekesi yake Jumatano Septemba 13,ametoa wito kwa ajili ya watu wa Libya waliokumbwa na maporomoko kutokana na mvua kali na kuuwa watu wengi,majeruhi na uharibifu.Amewaombea hata watu wa Morocco kwa tetemeko la ardhi.

Na Angella Rwezaula, - Vatican.

Mara baada ya Katekesi, kwa waamini na mahujaji waliunganika katika Uwanja wa Mtakatifu Petro mjini Vatican, Baba Mtakatifu Francisko, Jumatano tarehe 13 Septemba 2023, mawazo yake yamewaendea watu wa nchini Libya ambao wamekumbwa na mvua ya nguvu, ambayo ilisababisha mafuriko makubwa hadi  kusababisha kujaa kwa mabwawa mawili kwa wakati mmoja ambayo yaliporomoka na kuua watu wengi na majeruhi ikiwa ni pamoja na madhara makubwa ya miundo mbinu nchini humo. Kwa njia hiyo Baba Mtakatifu amesema: “Ninawaalika kuungana na sala yangu kwa ajili ya wale walipoteza maisha, kwa ajili ya familia zao na kwa wale waliorundikana. Wasikose mshikamano wetu  wa kuelekeza kwa kaka na dada waliojaribiwa namna hiyo na mkasa huu”.

Tetemeko la Morocco

Baba Mtakatifu Francisko akiendelea aidha mawazo yake pia yamewageukia watu watukufu wa Morocco "ambao wameteseka kutokana na mtikisiko wa ardhi, wa matetemeko haya. Tusali kwa ajili ya Morocco, tusali kwa ajili ya wakazi. Na Bwana awapatie nguvu za kuanza tena; ya kuanza tena baada ya janga hili lisilosemakana ambalo limepita.” Papa amekazia

Pyaisheni mwamko wa huduma ya Injili

Baba Mtakatifu vile vile amewaelekea na kuwakaribisha mahujaji wa lugha ya kitaaliano kwa namna ya pekee Watawa wa Shirika la Watumishi wa Masikini, huku akiwatakia wawe na Mkutano Mkuu mwema na kupyaisha mwamko wa kitume katika huduma ya Injili.

Manajeshi kutiwa moyo kwa huduma ya ndugu

Furaha ya Baba Mtakatifu pia ni kuwakaribisha kikundi cha AVIS ambacho ni chama cha Italia cha kutoa damu cha Vallecorsa, Kikundi cha kujitolea Love Bridges, Wanajeshi wa Motta ya Lavenza na wa Portogruaro ambapo amewatia moyo kila mmoja wa kikundi hicho katika shughuli ya huduma kwa ndugu.

Hatimaye kama kawaida yake, mawazo yake ni kwa vijana, wagonjwa, wazee na wenye ndoa wapya. Baba Mtakatifu Francisko amependa kukumbusha kila tarehe 14 Septemba ya kila mwaka, ambapo Mama Kanisa anaadhimisha sikukuu ya Kutukuka kwa Msalaba Mtakatifu. Kwa hiyo amesema: “Tusichoke kuwa waaminifu wa Msalaba wa Kristo, Ishara ya upendo na wa Wokovu. Na kwa wote amewabariki.

Baada ya katekesi 13 Septemba 2023
13 September 2023, 10:12