Papa Francisko:kwa mfano wa Yesu kuweni karibu na ndugu wote na kujenga dunia ya haki!
Mara baada ya katesi yake Papa tarehe 15 Januari 2020 iliyokuwa inahusu safari ya mwisho ya Paulo ambayo ilikuwa ni Roma, kwa mujibu wa Kitabu cha Matendo ya mitume amesalimia mahujaji wote kutoka Italia na ulimwengu mzima. Kwa namna ya pekee watawa wa Kifransiskani wa Alcanterine ambao wanafanya Mkutano wao mkuu na kuwatia moyo ili waweze kuweka karama yao katika huduma yao ya kwanza kwa Kanisa.
Aidha mahujaji wengi wa makundi mengi ya kutoka pande zote za Dunia ambapo hakusahau kama kawaida yake vijana, wazee, wagojwa na wanandoa wapya . Anawaomba wafungue mioyo yao katika mahitaji ya Kanisa kwa kufuata mfano wa Yesu ili wawe karibu na ndugu na wakati huo huo ili kujenga dunia yenye kuwa na haki zaidi.