Tafuta

2023.01.31  Papa Francisko akizungumza na waandishi wa habari wakati wa safari kuelekea DRC ,barani Afrika 2023.01.31 Papa Francisko akizungumza na waandishi wa habari wakati wa safari kuelekea DRC ,barani Afrika 

Papa katika ndege,wamesali kwa ajili ya wale waliokufa wakivuka Sahara

Katika salamu zake za kiutamaduni kwa waandishi wa habari wakati wa safari ya kuelekea Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo, Francisko mawazo yake yaliwaendea wengi waliopoteza maisha na wale waliowekwa katika kambi za mateso baada ya kuvuka jangwa.

Na Angella Rwezaula – Vatican

Ukimya na sala kama ule wa kutaka kubembeleza maisha ya mateso na watu waliokata tamaa wakati wakitafuta fursa mpya. Papa Francisko alisema alirudia kuonesha uchungu na huruma wakati akizungumza na  waandishi wa habari Jumanne tarehe 31 Januari 2023 asubuhi  katika safari ya ndege ya kutoka Roma kwenda Kinshasa, katika Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo, kituo cha kwanza katika ziara yake ya 40 ya kitume ambayo pia itampeleka nchini Sudan Kusini. Akizama Chini rangi za jangwa na jua, hakusahau kuwa na  kumbukumbu ya maisha  watu wengi waliozikwa ndani ya mchanga huo au kutombea kwa uzito na uchovu, kiu na vurugu.

Papa akiwasalimia waandishi wa habari
Papa akiwasalimia waandishi wa habari

Papa amesema kwa wakati huu tukiwa tunavuka Sahara tufikirie, kwa ukimya, maombi  kwa watu wote ambao, katika harakati za kutafuta ustawi kidogo, uhuru kidogo, wamevuka na hawajafanikiwa. Wagonjwa wengi wanaofika Mediterania baada ya kuvuka jangwa na kuwekwa katika kambi za mateso na kuteseka huko. Tuwaombee watu hao wote.

Papa ameondoa  kwa hija ya amani nchini Congo na Sudan Kusini

Kabla ya maombi hayo ya kimya na mazito hata hivyo Papa Francisko kama kawaida yake  aliwahutubia waandishi wa habari waliokuwepo,  takriban 75 kutoka nchi 12, wawili kati yao wakiwa Waafrika na kuwashukuru kwa kuandamana naye katika safari hiyo iliyokuwa inasubiriwa kwa mwaka mmoja. Papa akiendelea amesema “Ni safari nzuri, ningetamani kwenda Goma, lakini kwa sababu ya vita huwezi kwenda huko. Itakuwa Kinshasa na Juba tu, tukiwa huko tutafanya kila kitu. Asante kwa kuwa hapa pamoja nami tukiwa wote, asante kwa kazi yenu nzuri sana inasaidia sana maana inawapatia watu wanaopenda picha za safari, mawazo, tafakari yenu  ya safari, asante sana”, alisema Papa. 

Mwandishi wa habari akimkabidhi zawadi na kumuelezea maana yake
Mwandishi wa habari akimkabidhi zawadi na kumuelezea maana yake

Aidha Papa Francisko ameelezea masikitiko yake kwa kutofanya mzunguko wa kawaida wa kusalimiana nao hivyo amesema: “Lakini leo siwezi”, kwa hiyo Papa Francisko alibaki kwenye kiti chake na kusema “ninahisi aibu kidogo kuona kila mtu anakuja hapa, hivyo tunaweza kusalimiana kwa mbali”. Papaakipokea zawadi mbalimbali kutoka kwa waliomsindikiza katika safari hiyo, mwandishi wa habari Eva Fernandez wa Radio Cope, mtangazaji wa Baraza la Maaskofu wa Hispania, alitoa kipande cha mwamba wa Kiwu ambao wanachomoa coltan na kumweleza Papa Francisko kwamba kwa kila kilo kilo moja. Watu wawili wanakufa. Kisha kipande cha lava kutoka kwenye volkano ya Nyiragongo, karibu kilomita 12 kaskazini mwa jiji la Goma, ambalo husababisha mikasa.

Salamu za Papa kwa waandishi katika ndege
31 January 2023, 15:58