Tafuta

2023.09.12 Kanisa Kuu la Marsiglia litakalomwona Papa Francisko katika ziara yake 22-23 Septemba 2023 katika Mkutano wa bahari yetu ya Mediterrane 2023.09.12 Kanisa Kuu la Marsiglia litakalomwona Papa Francisko katika ziara yake 22-23 Septemba 2023 katika Mkutano wa bahari yetu ya Mediterrane  (Jacques Vanni )

Papa atafanya ziara huko Marsiglia kuanzia 22-23 Septemba 2023

Papa atakwenda Marsiglia,Ufaransa kushiriki hitimisho la Mkutano wa 'Rencontres Méditerranéennes' na kwamba ni mpango mzuri ambao unajitokeza katika miji muhimu ya Mediterania,ikiwaleta pamoja viongozi wa kikanisa na kiraia ili kukuza njia za amani,ushirikiano na mshikamano kuzunguka Bahari yetu kwa kuzingatia jambo la uhamiaji.

Na Angella Rwezaula,- Vatican.

Baba Mtakatifu Dominika tarehe 17 Septemba 2023, mara baada ya tafakari na sala ya Malaika wa  Bwana, akiwageukia waamini na mahujaji waliofika katika Uwanja wa Mtakatifu Petro mjini Vatican, amewaeleza jinsi ambavyo Ijumaa tarehe 22 Septemba 2023, atakwenda huko Marsiglia nchini ufaransa kwa ajili ya kushiriki hitimisho la Mkutano wa  Rencontres Méditerranéennes, yaani Mikutano ya Mediterania, na kwamba ni mpango mzuri ambao  unajitokeza katika miji muhimu ya Mediterania, ikiwaleta pamoja viongozi wa kikanisa na kiraia ili kukuza njia za amani, ushirikiano na mshikamano kuzunguka 'Nostrum mare', yaani 'Bahari yetu' kwa kuzingatia kwa namna ya pekee jambo la uhamiaji.  

Mji wa Marsiglia
Mji wa Marsiglia

Hii inawakilisha changamoto ambayo si rahisi, kama tunavyoona kutoka katika habari za siku za hivi karibuni, lakini ambayo lazima ikabiliwe kwa pamoja, kwani ni muhimu katika maisha ya baadaye ya kila mtu, ambayo yatakuwa na mafanikio ikiwa yatajengwa juu ya udugu, na kuweka hadhi na utu wa  binadamu, watu thabiti hasa wale wanaohitaji zaidi.  Baba Mtakatifu Francisko kwa kuongezea amesema kwamba: “Wakati ninawaomba mnisindikize  na safari hii kwa maombi, ningependa kuwashukuru viongozi wa serikali na wa kidini, na wale wanaofanya kazi ya kuandaa mkutano huko Marseille, jiji lenye watu wengi, linaloitwa kuwa bandari ya matumaini. Kuanzia sasa na kuendelea ninawasalimu wakazi wote, nikingoja kukutana na  kaka na dada wengi wapendwa.”

Mamia elfu ya waamini na mahujaji katika Uwana wa Mtakatifu Petro katika sala ya Malaika wa Bwana
Mamia elfu ya waamini na mahujaji katika Uwana wa Mtakatifu Petro katika sala ya Malaika wa Bwana

Amewasalimu wote, Warumi na mahujaji kutoka Italia na nchi mbalimbali, hasa wawakilishi wa baadhi ya parokia za Miami, Banda la Gaitas ya Batallon de San Patricio, waamini wa Pieve ya Cairo na Castelnuovo Scrivia, Masista Wamisionari. wa Mkombozi Mtakatifu wa Kanisa Katoliki la Kigiriki la Kiukraine.  

Papa ameomba kuwakumbua watu wa Ukraine wanaoteseika na vita na sehemu nyingine duniani
Papa ameomba kuwakumbua watu wa Ukraine wanaoteseika na vita na sehemu nyingine duniani

Lakini pia Papa akuhasahu kwamba “Na tunaendelea kuwaombea watu wa Kiukraine wanaoteswa na amani katika kila nchi iliyomwaga damu  na vita. Na amewasalimu Vijana wa Moy safi wa maria . Amehitimisha kwa kuwatakia  Dominika  njema na tafadhali wasisahau kumuombea. Mlo mwema, mchana mwema na kwaheri ya kuonana.

Papa ameelza safari yake ya Marsiglia Ijumaa 22-23 Septemba 2023
17 September 2023, 12:39