Papa Francisko:tujifunze kutoka kwa Mtakatifu Yosefu
Na Sr. Angela Rwezaula – Vatican.
Mara baada ya katekesi ya Papa Francisko akiwa katika Maktaba ya Kitume, Jumatano tarehe 9 Desemba 2020, katika salam kwa waamini kwa lugha mbali mbali, Papa amejikita kuelekeza kiini cha maisha ya Kanisa. Na zaidi amejikita kuzama mwaka wa Mtakatifu Yosefu. Papa amesema “ Patris Corde" yaaani "moyo wa Baba” ndiyo kichwa cha Barua ya Kitume ambayo inajikita kufafanua Mtakatifu Yosefu ambayo inaangazia miaka 150 tangu kutangazwa kuwa Msimamizi wa Kanisa la Ulimwengu. Barua hiyo inatoa ufupisho wa maisha yake na utume wake. Mungu alimkabidhi tunu zenye thamani kuu Yes una Marian a yeye alijibu kwa imani kuu, ujasiri, upendo na moyo wa ubaba. Tumwombwa ulizi wake juu ya Kanisa katika wakati huu, na tujifunze kutoka kwake kufanya dima kama yeye kwa unyenyekevu na mapenzi ya Mungu.
Malekezo ya kupokea Msamaha wa dhambi katika mwaka wa Mtakatifu Yosefu
Ikumbukwe kwamba Papa Francisko amechapisha Barua yake ya kitume inayomhusu kwa Baba mlinzi wa Yesu, na kwa maana hiyo kusindikiza Mwaka Maalum wa Mtakatifu huyo ambao umeanza tangu tarehe 8 Desemba utafungwa manmo tarehe 8 Desemba 2021. Kutokana na hilo, Hati ya kutoka Idara ya Kitume kuhsu Msamaha wa dhambi iliyoridhiwa na Papa, inatoa maelekezo muhimu ya uwezekano wa kupokea katika kipindi hicho msamaha maalum kufuatia na Mwaka Maalum wa sura ya Mtakatifu Yosefu, lakini kwa kufuata hali zake zinazotakiwa kama vile kufanya sakramenti ya kitubio, kupokea ekaristi na kusali kwa ajili ya nia za Baba Matakatifu.
Mtakatifu Yosefu amependwa na watu wengi katika historia
Kwa nafasi yake ya historia ya Kanisa, Papa anakumbusha katika Barua ya Patris corde, kwamba Mtakatifu Yosefu ni baba ambaye daima amependwa na wakristo, kama inavyo jionesha ulimwenguni kote ambapo amewekwa kuwa msimamizi wa makanisa mengi, taasisi mbali mbali za kidini, jumuiya mbali mbali za kidini, vyama vya kitume, makundi ya kikristo ambayo yanaongozwa na tasaufi yake na watakatifu wengi ambao wamefanya ibada kuu ya Mtakatifu huyo.
Kwa bahati mbaya wapo watoto wengi ambao ni kama yatima
Mtakatifu Yosefu kwa maana hiyo ni mfano wa baba. Kwa bahati mbaya, Papa anasema katika Waraka wa Kitume Patris corde, watoto mara nyingi wanaonekana kuwa yatima wa baba, wa baba wenye uwezo wa kumfundisha mtoto uzoefu wa maisha, bila kumshikilia au kummiliki, badala yake kumfanya awe na uwezo wa kuchagua, wa kuwa uhuru, na ili kuondoka.
Mtakatifu Yosefu alikweka katikati Yesu na Maria katika maisha yake
Alitambua kwa kina kutoweka katikati maisha yake binafsi bali kwa ajili ya Yesu na Maria. Papa Francisko kwa kusisitiza zaidi sura ya Mtakatifu huyo amefafanua kwamba "Ulimwengu leo hii unahitaji baba, wa kukataa mabwana na kwamba, kukataa wale ambao wanataka kutumia miliki ya mwenzake kwa kujaza utupu wao wenyewe; kukataa wale ambao wanachanganya mamlaka na ubabe, huduma na utumishi, mapambano na dhuluma, upendo na ustawi, nguvu na uharibifu. Kiukweli kila wito wa kweli umezaliwa kutoka na zawadi binafsi na hivyo hatuwezi kukubali kuacha ziendelea mantiki za kuwatesa kwa kwa sadaka.