Tafuta

Maandamamo ya vijana nchini Nigeria Maandamamo ya vijana nchini Nigeria 

Wasiwasi na maombi ya Papa kwa ajili ya Nigeria!

Papa Francisko ameonesha wasiwasi mkubwa uliopo hasa kwa kile kinachoendelea nchini Nigeria mahali ambapo kwa siku hizi mivutano mingi inaendelea kati ya vyombo vya dola na maandamano ya vijana.

Na Sr. Angela Rwezaula – Vatican

Ninafuatilia kwa wasiwasi hasa habari inayokuja kutoka Nigeria. Ndivyo Papa Francisko ameanza mara baada ya sala ya Malaika wa Bwana  akiwaeleza waamini na mahuaji waliounganika katika uwanja wa Mtakatifu Petro Vatican, na hasa kufuatia na mivutano ya ulimwengu hasa kwa  upande wa mapigano ya hivi karibuni kati ya polisi na waandamanaji vijana nchini humo. Papa amesema tuombe kwa Bwana ili kila aina ya vurugu iepukwe kila wakati katika kutafuta mara kwa mara maelewano ya kijamii kwa njia ya kuhamasisha  haki na wema wa wote.

Matukio ya mwezi huu Oktoba katika nchi ya Afrika inayoangalia Ghuba ya Guinea

Vuguvugu la maandamano lilianza mapema mwanzoni mwa mwezi  Oktoba, baada ya video kwenye mitandao ya kijamii kuenea ikioonyesha mawakala wa SARS kumuua kijana katika mji wa kusini mwa Ughelli  nchini humo mnamo tarehe 3 Oktoba, lakini mamlaka ya Nigeria inasema video ilikuwa ya uwongo. Mtu aliyetengeneza video hiyo alikamatwa na kuongeza hasira ya waandamanaji. Kwa namna ya pekee  kuna maandamano dhidi ya matumizi ya nguvu na polisi, hasa na Kikosi Maalum cha Kupambana na Ujambazi (SARS), vitengo ambavyo vimeshutumiwa kwa miaka mingi kuhusu ukiukaji mkubwa wa haki za binadamu ambao waandamanaji wanataka kukomeshwa. Hata hivyo pia  waandamanaji wameanza kutoa wito wa kuwepo mageuzi kwa jumla katika nchi hiyo.

25 October 2020, 15:37