Tafuta

2024.01.07 Kardinali Brenes aliweka wakfu mapadre 9 katika kanisa Kuu la Managua, Nicaragua (6 Janyari  2024). 2024.01.07 Kardinali Brenes aliweka wakfu mapadre 9 katika kanisa Kuu la Managua, Nicaragua (6 Janyari 2024). 

Nicaragua,mapadre wapya 9 wawekwa wakfu.Wito mpya wa UN

Kardinali Brenes aliwaweka wakfu mapadre tisa huko Managua,huku Kamishna Mkuu wa Haki za Kibinadamu wa Umoja wa Mataifa akiiomba serikali ya Nicaragua kufichua mahali alipowekwa kizuizini Askofu Isidoro Mora wa Siuna:"wimbi jipya la kukamatwa kwa watu wa dini linadhoofisha haki ya kidini,huru,nguzo ya kila nchi ya kidemokrasia.”

Vatican News

Jimbo kuu la Managua nchini Nicaragua limepata mapadre wapya tisa waliowekwa wakfu mnamo tarehe 6 Januari 2024, katika maadhimisho ya Siku Kuu ya Epifania, yaani Tokeo la Bwana kwa kuongozwa na Askofu mkuu, Kardinali Leopoldo José Brenes Solórzano.Waamini wengi walishiriki kwa shangwe na hisia kali  katika ibada hiyo, iliyofanyika katika Kanisa Kuu la Managua.


Brenes: makuhani, mashahidi wa udugu

Katika mahubiri yake, Kardinali alimshukuru mwenyezi “Mungu kwa zawadi ya ajabu ya mapadre wapya, huku  akisema kwamba ukuhani si nguvu, bali utume na huduma. Mapadre ni watumishi na mashahidi, wanaoitwa kuishi ushirika na udugu,” alisema.

Mashemasi wakati wa litania ya watakatifu kabla ya kuwekwa wakfu wa kikuhani
Mashemasi wakati wa litania ya watakatifu kabla ya kuwekwa wakfu wa kikuhani

Wimbi la kukamatwa

Mapadre wapya waliwekwa wakfu katika wakati mgumu kwa Kanisa la Nicaragua. Ni tangu tarehe 20 Desemba 2023, ambapo mapadre wasiopungua 14, waseminari wawili na askofu Isidoro del Carmen Mora Ortega wa Siuna, walikamatwa na kutekwa nyara baada ya kumuombea Aslofu  Rolando José Álvarez Lagos, wa jimbo la Matagalpa na msimamizi wa kitume wa Jimbo katoliki la  Estelí  aliyehukumiwa kifungo cha miaka 26 jela bila kufikishwa mahakamani na bila sheria tangu mwezi Februari 2023. Katika jumuiya ya kikanisa  hata hivyo kuna wasiwasi, hasa, kwa mapadre waliotekwa nyara ambao wana matatizo ya kiafya, akiwemo Padre Ismael Serrano, paroko wa Mtakatifu  Mikaeli Mkuu na Padre Gerardo Rodrígues, padre wa Kanisa la Mama Safi wa Moyo , ambao wote ni  kutoka Jimbo kuu la Managua na ni wagonjwa na wanahitaji matibabu.


UN yatoa wito kwa serikali ya Nicaragua

Kwa upande wake, Ofisi ya Kamishna Mkuu wa Umoja wa Mataifa wa Haki za Kibinadamu kwa Amerika ya Kati (OACNUDH) amezindua wito mpya kwa serikali ya Nicaragua ili  kufichua kwa haraka mahali  ambapo AskofuMora,  ambaye ni “mwathirika wa kutoweka kwa lazima  anashikiliwa kwa siku 16, alipo.” Kwa kuficha habari hizi, kama inavyosemokea( si legge in un post su X )- “ Maisha yake yako hatarini.”

Litania kabla ya kuwekwa wakfu makunai 9 wa Managua nchini Nicaragua
Litania kabla ya kuwekwa wakfu makunai 9 wa Managua nchini Nicaragua

Tayari tarehe 28 Desemba Ofisi ya Kamishna Mkuu wa Umoja wa Mataifa wa Haki za Binadamu wa Amerika ya Kati (OACNUDH)ilikuwa imelaani “kutoweka kulazimishwa kwa Askofu Isidoro Mora na wimbi jipya la kukamatwa kwa watu wa kidini  ni kinyume na haki ya uhuru wa kidini, nguzo ya kila nchi ya kidemokrasia.” Kulingana na Kamishna Mkuu wa Umoja wa Mataifa wa Haki za Kibinadamu, Nicaragua inakwenda “kuongezeka” kutoka katika utawala wa sheria na “kutoka katika uhuru wa kimsingi” kwa kuwatesa “viongozi wa kisiasa na raia, washiriki wa Kanisa Katoliki, wanaharakati na waandishi wa habari” kwa “kesi zinazorudiwa mara kwa mara za kuwekwa kizuizini kiholela.”

Kardinali Brenes akiweka wakfu wa kikuhani kwa mapadre 9 wa jimbo la Managua,Nicaragua
Kardinali Brenes akiweka wakfu wa kikuhani kwa mapadre 9 wa jimbo la Managua,Nicaragua

Papa Francisko aliombea Maaskofu na mapadre walionyimwa uhuru

Hivi karibuni, mara baada ya sala ya Malaika wa Bwana kwa waamini na mahujaji waliofika katika Uwanja wa Mtakatifu Petro mjini Vatican, Baba Mtakatifu, alikuwa  amewaombea watu wa dini hao. Katika siku hiyo alisema: “Ninafuatilia kwa wasiwasi mkubwa kile kinachotokea Nicaragua, ambako Maaskofu na mapadre wamenyimwa uhuru wao. Nimawaeleza wao, familia zao na Kanisa zima nchini ukaribu wangu katika maombi. Pia ninawaalika ninyi nyote mliopo hapa na Watu wote wa Mungu kusali kwa bidii, huku nikitumaini kwamba ni kutafuta daima njia ya mazungumzo ili kuondokana na matatizo. Hebu tuiombee Nicaragua leo.”


Ikumbukwe kufikia sasa mamlaka ya Nicaragua haijathibitisha wala kukanusha kuzuiliwa kwa mapadre hao ambao waliripotiwa kutoweka.

09 January 2024, 14:25