Tafuta

Papa Francisko wakati wa sala ya Malkia wa Mbingu Papa Francisko wakati wa sala ya Malkia wa Mbingu 

Papa Francisko:Hatuwezi kuwa wakristo wema ikiwa hatubaki na Yesu

Hatuwezi kuwa wakristo wema ikiwa hatukai na Kristo.Bwana anahitaji ushuhuda wa misha yetu ya Kikristo.Baada ya Kristo kupaa Mbinguni kazi yetu kama wafuasi wa Kristo ni kupelekea matunda ya upendo.Kuzaa matunda yanategemea sala ili kuwasaidia maskini kama alivyofanya Bwana.Ni tafakari ya Papa katika Dominika ya V ya Pasaka kwa kuongoza kwa Injili ya siku.

Na Sr. Angela Rwezaula -Vatican.

Kabla ya sala ya Malkia wa Mbingu Dominika ya V ya Pasaka, tarehe 2 Mei 2021, Papa Francisko akiwa katika dirisha akiwageukia waamini na mahuji waliofika katika uwanja wa Mtakatifu Petro ametafakari Injili ya Siku. Papa Francisko amesema: Katika Injili ya Dominika ya V ya Pasaka, (Yh 15,1-8) Bwana anajionesha kuwa mzabibu wa kweli na anazungumza kuwa sisi ni matawi ambayo hayawezi kuishi bila kubaki yameungana na Yeye. Bwana amesema hivi: “Mimi ndimi mzabibu wa kweli na ninyi ni Matawi (Yh 15,5). Hakuna maisha bila matawi kwa maana yote yanategemeana. Matawi hayana nguvu kwa sababu yanategemea moja kwa moja kutoka mzabibu ambao ni chanzo  cha kudumu kwake.

Bila kiini hakuna maisha:Mti na matawi vinahitajiana

Yesu anasisitiza neno la kukaa. Amerudia neno hilo mara saba katika kifungu cha Injili ya siku. Kabla ya kuacha ulimwengu huu na kwenda kwa Baba, Yesu anataka kuwahakikishia mitume wake ambao wanaweza kuendelea na muungano na Yeye. “kaeni ndani yangu nami ndani yenu ( Yhn 15, 4). Kukaa maana yake si kukaa bila kazi, kwa kulala ndani mwa Bwana, kuacha umbembelezwe na maisha. Hapana, siyo hivyo. Kubaki katika Yesu ambako Yesu anapendekeza kwetu, ni kubaki na uhai na kwa umoja. Kwa nini? Ni kwa sababu bila mzabibu hakuna maisha, haiwezekani kufanya lolote, kwa sababu kunahitaji kiini ili kukua na kuzaa matunda; lakini vilevile hata maisha yanahitaji mzabibu kwa sababu bila matunda kisiki cha mti hakiwezi kuwapo. Ni kuhitajiana, ni kubaki na muungano ili kutoa matunda. Ni kubaki katika Yesu na Yeye ndani mwetu. Awali ya yote sisi tunamwitaji Yeye. Bwana anataka kutwambia kuwa kabla ya kutimiza amri zake, kabla ya heri, kabla ya matendo ya huruma ni lazima kuungana na yeye, na kubaki na Yeye. Hatuwezi kuwa wakristo wema ikiwa hatubaki na Yesu. Na katika yeye tunaweza yote (Fil 4,13). Pamoja na Yeye tunaweza kufafanya kila kitu.

Yesu anahitaji ushuhuda wetu wa maisha ya kikristo

Papa Francisko amesema kuwa, lakini hata Yesu kama mti na matawi yake anahitaji sisi. Na labda inaweza kushangaza, kusema hivyo na kwa maana hiyo ni kujiuliza, ina maana gani kusema Yesu ana haja nasi? Yeye anahitaji ushuhuda wetu. Tunda mbalo tunapaswa kutoa kutoka kwetu ni ushuhuda wa maisha ya kikristo. Baada ya Yesu kupaa kwenda kwa Baba, ilibaki kazi ya wafuasi ambayo ni kazi yetu ya kuendelea kutangaza Injili, kwa maneno na matendo. Kwa kukaa karibu sana na Kristo, tunapokea zawadi za Roho Mtakatifuna kwa namna ambayo tunaweza kufanya vema kwa jirani na kwa jumuiya na Kanisa. Mti mwema unatambuliwa kwa matunda yake. Maisha Mema ya Kikristo yanatoa ushuhuda kwa Kristo. Na Je ni jinsi gani ya kuweza? Yesu anasema :“Ninyi mkikaa ndani yangu, na maneno yangu yakikaa ndani yenu, ombeni mtakalo nanyi mtatendewa” (Yh 15,7). Hiyo kweli ndiyo habari na uhakika kuwa kile abacho tutaomba tutapewa. Kuzaa matunda katika maisha yetu kunategemeana na sala.

Kupeleka ulimwenguni matunda ya upendo na amani

Tunaweza kuomba na kufikiria kama Yeye, kutenda kama Yeye, kutazama ulimwengu kama Yeye na kuwapenda kaka na dada, kunzia maskini na wanaoteseka kama alivyofanya Yeye na kuwapenda kama  moyo wake na kutoa matunda mengi  katika ulimwengu, ya wema, matunda ya upendo na matunda ya amani. Papa amehitimisha kwa kuomba kwa njia ya maombezi ya Bikira Maria. Yeye alibaki daima ameungana kabisa na Yesu na kutoa matunda mengi. Atusaidie Yeye kubaki katika Kristo, katika moyo wake , katika neno lake, kwa kushuhudia Bwana Mfufuka katika ulimwengu.

TAFAKARI YA PAPA DOMINIKA YA 5 YA PASAKA

 

 

02 May 2021, 13:26

Sala ya Malkia wa Mbingu ni nini?
 

Utenzi wa Malkia wa Mbingu ni kati ya tenzi nne za Bikira Maria (nyingine ni:Tunakimbilia Ulinzi wako,  Salam Malkia wa Mbingu, Salam Malkia). Kunako mwaka 1742, Papa Benedikto XIV alipoandika kwamba, waamini wasali Sala ya Malkia wa Mbingu wakiwa wamesimama, kama alama ya ushindi dhidi ya kifo, wakati wa Kipindi cha Pasaka, yaani kuanzia Domenika ya Ufufuko wa Bwana hadi Sherehe ya Pentekoste. Hii ni Sala ambayo husaliwa mara tatu kwa siku kama ilivyo pia Sala ya Malaika wa Bwana: Asubuhi, Mchana na Jioni ili kuweka wakfu Siku kwa Mwenyezi Mungu na Bikira Maria.

Utenzi huu kadiri ya Mapokeo ulianza kutumika kunako karne ya VI au Karne X, lakini kuenea kwake kunaanza kujitokeza katika nyaraka mbali mbali kati kati ya Karne ya XIII, ilipoingizwa kwenye Kitabu cha Sala za Kanisa cha Wafranciskani. Hii ni Sala inayoundwa na maneno mafupi manne yanayohitimishwa na Alleluiya na sala ya waamini wanaomwelekea Bikira Maria, Malkia wa mbingu, ili kufurahia pamoja naye kuhusu Fumbo la Ufufuko wa Kristo Yesu.

Papa Francisko tarehe 6 Aprili 2015 wakati wa Sala ya Malkia wa Mbingu, siku moja baada ya Sherehe ya Pasaka, aliwashauri waamini kuwa na moyo wa furaha wanaposali sala hii. “Tunamwendea Bikira Maria, tukimwomba afurahi, kwa sababu yule Mwanaye mpendwa aliyekuwa amemchukua mimba amefufuka kweli kweli kama alivyosema; tunajiaminisha kwa sala na maombezi ya Bikira Maria. Kimsingi furaha yetu ni mwangi wa furaha ya Bikira Maria kwani ndiye aliyetunza na anaendelea kutunza matukio mbali mbali ya maisha ya Yesu. “Tusali sala hii kwa furaha ya kuwa waana wa Mungu ambao wanafurahi kwa sababu Mama yao anafurahi”

 

Sala ya Malaika wa Bwana/ Malkia wa Mbingu ya hivi karibuni

Soma yote >