Papa Francisko:uhuru wa Kanisa katika kuhudumia nchi za Ethiopia na Eritrea!
Na Sr. Angela Rwezaula – Vatican
Papa Francisko tarehe 11 Januria 2020 amekutanta na Jumuiya ya Kiethiopia wakiwa katika maadhimisho ya Jubilei ya miaka 100 tangu uwepo wa Taasisi ya Kipapa ndani ya Mji wa Vatican. Ametoa salam kwa Maaskofu kutoka Ethiopia na Eritrea na miongoni mwao wakiwepo maaskofu wakuu wawili Kardinali, Berhaneyesus, Askofu Mkuu Menghesteab Tesfamariam, M.C.C.I. wa Jimbo Kuu katoliki la Asmara nchini Eritrea, jumuiya ya wanafunzi na viongozi wakuu wa mashirika kwa namna ya pekee Gombera na Makamu wake, watawa ambao wanatoa huduma katika katika taasisi hiyo ya kipapa na wafanyakazi walei. Salam pia kwa Kardinali Leornardo Sandri, Rais wa Baraza la Kipapa la Makanisa ya Mashariki na Askofu Basil na kuwashukuru Baraza la Kipapa la Makanisa ya Mashariki linaloshughulikia Taasisi hiyo. Papa amewashukuru wafadhili na kuwa na utambuzi wa namna ya pekee kwa ukarimu wao. Jumuiya ya watawa wakapuchini, wakiwepo Mkuu wa shirika hilo na wawakilishi wa Taasisi ya Kipapa ya nchi za Mashariki na idadi kubwa ya mapdre na mafrateli wa Ethiopia na Eritrea.
Miaka 100 ya historia ya uwepo wa waethiopia mjini Vatican
Papa ameanza kueleza historia ya uwepo wa Waethiopia katika kuta za Vatican na wakiwa ni jumuiya ya kwanza kikaribishwa na kuendelea na ukarimu huo kwa miaka 100 sasa wakipeleka mbele neno ukarimu. Katika Kaburi la Mtume Petro kwa karne nyingi wamepata nyumba na ukarimu kama watoto kutoka mbali ya Roma na kama kuwa na ukaribu wa imani ya mitume katika kukiri Yesu Kristo. Na Maneno mazuri ya kueleza hivyo, Papa ametaja kuwa yanatoka kwa kwa Mmonaki mkubwa Tesfa Sion, Petro wa Ethiopia ambaye amezikwa katika Kanisa la Mtakatifu Stefano wa Ethiopia, mahali ambapo wao kwa siku mbili nwaadhimisha Liturujia zao. Yeye alisema: “mimi ni mwethiopia, mhujaji kutoka mahali na kwenda mahali(…). Lakini hakuna eneo zaidi ya Roma nimewahi kupata utulivu wa roho na mwili; utulivu wa roho kwa sababu hapa kuna imani ya kweli; na utulivu wa mwili kwa sababu hapa nimepata Mfuasi wa Petro ambaye anatusaidia katika mahitaji yetu”. Mmonaki huyo aliweza kutajirishwa na hekima yake ndani ya makao makuu ya Roma na katika kujikita k kutafsiri na kutangaza Biblia ya Agano jipya katika lugha ya kiethiopia, Papa Francisko amefafanua.
Wanafunzi mapadre wadumishe utajiri wa historia ya nchi yao watakaporudi kwao
Papa Francisko akiendela na hutuba yake amewaangazia wanafunzi, mapadre kutoka Ethiopia na Eritrea, ambayo anasema ni Makanisa mawili yaliyoungana kwa utumaduni unaofanana, na kwa hiyo anawaomba leo hii wapeleke katikati yao ule utajiri wa historia ya nchi zao hasa wa kuendeleza utamaduni wa kizamani na kuuishi kwa pamoja kati ya wanaume na wanake unaotokana na dini ya kiyahudi na ile ya kiislam, zaidi ya upamoja wa ndugu wengine wengi wa Kanisa la Kiorthodox Tewahedo. Aidha Papa amekumbuka jinsi alivyoweza kukutana mjini Roma na Patriaki Mathiasi wa Ethiopia ambaye amemtumia salam kindugu.
Fursa ya kuwakumbuka ndugu wengi wa Ethiopia na Eritrea wanaoteseka na umaskini na vita iliyopita
Papa Francisko amesema, kwa kukutana nao, umempa hta ya kukumbuka ndugu wengi, kaka na dada wa Ethiopia na Eritrea ambao wanaishi katika umaskini na zaidi miezi michache iliyopita walikuwa wanaishi vita na misuko suko, ambayo kwa kuhitimisha kwake ni shukrani kwa Bwana na wale ambao katika nchi wamekuwa mstari wa mbele katika harakati za mktadha wa amani na mapatano. Anawaombea sehemu zote mbili kutokana na uchungu waliouishi na kwamba usiweze kurudiwa tena mgawanyiko kati ya kabila na kati ya nchi katika mizizi yao inayowaunganisha. Kwa njia hiyo wanaweza kweli kuelimisha na kukuza zawadi ya Mungu kwa waamini ambao watakabidhiwa na kuhudumia majeraha ya ndani na nje ambayo wataweza kukutana na kutafuta kusaidia michakato ya mapatano na kwa ajili ya watoto endelevu na kizazi cha vijana katika nchi zao.
Kanisa la Ethiopia na Eritrea lihakikishiwe uhuru wa kuhudumia kwa ajili ya ustawi wa wote.
Papa Francisko amewatia moyo wa kuhifadhi tunu msingi za utamaduni wa Kanisa, na daima wakiungana na upeo wa kimisionari. Ni matashi mema kwamba Kanisa katika mataifa yao mawili yanaweza kuhakikishiwa ule uhuru wa kuhudumia kwa ajili ya ustawi wa wote, ikiwa ni kuruhusu pia wanafunzi waweze kwenda na kumalizia masomo yao Roma au sehemu nyingineyo, wakati wakilinda Taasisi za elimu, afya na hduma zote za utunzaji, kwa uhakika kwamba, Wachungaji na waamini wanatamani pamoja na wengine kuchangia wema na matarajio ya mataifa yao. Kama watoto wa Makanisa ya Ethiopia na Eritrea, wazidi kumpenda Mtakatifu Bikira Maria Mama wa Mungu, ambaye kama utamaduni wao wa kumwita Mama Maria ( Resta Maryam feudo” na katika kila mwezi wanayo liturujia iitwayo (Kidna Mehrat) maana yake (mapatano ya huruma) watambue kumkabidhi kila maombezi na kila sala. Na kwa maana hiyo katika sala hizo wasisahau kumwombea hata Papa.