Tafuta

Bahari ziunganishe na zisiwe mahali pa misiba . Bahari ziunganishe na zisiwe mahali pa misiba .  (ANSA)

Papa Francisko:bahari ziunganishe watu na sio mahali pa vifo

Katika ujumbe uliotiwa saini na Kardinali Parolin katibu wa Vatican katika fursa ya mkutano kuhusu Bahari Yetu,uliohitimishwa hivi karibuni katika Jiji la Panama,Papa Francisko anasisitiza umuhimu wa bahari kama chanzo cha miunganisho ambayo wanadamu wote wanategemea.Ni vema kupitisha maono na maendeleo fungamani ya ikolojia.

Na Angella Rwezaula – Vatican.

Bahari inaweza kuwa jambo muhimu la muungano, miunganisho ya uhusiano, na sababu ya kawaida ya pamoja. Ili kupata muunganisho huo, ni muhimu kusikiliza kilio cha maskini na kilio cha Dunia na kupitia mikakati ya ukuaji kulingana na upotevu na matumizi, juu ya mifano isiyo ya haki na isiyo endelevu ya uzalishaji, usafiri, usambazaji na matumizi. Hayo yamebainishwa na Baba Mtakatifu Francisko katika ujumbe uliotiwa saini na Kardinali Pietro Parolin, Katibu wa Vatican uliotumwa kwa washiriki wa mkutano wa nane wa Mkutano wa Bahari Yetu uliofanyika katika Jiji la Panama kuanzia tarehe 2 hadi 3 Machi 2023 ambao mwaka huu umeongozwa na kauli mbiu “Bahari Yetu, uhusiano wetu”.

Uhusika kuanzia chini hadi ngazi ya kimataifa

Katika ujumbe huo unasisitiza mambo mengine mawili msingi kwamba ili kuweza kuishi uhusiano huu na ukweli wote unaohusika, kuanzia na tawala hadi sekta binafsi, kutoka katika ulimwengu wa utafiti hadi wale wa siasa na utamaduni, kuanzia mashirika ya kidini na vijana hadi jumuiya ya kimataifa. Mojawapo ya hoja hizi inawakilishwa na hitaji la kuungana ili kulinda na kurejesha mifumo ya ikolojia ya baharini, pwani na mito, nyingine inaoneshwa na umuhimu wa kuwezesha utawala bora na uratibu wa kitaasisi unaoendana na ukubwa na ugumu wa manufaa ya kulinda, bahari.

Maono fungamani ya maendeleo ya ikolojia

Ujumbe huo unakumbusha jinsi wanadamu wote wanavyotegemea bahari, walizopokea kama zawadi kutoka kwa Muumbaji, na jinsi matumizi yao yanatarajiwa kuwa ya haki na endelevu ili kupitishwa kwa vizazi vijavyo katika hali nzuri. Kwa hiyo familia nzima ya binadamu inaitwa, kama inavyooneshwa na  Waraka wa Laudato si', kuchukua maono fungamani ya  maendeleo na maono fungamani  ya ikolojia. Kwa bahati mbaya Baba Mtakatifu amebainisha , hata hivyo, matukio ya kutisha ya uchafuzi wa bahari, tindikali, uvuvi haramu na uvuvi wa kupindukia bado upo, pamoja na wasiwasi mkubwa wa maendeleo ya sekta ya uchimbaji kwenye bahari, na kwa mikasa ya wahamiaji katika dhiki kwenye bahari kuu, usafirishaji haramu wa binadamu unaofanyika baharini

Mazingira magumu ya kazi ya mabaharia

Kama hiyo haitoshi pia kuna, mazingira magumu na wakati mwingine haramu ya kazi ya mabaharia na mivutano ya kijiografia katika maeneo ya bahari inachukuliwa kuwa muhimu. Maji, ni elekezo,  ni muktadha wa uhusiano na bahari haina mipaka ya kisiasa au kiutamaduni, kwa kuwa ni mikondo yake, inayovuka sayari, ambayo itoa nuru ya muunganisho na kutegemeana kati ya jamii na nchi.  Baba Mtakatifu amesema “Sisi ni familia moja  kwa hivyo tuna shiriki hadhi sawa  ya  kibinadamu usioweza kuondolewa, tunaishi katika nyumba ya pamoja ambayo tumeitwa kuitunza.

Ujumbe wa Papa kwa Mkutano kuhusu bahari yetu, huko Panama 2/3 Machi 2023
06 March 2023, 16:49