Tafuta

Askari wa Ukraine akilia machozi. Askari wa Ukraine akilia machozi. 

Ukraine:Maaskofu wa Ukraine wanakutana na Rais Zelensky wakiwa na wasiwasi!

Maaskofu wamekuwa na wasiwasi kuhusu uwezekano wa mapadre wao kuhamasishwa katika uwanja wa kijeshi kwa njia hiyo walikuana na Rais Volodymyr Zelensky ltarehe 2 Aprili 2024.Katika taarifa kutoka katika Tovuti ya Baraza la Maaskofu: ““uuangalifu hasa ulitolewa kwa suala la uwezekano wa uhamasishaji wa mapadre kama askari.”

Na Angella Rwezaula – vatican.

Katika ujumbe wa maaskofu wa Kanisa Katoliki la Kilatini na Makanisa ya Kiprotestanti ya Ukraine wamekutana na Rais Volodymyr Zelensky ltarehe 2 Aprili 2024. Katika mkutano huo - ambao ulitangazwa na Baraza la Maaskofu wa Ukraine - Waliokuwapo ni:  askofu Pavlo Honcharuk wa Kharkiv-Zaporizhsky, askofu Stanislav Shirokoradiuk wa Odessa-Simferopol, askofu Leon Dubravskyi wa Kamianets-Podilskyi, askofu Mykola Luchok wa Mukachevo, askofu Vitaly Skomarovskyi wa Kyiv-Zhytomyr.

Matatizo makubwa ambayo yanaweza kujitokeza

Mkutano katika muundo  kama huu ulifanyika kwa mara ya kwanza. Kulingana na tovuti ya Kanisa Katoliki la Kiukreni, libabainisha kuwa “uuangalifu hasa ulilipwa kwa swali la uwezekano wa uhamasishaji wa mapadre kama askari.” Tulisisitiza kwamba ikiwa mapadre wa parokia au wale wanaohusika na sekta ya kibinadamu watahamasishwa, hasa Caritas na tarafa zake zote, basi matatizo makubwa yataanza. Ikiwa baadhi ya watu muhimu, na wakati mwingine hata wafanyakazi wenyewe, wataacha ibada hii na kupelekwa mbele,” alisema Askofu Vitaly Kryvytskyi, ambaye anaongoza Tume ya Mahusiano ya Kanisa na wa Jimbo katiliki la  Uaskofu wa Ukraine.

Kwa mujibu wa Ofisi ya Rais: shukrani kwa huduma 

Hata hivyo Ofisi ya Rais pia iliripoti juu ya mkutano huo kwenye tovuti yake, kwa lugha yaKiingereza. Rais Zelensky aliwapongeza wawakilishi wa makanisa katika hafla ya Pasaka, huku akiwatakia “ushindi wa Ukraine katika vita dhidi ya wavamizi wa Urusi. Hakika itakuja shukrani kwa askari wetu, watu wetu na maombi yenu ya dhati,” Zelensky alisema, kulingana na Ofisi ya Rais. Zelensky kisha walibainisha kuwa alionesha “shukrani kwa huduma ya makasisi wetu wa kijeshi. Shukrani kwenu, wanaume na wanawake wetu walio mbele, ambao wana fursa ya kuwasiliana na kuhisi msaada wenu.” Rais aliwahimiza wawakilishi wa Makanisa kudumisha uhusiano wa kimataifa ili kueneza habari za kweli kuhusu Ukraine  na uhalifu wa Warusi. “Baada ya yote, Kanisa lina ushawishi mkubwa kwa jamii, kwa viongozi wa serikali. Na kwa hivyo hii ni ishara muhimu sana kwetu kuhusu uungwaji mkono wa washirika wetu,” alisisitiza. Pia kwenye mkutano huo alikuwapo Valerii Antoniuk, mkuu wa Umoja wa Makanisa ya Kiinjili ya  na mshiriki wa Baraza la Makanisa na Mashirika ya Kidini ya Ukraine yote.

03 April 2024, 15:56