Tafuta

2020.08.13 Kikundi cha watawa wa Brazil mjini Roma 2020.08.13 Kikundi cha watawa wa Brazil mjini Roma 

Papa Francisko:Ili kuhudumia kwa furaha kazia mtazamo wa Yesu!

Papa Francisko amewaandikia watawa wa kike na kiume nchini Brazil ambao tarehe 16 wameanza Wiki ya Maisha ya kitawa kwamba ili kuwa zawadi kwa wengine na kuhudumia kwa furaha lazima kukazia macho kwa Yesu,vinginevyo ni hatari ya maono ya mambo ya kidunia.

Na Sr. Angela Rwezaula- Vatican

Maisha ya kitawa ni suala la kuwa na mtazamo wa macho. Kuwa katikati ya watu, mtawa anaweza kuishi utume wake akiwa na mtazamo wake  kwa Mungu au wa  ulimwengu. Suluhisho la kutopuuzwa ni sawa sawa  na la siku zote daima hasa katika  kutoa kipaumbele cha sala. Ndivyo Papa Francisko anaeleza katika barua aliyotuma kwa Baraza la watawa  nchini  Brazil, chombo  ambacho kimeandaa Wiki ya Maisha ya Kitawa katika nchi hiyo kuanzia tarehe 16 hadi 22 Agosti pia kupitia majukwaa ya kidigitali.

Wito katika furaha

Hata hivyo Papa Francisko kiukweli alianza jana,  Jumapili tarehe 16 Agosti 2020 alipotamka “mbele!" kwa kuwageukia kikundi cha watawa waliokuwa wamekusanyika katika uwanja wa Mtakatifu Petro wakiwa wameshika bendera ndani ya umati mkubwa wa mahujaji na waamini.  Mwakilishi katika jitihada za  kufuatilia kazi hiyo kutoka Roma anaendelea kwa maelfu ya watawa na waamini wa mashirika  mengi yaliyopo huko Brazili ambayo Papa Francisko amewaomba  kuwa na ukweli wa maisha, akikumbuka, kwamba safari ya wito ina asili yake katika uzoefu wa kujua kuwa wamependwa na Mungu  na kwamba wito ni furaha na hivyo  hupatikana tu katika zawadi ya kujitoa binafsi kwa wengine.

Kuishi ili kutumikia

Kwa upande mwingine Papa Francisko  anatazama mbele ya  kukabiliana na changamoto zilizowekwa na jamii ya sasa, ambayo inaendelea kuleta mabadiliko ya wakati na kusema kuwa  “lazima tuwe macho ili kuepusha vishawishi vya kuwa na maono ya kidunia, ambayo yanatuzuia kuona neema ya Mungu kama mhusika mkuu wa maisha na kutuongoza kwenda kutafuta mbadala wowote ule”. Udhibitisho uliobora zaidi wa kishawishi hiki  anasema Papa, ni kutoa kipaumbele cha sala katikati ya shughuli zetu zote na hakika kwamba wale ambao wanakazia mtazamo wao kwa Yesu wanajifunza kuishi  kwa ajili ya kutumikia.

Na moyo wa Mungu

Katika ujumbe huo Papa Francisko aidha  anatoa swali la kujiuliza na ambalo ni sawa na lile alilokuwa amekwisha toa  na kuwakumbusha :Nilipendekeza katika Barua ya Kitume ya mwaka wa 2014 kwa watawa, kwamba  je  Yesu ndiye upendo wa kwanza na wa pekee, kama tulivyopendekeza wakati tulikuwa tukitoa viapo wakati wa nadhiri zetu? “Ikiwa tutafanya hivyo  tu,  anahitimisha Papa, tutakuwa na uwezo kama jukumu letu, kumpenda kweli kila mtu ambaye tunakutana naye kwenye safari yetu, kwa sababu tutakuwa tumejifunza kutoka kwake ni nini maana ya upendo na jinsi ya kupenda. Tutajua jinsi ya kupenda, kwa sababu tutakuwa na moyo wake”.

17 August 2020, 14:19