Tafuta

2023.06.05 Papa amekutana na washiriki wa Tamasha la Kijani na Blu katika Siku ya Kimataifa ya Mazingira: "Sayari kwa wote" 2023.06.05 Papa amekutana na washiriki wa Tamasha la Kijani na Blu katika Siku ya Kimataifa ya Mazingira: "Sayari kwa wote"  (Vatican Media)

Papa Francisko:tusiibie vizazi bali kuwapa tumaini la maisha bora ya baadaye!

Katika fursa ya maadhimisho ya Siku ya Mazingira Duniani,'Syari kwa wote',Papa amekutana na wahamasishaji wa Tamasha la Kijani na Bluu:mabadiliko ya tabianchi yanatuita kwenye majukumu yetu na huathiri zaidi ya maskini wote,ni suala la haki badala ya mshikamano.Kuna haja ya kuwajibika mbele Mungu na ushirikiano wa kila mtu ili kukabiliana na tabianchi.

Na Angella Rwezaula, - Vatican.

Changamoto kubwa na inayodai jitihada kubwa kwa sababu inahitaji kubadili dira, maamuzi stahiki ya mabadiliko katika mtindo wa sasa wa matumizi na uzalishaji ambao mara nyingi hushiriki katika utamaduni wa kutojali na uharibifu wa mazingira na watu. Hata hivyo changamoto  hiyo ni fursa ya kusisimua na inayoweza kufikiwa, kwa sababu inakuwezesha kuhama kutoka katika utamaduni huo hadi katika  maisha kulingana na heshima na huduma kwa kazi ya  uumbaji na jirani. Haya ndiyo ambayo Baba Mtakatifu Francisko amezindua, Jumatatu tarehe 5 Juni 2023 alipokutana na Wahamasishaji wa  Tamasha la Kijani na Bluu, lililoandaliwa mjini Roma, tarehe 5 Juni na kuanzia tarehe 6 hadi 8 Juni litafanyika huko  Milano Italia ambalo ni mpango  wa uchapishaji wa kikundi cha Kiitaliano kiitwacho Gedi kinachojitolea kwa ajili ya uendelevu na mazingira.

Wahamasishaji wa Kijani na Blu katika siku ya mazingira duniani
Wahamasishaji wa Kijani na Blu katika siku ya mazingira duniani

Kwa njia hiyo ilikuwa ni fursa ya kupendekeza utamaduni wa malezi na jinsi watoto wanavyotunzwa, ambayo inaweka hadhi ya  binadamu na manufaa ya wote katika kitovu hicho cha  Siku ya Mazingira Duniani kote ambayo uhadhimishwa kika  tarehe 5  Juni katika kumbukumbu siku hiyo iliponzishwa mnamo mwaka 1972 ya Mkutano wa kwanza wa Umoja wa Mataifa kuhusu Mazingira ya Binadamu huko Stockholm, Sweden. Katika miaka hii hamsini,  Papa Francisko  amebainisha, juu ya ufahamu wa masuala haya kuwa  “umeongezeka na ujuzi wetu wa athari za matendo yetu kwa nyumba yetu ya pamoja  na kwa wale wanaoishi ndani yake na watakaokaa ndani umepanuka, pia kuongezea hisia zetu za uwajibikaji kwa Mungu, ambaye ametukabidhi utunzanji wa kazi ya  uumbaji, mbele ya jirani zetu na mbele ya vizazi vijavyo.”

Kwa mujibu wa Baba Mtakatifu hasa amekumbuka kwamba alitaka kuchapisha waraka wa Laudato si' kabla ya  COP 25 huko Paris kuhusu hali ya tabianchi na anasikitika kwamba tukio hilo chanya halikufuatwa na wengine wa kiwango sawa. Imethibitishwa, kwani  Papa amesisitiza, huku  akinukuu ripoti ya Jopo la Serikali Mbalimbali la Mabadiliko ya Tabianchi (IPCC) kuhusu tabianchi , kwamba chaguo na hatua zinazotekelezwa katika muongo huu zitakuwa na athari kwa maelfu ya miaka, hasa kuhusu athari kwenye sayari. Hali ya mabadiliko ya tabianchi  inatukumbusha kwa uthabiti wajibu wetu na inawagusa watu maskini zaidi na walio dhaifu zaidi, wale ambao wamechangia kidogo sana  katika mabadiliko yake. Na hivyo awali ya yote ni suala la haki na baadaye mshikamano amesisitiza.

Siku ya Kimataifa ya Mazingira 5 Juni ya kila mwaka
Siku ya Kimataifa ya Mazingira 5 Juni ya kila mwaka

Hii inamaanisha kuegemeza hatua yetu kwenye ushirikiano unaowajibika kwa upande wa wote. Kama janga la Uviko-19 limeonesha, ulimwengu wetu sasa unategemeana sana na hauwezi kumudu kugawanywa katika vikundi vya nchi zinazoendeleza masilahi yao kwa njia ya pekee au isiyo endelevu. Tabia ya kutowajibika kiukweli ni adui halisi na ina athari kwa ubinadamu wetu leo ​​na kesho. Kuhusiana na hilo, Papa Francisko alikumbuka mkutano wake na wavuvi wa Mtakatifu Benedetto wa Tronto, Italia ambao badala ya kurudisha samaki wa siku hiyo kwenye boti zao, walirudi na tani za plastiki, wakipoteza mapato yao ya uvuvi, lakini waliboresha mazingira.

Mabadiliko, amesisitiza, ni ya dharura na hayawezi kuahirishwa tena. Kwa maana hiyo, alikumbuka jinsi hivi karibuni alikutana na watendaji wa migahawa ya chakula cha haraka ya McDonald, ambayo imebadilisha kutoka plastiki kwa ajili ya ufungaji hadi karatasi iliyosindikwa, na jinsi Vatican pia imepiga marufuku plastiki, iliyopunguzwa kwa asilimia  93%. Hatua madhubuti za kuhakikisha kwamba wale waliozaliwa  katika miaka 30 hawaishi katika ulimwengu usio na makazi. Papa amesisitiza kwamba “Tusiibe vizazi vipya"” bali kuwapa  tumaini la maisha bora ya baadaye.

Papa amakutana na wahamasishaji wa kijani na blu katika siku ya kimataifa ya mazingira
05 June 2023, 16:29