Tafuta

2023.05.10 Papa amkutana na washiriki wa Mkutano ulioahamaisha na Taasisi ya Kipapa ya sayansi kuhusu:Chakula na migogoro ya kibinadamu:sayansi na sera za kuzuia na kupunguza”. 2023.05.10 Papa amkutana na washiriki wa Mkutano ulioahamaisha na Taasisi ya Kipapa ya sayansi kuhusu:Chakula na migogoro ya kibinadamu:sayansi na sera za kuzuia na kupunguza”.  (Vatican Media)

Papa:vita na taabu ni sababu za kupungua kwa udugu wa kibinadamu

Papa akikutana na washiriki wa mkutano kuhusu chakula na majanga ya kibinadamu unaoendelea mjini Vatican amezungumzia udharura wa kupunguza mateso kwa wale wanaoteseka na njaa.Mawazo yake pia Ukraine:“Mara nyingi hali zinazoambatana na majanga ya asili pia kuna migogoro ya kivita,ufisadi wa kisiasa au kiuchumi na unyonyaji wa ardhi,vinavyotishia usambazaji wa chakula kwa watu wote”.

Na Angella Rwezaula, - Vatican

Baba Mtakatifu Franciko, Jumatano tarehe 10 Mei 2023, amekutana na washiriki wa Mkutano wa Chuo cha Kipapa cha Sayansi kuhusu “Chakula na migogoro ya kibinadamu:sayansi na sera za kuzuia na kupunguza”, ambapo katika hotuba yake amewakaribisha wote kwa moyo mkunjufu katika fursa ya mkutano hu ona kumshukuru  Rais wa Chuo hicho von Braun kwa salamu zake  za utangulizi kwa niaba ya wote. Papa amesema kwamba mada waliyochagua ni ya wakati muafaka kuliko wakati mwingine wowote, si kwa ajili ya mjadala wa kitaaluma tu, bali pia kwa sababu inavutia mamlaka zinazoona mbali na mazoea ya kisiasa, ili kupunguza mateso ya kaka na dada zetu wengi wanaokosa lishe bora na upatikanaji wa chakula cha kutosha. Papa amekumbusha tena kwamba “Msomi mmoja aliniambia miezi michache iliyopita: kuwa ‘Kama silaha hazingetengenezwa kwa mwaka, njaa ya ulimwengu ingeisha.’

Kundi la washiriki wa Mkutano ulioandaliwa na Taasisi ya Kipapa ya Sayansi.
Kundi la washiriki wa Mkutano ulioandaliwa na Taasisi ya Kipapa ya Sayansi.

Hii ni changamoto ya dharura, kwa sababu mara nyingi hali zinazooneshwa na majanga ya asili, lakini pia  kuna  migogoro ya silaha ambapo Papa mawazo yake amefikiria  hasa vita vya Ukraine, ufisadi wa  kisiasa au kiuchumi na unyonyaji wa ardhi, nyumba yetu ya kawaida ya pamoja, huzuia uzalishaji wa chakula, kudhoofisha mifumo ya kilimo na kutishia usambazaji wa lishe kwa watu wote. Wakati huo huo, migogoro hii mbalimbali imezidishwa na athari za muda mrefu za janga la Uviko-19, huku pia tunashuhudia kupungua kwa mshikamano wa kidugu  huu ni ukweli ambapo  vita na mikasa hiyo husababisha kupungua kwa mshikamano wa kidugu  na kushuka huku kumedhamiriwa, miongoni mwa mambo mengine, na madai ya ubinafsi yaliyo katika baadhi ya mifano ya sasa ya kiuchumi, Papa amekazia.

Papa anasisitiza  juhudi za umoja ili kutafuta suluhisho la njaa
Papa anasisitiza juhudi za umoja ili kutafuta suluhisho la njaa

Katika mtazamo huo, ni muhimu kufahamu zaidi kwamba kila kitu kinahusiana kwa karibu kwa hiyo “matatizo ya leo yanahitaji maono yenye uwezo wa kuzingatia kila kipengele cha mgogoro wa kimataifa”(Fratelli tutti, 137). Kipengele muhimu cha maono haya ni kuelewa kwamba mgogoro unaweza pia kuwa fursa, tukio la kupendeza la kutambua na kujifunza kutokana na makosa ya zamani. Kwa maana hiyo, nimatumaini kuwa Mkutano wao utatusaidia sote kuibuka vyema zaidi kutoka katika machafuko tunayopitia, sio tu kwa kuzingatia suluhisho za kiufundi, lakini zaidi ya yote kwa kukumbuka jinsi ilivyo muhimu kukuza mtazamo wa mshikamano wa ulimwengu wote unaozingatia udugu, upendo na kuelewana.

Kwa maana hiyo, Kanisa linaunga mkono kwa moyo wote na kuhimiza juhudi zenu, pamoja na wale wote wanaofanya kazi si tu kulisha wengine au kukabiliana na majanga, lakini pia kukuza maendeleo shirikishi ya binadamu, haki kati ya watu na mshikamano wa kimataifa, hivyo kuimarisha umoja. nzuri ya jamii. Kwa hiyo, kwa mara nyingine tena  Papa ametoa shukrani zake za dhati kwa huduma yao adhimu kwa kushirikiana na Chuo cha Kipapa cha Sayansi na anawahakikishia sala zake, kwamba kazi yao itazaa matunda katika kusaidia kutatua matatizo mengi yatokanayo na majanga ya chakula na masuala mengine ya kibinadamu migogoro.

Mzozo ni tofauti na migogoro

Migogoro imefungwa ndani yake yenyewe, ni ngumu kutoka katika mzozo kwa njia ya kujenga. Badala yake, tunaweza kutoka kwenye mizozo, lna azima tutoke, lakini kwa masharti mawili kwamba: “hatuwezi kutoka kwenye shida peke yetu, ama tutoke pamoja au hatuwezi kutoka. Hili ni muhimu, huwezi kutoka peke yako, unahitaji jumuiya, kikundi kutoka nje. Na, kwa upande mwingine, unaibuka kutoka katika shida ili kuboresha, daima kusonga mbele, na maendeleo. Kwa hilo Papa amewashukuru kwa mtazamo wao katika uso wa shida hiyo, kutoka pamoja na kwenda nje vizuri zaidi. Kwa upande wake ameomba baraka tele za Mwenyezi Mungu juu yao na kuwaomba tafadhali wamwombee.

Hotuba ya Papa kwa washiriki wa mkutano wa Taasisi ya Kipapa ya Sayansi
10 May 2023, 16:30